Ng'wanamangilingili
JF-Expert Member
- Aug 22, 2015
- 5,778
- 4,859
FactHizo zama zilishapita, sijasikia wakiitwa mabeberu kwa miezi kama 9 sasa, hata Jamvi la Habari naona nao wamelisahau hilo neno
God is Good,View attachment 2046950===
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regina Hess, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa juhudi inazochukua kupambana na ugonjwa wa Uviko-19 ambazo zimezaa matunda kufuatia uwepo wa visa vichache vya ugonjwa huo vilivyorekodiwa wimbi lililopita.
Mhe. Hess amesema Serikali ya Ujerumani inaridhishwa na hatua mbalimbali ambazo zimechukuliwa na Tanzania katika kupamabana na Uviko-19, ikiwemo elimu kwa wananchi pamoja na kampeni ya uhamasishaji ya kuhakikisha watanzania wanapata chanjo ya UVIKO-19
Balozi Regina Hess ametoa pongezi hizo leo 16/12/2021 wakati akikabidhi msaada wa vifaa tiba, vilivyotolewa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la GIZ, kwa Mfamasia Mkuu wa Serikali na Uongozi wa MSD kwenye Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) yaliyoko Keko jijini Dar es salaam.
Vifaa hivyo vyenye thamani ya takribani shilingi bilioni mbili na laki tatu (2.330.958.072) vikijumuisha mashine za kusaidia kupumua 50 (ventilators)na mashine za kupima kiwango cha Oksjijeni ndani ya mwili zipatazo 5000 (pulse oximeters).
Balozi Hess ameongeza kwamba Serikali ya Ujerumani imekua ikishirikiana na itaendelea kushirikiana na Tanzania kwenye Nyanja mbalimbali za kimaendeleo, ikiwemo sekta ya afya, hasa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19, ambapo awali ilitoa msaada wa maabara zinazotembea kwa serikali ya Tanzania ili kurahisisha upimaji wa wagonjwa wa UVIKO-19.
Akipokea Vifaa hivyo kwa niaba ya Serikali, Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi, ameishukuru Ujerumani kwa kuendelea kusaidia Tanzania katika mapambano dhidi ya UVIKO-19, na kusema vifaa hivyo vitasaidia kwa kiasi kikubwa katika utoaji wa huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
“Tunaishukuru sana Serikali ya Ujerumani kwani msaada huu umekuja kwa wakati muafaka, hasa kipindi hiki ambacho dunia imeshuhudia mlipuko wa wimbi jipya la virusi vya Corona aina ya Omicron tutasambaza vifaa tiba hivi kwenye maeneo mbalimbali nchini, ili vikaongeze nguvu kwenye mapambano dhidi ya UVIKO-19” alisema Msasi.
Bw.Msasi amesisitiza kwamba Vifaa tiba hivyo vitasambazwa kwenye takribani vituo 500.
Mimi ni CHADEMA
Huyu mama si ndiye yule ambaye Naibu wake Kathrin Steinbrenner alikwenda kuteta na Mbowe Kisutu Mahakamani?Ujerumani wametusaliti kama Zitto
Wanatoaje Misaada wakati Mwenyekiti ana 'kesi' ya kubambikiwa na bado yupo mahabusu?
Halafu nyie mtasema SSH kamwaga mabilioni mapambano ya UVIKO19....wakati ni reciprocity ya German government Grant's....na nyie mjifunze kwa watoaji ndio maana huoni wakisema Olaf Schloz ...get it now is no longer Angel Markel...katoa billions kwa serikali ya Tanzania. They just mention serikali ya ujerumani.
Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Tanzania yetu bwana, magumashi ya kutosha yani kama vile tumekatwa vichwa,View attachment 2046950===
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regina Hess, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa juhudi inazochukua kupambana na ugonjwa wa Uviko-19 ambazo zimezaa matunda kufuatia uwepo wa visa vichache vya ugonjwa huo vilivyorekodiwa wimbi lililopita.
Mhe. Hess amesema Serikali ya Ujerumani inaridhishwa na hatua mbalimbali ambazo zimechukuliwa na Tanzania katika kupamabana na Uviko-19, ikiwemo elimu kwa wananchi pamoja na kampeni ya uhamasishaji ya kuhakikisha watanzania wanapata chanjo ya UVIKO-19
Balozi Regina Hess ametoa pongezi hizo leo 16/12/2021 wakati akikabidhi msaada wa vifaa tiba, vilivyotolewa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la GIZ, kwa Mfamasia Mkuu wa Serikali na Uongozi wa MSD kwenye Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) yaliyoko Keko jijini Dar es salaam.
Vifaa hivyo vyenye thamani ya takribani shilingi bilioni mbili na laki tatu (2.330.958.072) vikijumuisha mashine za kusaidia kupumua 50 (ventilators)na mashine za kupima kiwango cha Oksjijeni ndani ya mwili zipatazo 5000 (pulse oximeters).
Balozi Hess ameongeza kwamba Serikali ya Ujerumani imekua ikishirikiana na itaendelea kushirikiana na Tanzania kwenye Nyanja mbalimbali za kimaendeleo, ikiwemo sekta ya afya, hasa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19, ambapo awali ilitoa msaada wa maabara zinazotembea kwa serikali ya Tanzania ili kurahisisha upimaji wa wagonjwa wa UVIKO-19.
Akipokea Vifaa hivyo kwa niaba ya Serikali, Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi, ameishukuru Ujerumani kwa kuendelea kusaidia Tanzania katika mapambano dhidi ya UVIKO-19, na kusema vifaa hivyo vitasaidia kwa kiasi kikubwa katika utoaji wa huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
“Tunaishukuru sana Serikali ya Ujerumani kwani msaada huu umekuja kwa wakati muafaka, hasa kipindi hiki ambacho dunia imeshuhudia mlipuko wa wimbi jipya la virusi vya Corona aina ya Omicron tutasambaza vifaa tiba hivi kwenye maeneo mbalimbali nchini, ili vikaongeze nguvu kwenye mapambano dhidi ya UVIKO-19” alisema Msasi.
Bw.Msasi amesisitiza kwamba Vifaa tiba hivyo vitasambazwa kwenye takribani vituo 500.