Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,752
- 7,861
...mambo mengine tukisema ni ujinga wa mwafrika, tunakosea. Huu wizi wa vifaa vya hospitali, mfano huu wa kuiba mashine ya saratani, ni ujinga wa mtanzania.
hii ni Inside job, inayowahusisha wafanyakazi wote... walinzi, watumiaji (lab technician), wabebaji, dereva aliyehusika, middleman 'aliyechonga huo mchongo', pamoja na huyo mnunuzi!... WAFUNGWE WOTE wakipatikana!!!
hii ni Inside job, inayowahusisha wafanyakazi wote... walinzi, watumiaji (lab technician), wabebaji, dereva aliyehusika, middleman 'aliyechonga huo mchongo', pamoja na huyo mnunuzi!... WAFUNGWE WOTE wakipatikana!!!
Mashine tiba ya kansa yaibwa Ocean Road
2009-01-31 10:50:32
Na Tamara Manyata
Zaidi ya wagonjwa 170 hawatapata matibabu ya saratani (kansa) katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es salaam baada ya mtambo wa kuendeshea mashine za kuchoma mionzi kuibwa hospitalini hapo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka taasisi hiyo, kuibiwa kwa kifaa hicho kunafanya shughuli nzima ya uchomaji wa mionzi na tiba ya saratani kusimama.
Akielezea tukio hilo, Mkurugenzi wa Ttaasisi hiyo, Dk Twalib Ngoma, alisema kuwa mtambo huo uliibiwa usiku wa kuamkia jana huku kukiwa na takribani wagonjwa 170 wanaohitaji tiba inayotolewa na mitambo hiyo.
Kwa mujibu wa Dk. Ngoma, mtambo huo hapa nchini upo Ocean Road tu.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Alisema kuwa Jeshi la Polisi linawashikilia watumishi sita kutoka Taasisi hiyo kwa ajili mahojiano zaidi.
Aidha, huduma za tiba ya saratani zitaendelea baada ya kifaa hicho kupatikana au kununuliwa kingine.
Kifaa hicho pamoja na mashine ya mionzi kinagharimu kiasi cha Sh bilioni moja.