ulimi waupanga
JF-Expert Member
- Aug 31, 2014
- 493
- 1,223
Miaka ya 1800's walikuwepo ndugu wawili kwa Majina ya KEMPANJU NA KASSA, huko mkoani Kagera wilaya ya Bukoba( Misenyi kwa sasa).
Imenichukua mwendo wa lisaa kutoka Bukoba mjini mpaka kata ya Buyango, kijiji Lwamachu kitongoji Nyakihanga ambapo ndiko haswa nyumbani kwa ayo majina mawili ambayo moja wapo( KEMPANJU) ndiyo chanzo cha safari yangu baada ya kusikia kuwa huyo mtu alikuwa na nguvu kubwa sana za kimizimu baada ya kifo chake.
Baada ya kufika apo kijijini lwamachu nikaelekezwa kwa Kempanju, kwa mwonekano ilionekana ni familia yenye heri kimaisha lakini ikiwa ina watu wachache. Baada ya kujitambulisha kwa mwenyeji wangu ambaye alikuwa ni mama wa makamo na kumwambia kuwa nahitaji kufahamu machache kuhusu huyu mtu KEMPANJU alionekana kusutuka na kunijibu " Mwanangu mimi apa ni mwolewaji tu wala hapa ulipo siyo Nyaruju( Ikuru) ya huyo Mzee" nikaendelea kumdadisi akanambia" Nitakuongoza mpaka kwa Mzee Marceli huyu ndiye atakupatia taarifa zote".
Baada ya mwendo kama Nusu kirometa katikati ya Mashamba ya Migomba tunafika Kwenye familia moja, anaishi Mzee mmoja na vijana watatu, kumbe huyu ndiye Mzee Marceli. Baada ya kujitambulisha kwingi na maswali Lukuki Mzee anakubali kunimegea historia ya huyu mtu KEMPANJU. Anasema:
KEMPENJU NA KASSA walikuwa ni ndugu wa damu wajukuu wa mtu mmoja aliyekuwa anaitwa KASHASHA Mwenye hasili ya Mpololo Uganda aliyehamia Bukoba kipindi cha mfalme mmoja wa Kiziba aliyeshindwa kupata mtoto akashauliwa kwamba Uganda kuna mganga anaweza kumsaidia. Hapo ndo KASHASHA NA Nduguye KALENGE walipopata nafasi ya kuvuka mto Kagera na kuingia Kiziba kwa ajili ya kumtibu mfalme. Baada ya kazi yao kufanikiwa ndipo mfalme akawakabidhi eneo la kuishi mmoja akapewa kata ya Kitobo uyo KALENGE, na KASHASHA akapewa Kantale kata ya Bwanjai.
Baada ya KASHASHA Kuongezeka sana na kusitawi, vizazi vyake vilianza kujitanua, ndipo mmoja kati ya watoto wake alihamia kijiji jirani cha Lwamachu kitongoji Nyakihanga apo ndo akazaa watoto wawili KEMPANJU NA KASSA. Huyu KEMPANJU akalithi mikoba ya Uganga ya Babu yake KASHASHA na kustawi sana katika fani ya Uganga na utabiri.
Mzee Marceli anaendelea kusimulia kwamba" Maisha yaliendelea vizuri apo kijijini kati ya hawa ndugu wawili huku wakiishi maisha ya kijamaa, kiasi kwamba KASSA akichinja Mbuzi au Ng'ombe lazima nusu ipelekwe kwa Kaka yake KEMPANJU na huyu naye hivyo hivyo. Anasema, KEMPANJU katika Uganga wake alikuwa na mwiko(ekihagale) mmoja ambao ni kutokula chakula kilichoguswa na mtu mwenye ( ebishoona) kwa tafsiri hisiyo rasmi sana huu ni ugonjwa kama Ukurutu.
Shida ilikuja ambapo siku moja KASSA alichinja mbuzi kama kawaida yao akamwagiza mwanae akate nyama kwa ajili ya kumpelekea KEMPANJU, huyu mwanaye KASSA alikuwa na mke ambaye kwa siku alikuwa ameugua huo ugonjwa wa Ebishoona lakini akawa amejificha maana kipindi hicho ilikuwa kama laana mtu kuonekana na ugonjwa huo. Kwahiyo huyo kijana wa KASSA naye akamwambie mke wake akate nyama kama alivyoagiza Mzee KASSA iende kwa KEMPANJU.
Huyu mama mwenye Ugonjwa akafanya kama alivyoagizwa na mumewe na mboga ikapelekwa kwa KEMPANJU, KEMPANJU bila kujua kama ile nyama imeguswa na mtu najisi akapikiwa na kula, alipokula ile nyama hapo hapo akafariki Dunia. Kuanzia hapo ndipo Mizimu( enchweke) ya KEMPANJU ilipoanza sarakasi zake.
Anaendelea kusimlia kuwa" Ile Siku wamemaliza kumzika Mzee KEMPANJU, siku iyo iyo wazee wote walipandisha roho vichwani na kuanza kunena kwa sauti ya Marehemu akilia na kusema kwa ukali" watata wakunyisile?" Yaani (ndugu yangu wewe ndiye ungeniua?), ikabidi KASSA adakie na kuuliza maana yeye alikuwa hajapandwa na roho ya Marehemu ( enchweke), watata nakwita ntai? Yaani ( ndugu yangu nimekuua vipi), Ile roho kwa vinywa vya wale wazee ikazidi kunena " watata nomanya okwo ntalya bihagalo, kyonkai wandetela ebihagalo byanyita" yaani( ndugu yangu unajua sili najisi lakini wewe umeniletea najisi nimekula na kufariki).
Hapo hapo ile roho kupitia vinywa vya wale wazee ikasema " kuanzia Leo naweka uhasama kati ya KEMPANJU na KASSA aliye wa KASSA akikanyaga aridhi ya KEMPANJU atakufa, hata mbuzi au kuku aliye wa KASSA hasikanyage kwa KEMPANJU...........!
Itaendelea....................!
Imenichukua mwendo wa lisaa kutoka Bukoba mjini mpaka kata ya Buyango, kijiji Lwamachu kitongoji Nyakihanga ambapo ndiko haswa nyumbani kwa ayo majina mawili ambayo moja wapo( KEMPANJU) ndiyo chanzo cha safari yangu baada ya kusikia kuwa huyo mtu alikuwa na nguvu kubwa sana za kimizimu baada ya kifo chake.
Baada ya kufika apo kijijini lwamachu nikaelekezwa kwa Kempanju, kwa mwonekano ilionekana ni familia yenye heri kimaisha lakini ikiwa ina watu wachache. Baada ya kujitambulisha kwa mwenyeji wangu ambaye alikuwa ni mama wa makamo na kumwambia kuwa nahitaji kufahamu machache kuhusu huyu mtu KEMPANJU alionekana kusutuka na kunijibu " Mwanangu mimi apa ni mwolewaji tu wala hapa ulipo siyo Nyaruju( Ikuru) ya huyo Mzee" nikaendelea kumdadisi akanambia" Nitakuongoza mpaka kwa Mzee Marceli huyu ndiye atakupatia taarifa zote".
Baada ya mwendo kama Nusu kirometa katikati ya Mashamba ya Migomba tunafika Kwenye familia moja, anaishi Mzee mmoja na vijana watatu, kumbe huyu ndiye Mzee Marceli. Baada ya kujitambulisha kwingi na maswali Lukuki Mzee anakubali kunimegea historia ya huyu mtu KEMPANJU. Anasema:
KEMPENJU NA KASSA walikuwa ni ndugu wa damu wajukuu wa mtu mmoja aliyekuwa anaitwa KASHASHA Mwenye hasili ya Mpololo Uganda aliyehamia Bukoba kipindi cha mfalme mmoja wa Kiziba aliyeshindwa kupata mtoto akashauliwa kwamba Uganda kuna mganga anaweza kumsaidia. Hapo ndo KASHASHA NA Nduguye KALENGE walipopata nafasi ya kuvuka mto Kagera na kuingia Kiziba kwa ajili ya kumtibu mfalme. Baada ya kazi yao kufanikiwa ndipo mfalme akawakabidhi eneo la kuishi mmoja akapewa kata ya Kitobo uyo KALENGE, na KASHASHA akapewa Kantale kata ya Bwanjai.
Baada ya KASHASHA Kuongezeka sana na kusitawi, vizazi vyake vilianza kujitanua, ndipo mmoja kati ya watoto wake alihamia kijiji jirani cha Lwamachu kitongoji Nyakihanga apo ndo akazaa watoto wawili KEMPANJU NA KASSA. Huyu KEMPANJU akalithi mikoba ya Uganga ya Babu yake KASHASHA na kustawi sana katika fani ya Uganga na utabiri.
Mzee Marceli anaendelea kusimulia kwamba" Maisha yaliendelea vizuri apo kijijini kati ya hawa ndugu wawili huku wakiishi maisha ya kijamaa, kiasi kwamba KASSA akichinja Mbuzi au Ng'ombe lazima nusu ipelekwe kwa Kaka yake KEMPANJU na huyu naye hivyo hivyo. Anasema, KEMPANJU katika Uganga wake alikuwa na mwiko(ekihagale) mmoja ambao ni kutokula chakula kilichoguswa na mtu mwenye ( ebishoona) kwa tafsiri hisiyo rasmi sana huu ni ugonjwa kama Ukurutu.
Shida ilikuja ambapo siku moja KASSA alichinja mbuzi kama kawaida yao akamwagiza mwanae akate nyama kwa ajili ya kumpelekea KEMPANJU, huyu mwanaye KASSA alikuwa na mke ambaye kwa siku alikuwa ameugua huo ugonjwa wa Ebishoona lakini akawa amejificha maana kipindi hicho ilikuwa kama laana mtu kuonekana na ugonjwa huo. Kwahiyo huyo kijana wa KASSA naye akamwambie mke wake akate nyama kama alivyoagiza Mzee KASSA iende kwa KEMPANJU.
Huyu mama mwenye Ugonjwa akafanya kama alivyoagizwa na mumewe na mboga ikapelekwa kwa KEMPANJU, KEMPANJU bila kujua kama ile nyama imeguswa na mtu najisi akapikiwa na kula, alipokula ile nyama hapo hapo akafariki Dunia. Kuanzia hapo ndipo Mizimu( enchweke) ya KEMPANJU ilipoanza sarakasi zake.
Anaendelea kusimlia kuwa" Ile Siku wamemaliza kumzika Mzee KEMPANJU, siku iyo iyo wazee wote walipandisha roho vichwani na kuanza kunena kwa sauti ya Marehemu akilia na kusema kwa ukali" watata wakunyisile?" Yaani (ndugu yangu wewe ndiye ungeniua?), ikabidi KASSA adakie na kuuliza maana yeye alikuwa hajapandwa na roho ya Marehemu ( enchweke), watata nakwita ntai? Yaani ( ndugu yangu nimekuua vipi), Ile roho kwa vinywa vya wale wazee ikazidi kunena " watata nomanya okwo ntalya bihagalo, kyonkai wandetela ebihagalo byanyita" yaani( ndugu yangu unajua sili najisi lakini wewe umeniletea najisi nimekula na kufariki).
Hapo hapo ile roho kupitia vinywa vya wale wazee ikasema " kuanzia Leo naweka uhasama kati ya KEMPANJU na KASSA aliye wa KASSA akikanyaga aridhi ya KEMPANJU atakufa, hata mbuzi au kuku aliye wa KASSA hasikanyage kwa KEMPANJU...........!
Itaendelea....................!