haha haaaKwasababu unajipenda sana, ukiumwa malaria wa pembeni yako atahisi huyu jamaa hamalizi nusu saa anarudisha jezi
Pole sana jomba!!!Nasikitika maisha haya sijui nampenda nani daah. Baba? Mama? Dada? Kaka? Sina jibu kabisa maana sina feeling na mtu yeyote hadi huwa najishtukia.
Tatizo malezi niliyopitia, ndio madhara ya kukulia ghetto na wazazi kutoishi pamoja.
Mama yangu ndiye tafsiri halisi ya upendo. Hata akifa, bado ataendelea kuishi ndani ya nafsi yangu. Nampenda sana mama yanguBabu mmoja aling’ng’ania kwenda mjini kwenye harusi ya mjukuu wake, pamoja na hali yake ya kiafya kuwa mbaya lakini alitaka hivyo. Alihudhuria na siku ya harusi baada ya sherehe alimuomba mjukuu wake aongee naye kabla hawajaenda honeymoon.
Watu walitaka asubiri kwanza lakini aliwaambia hapana, mjukuu aliitwa na alianza kuongea naye. “Mjukuu wangu najua sina muda sana ila kuna kitu nataka kukuambia, leo umeoa sitaki ufanye kosa kama nililofanya mimi na alilofanya Baba yako. Baba yako nilimfundisha kua wanawake si watu wa kuaminiwa na unapaswa kuamini familia kwanza.
Nilikosea na ndiyo maana leo pamoja na kuwa Bibi yako bado yupo lakini nakufa mpweke. Ukweli nikua mjukuu wangu mkeo ndiyo anapaswa kuwa namba moja kwako kwa kila kitu kwani huyo ndiyo mtu pekee ambaye utazeeka naye na utakufa pembeni yake.
Mimi nilimpenda Mama yangu kuliko Bibi yako, lakini leo hayupo, nikawapenda Dada zangu lakini leo wanakufa na waume zao, nikawapenda Kaka zangu lakini leo wanakufa na wake zao. Mtu pekee ambaye nilimdharau na kumnyanyasa ni Bibi yako na ndiye ambaye tumetelekezwa naye Kijijini.
Angalia Baba yako, walikua wakipendana sana na Baba zako wadogo lakini leo wako wapi, kila mmoja anakufa na wake. Hivyo mjukuu wangu kama ukimpenda mkeo sasa basi wakati mkiwa wazee hutakua ukijuta hasa ukikumbuka kuwa ulimtesa zamani kama mimi ninavyojuta sasa.
Mjukuu wangu mtu hazeeki na Mama yake, mwanaume ambaye huzeeka akiwa anaishi kwa Mama yake huyo si mwanaume ni Dung’uthi, mwanaume ambaye huzeekea akiwa anaishi kwa Dada yake huyo ni Zezeta na mwanaume ambaye huzeeka akiwa anaishi kwa Kaka yake huyo ni Kapuku ila ambaye huzeeka na mkewe huyo ndiyo Mwanaume.”
Babu alimaliza kuongea na kuwaruhusu wajukuu zake kwenda kusherehekea harusi yao. Siku tatu baadaye babu alifariki akiwa pembeni ya mkewe “Bibi”, mwanamke ambaye alitumia ujana wake wote kumnyanyasa. Maneno ya Babu yalitimia, alikufa pemeni ya mwanamke aliyekua akimnyanyasa na kumuona kama takataka.
Unampenda sana mama yako lakini tafadhali mkuu jiepushe na hiyo statement 'hata akifa ataendelea kuishi ndani ya nafsi yangu'....maana anaejua nani atatangulia mbele za haki kati yako na yeye ni Mola MwenyeweMama yangu ndiye tafsiri halisi ya upendo. Hata akifa, bado ataendelea kuishi ndani ya nafsi yangu. Nampenda sana mama yangu
Elewa maana ya neno "hata"Unampenda sana mama yako lakini tafadhali mkuu jiepushe na hiyo statement 'hata akifa ataendelea kuishi ndani ya nafsi yangu'....maana anaejua nani atatangulia mbele za haki kati yako na yeye ni Mola Mwenyewe
Nimeshauri tu mkuu, pole kama sija eleweka na samahaniElewa maana ya neno "hata"
Mapenzi ya mke ni unique kwakweli, Mungu Kaumba kamaliza paleNi kweli kabisa ujumbe mzuri sana Mama ana nafasi yake sana lakini mke pia ana nafasi mtu unayelala naye kitanda kimoja mtu ambaye ukiumwa yeye ndio anajua ahangaike na wewe
Kweli kabisa mkuu ndio mana msiba wa mke au mume na wazazi wa mume na mke unauma sana mmezoeana sana sana kulala na mtu kesho hayupo lazima uchanganyikiwe mpaka uje kusahau sio leoMapenzi ya mke ni unique kwakweli, Mungu Kaumba kamaliza pale
Mara nyingi nashuhudia wanaume wanalia kama watoto wadogo wanapoondokewa na wake zao kitu ambacho ni nadra kuona wakati wamefiwa na mzazi, yaani kwa kifo ch amzazi anaweza akajikazaKweli kabisa mkuu ndio mana msiba wa mke au mume na wazazi wa mume na mke unauma sana mmezoeana sana sana kulala na mtu kesho hayupo lazima uchanganyikiwe mpaka uje kusahau sio leo
Huu ndio ukweli mkuuMara nyingi nashuhudia wanaume wanalia kama watoto wadogo wanapoondokewa na wake zao kitu ambacho ni nadra kuona wakati wamefiwa na mzazi, yaani kwa kifo ch amzazi anaweza akajikaza