nguluvisonzo
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 515
- 71
Niliwahi kwenda kuulizia kazi ktk ofisi moja mjini aeusha, nilishangaa mkuu wa ofisi akaniuliza 'wani wewe ni mhaya', nikamwambia hapana akasema basi kama sio mhaya ondoka tu ndugu yangu. Taratiiiibu nikasepa mtoto wa kiume.......... Ni ngumu kuamini lakini hii thread ina kaukweli ambako huwezi kukatetea kwa hali historia ilivyoshape mambo. Napitapita humuhumu tu wakuuu!
samvulechole... hakuna hoja ambayo ni ngeni hapa.. madai ya makabila hayo kupendelewa hayakuanza leo! tangu mara tu baada ya uhuru kulikuwa na tuhuma hizo hizo.. so.. there is nothing there..! Hata hivyo hatari unayoweza kuleta siyo ukabila bali ubaguzi, kuwa kama mtu anatoka kwenye makabila hayo basi asipewe nafasi fulani kwa vile watu fulani wanadhani kuna ukabila! Nitakupa mfano, kuna wanasheria watatu wote ni maprofesa... kuna Prof. Mwakalindile (Sheria, uzoefu miaka 30), Prof. Mtimba (mmakua, uzoefu miaka 10, sheria), na Prof. Chanda (Mzigua, sheria uzoefu miaka 5). Assuming maeneo ya fani zao ni sawa, ceteris paribus Rais anataka kumteua mshauri wa kisheria.. nani apewe kwa haki? Wengi watasema prof. Mwakalindile! Sasa kwa kufanya hivyo hata hivyo kuna wanyakyusa wawili tayari hapo ikulu ambao wameshapata nafasi zao, je tumnyime Mwakalindile kwa vile itaonesha ukabila?
Kabla hatujafikia hapo pa kudai ukabila tujiulize: "Kwanini inaonekana kuna wasomi wengi wa makabila hayo matatu Wachaga, Wahaya, na Wanyakyusa"? Je, tupunguze wanafunzi wanaotoka kwenye makabila hayo na kuwapa nafasi watu wa makabila mengine ili kuleta uwiano (parity)? Je tukiamua kufanya hivyo hatutakuwa tunaanza ubaguzi wa kikabila?
Tarehe 9 Disemba 1968 Nyerere alitumia siku ya Jamhuri kuzungumzia "Vitu ambavyo ni lazima Tuvisahihishe", vitu ambavyo baada ya uhuru havikwenda vilivyotarajiwa. Alizungumzia ukabila; kwanza alisema hivi:
"the man who talks about tribalism being practised without having any evidence for his statement is often a man who wants to stir up tribalism. Even if that is not his purpose, the result can be just the same. People will begin to think that there is tribalism, and, once people begin to think in these terms, then tribalism has begun to enter tinto our society"
Kuhusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachaga kupata nafasi nyingi katika serikali, Mwalimu alisema hivi miaka karibu 30 iliyopita:
"..the work of the civil servants and people in the parastatal organizations does require education..it so happened that the Tanzanians who had the opportunity for higher education under the colonialists were mostly Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa. And because most of the education was provided by missionaries, most of these people are also Christians. That was our inheritance. These conditions will change, but they have not changed yet. And for these reasons, when we get rid of the Europeans who were doing responsible jobs, and give these jobs to Tanzanians, the people who get them come mostly from one or other of these three tribes".
Akaongeza pia,
"Therefore, if you ask me why Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa have most of the jobs which require higher education, the answer is very obvious. They were the ones who received higher education during colonial times. I'd say: investigate the position in politics where a man is not asked about his educational qualifications. Look at the Parliament, the National Executive and Central Committee of TANU, and at the Cabinet. How many Wanyakyusa, Wahaya, or Wachagga are members? You will find that perhaps there aren't any, or there are one or two. This is the truth"
kwa umahiri wake wa maneno JKN akatoboa ukweli huu
"Anyone who refuses to accept a very obvious truth like this, and says that the reason is tribalism, must provide us with the evidence for his statement. If he cannot provide any evidence, we must conclude either that he is a fool, or that he is strirring up tribalism deliberately. He is the sort of (a) person who begs work on a tribal basis, and when he is refused because he does not have the capabilities, he pretends he was refused on tribal grounds."
Akasema pia ni jukumu la serikali kusaidia sehemu ambazo bado ziko nyuma kielimu. Na alimaliza kwa kusema:
".. if a Mchagga, a Mhaya, or a Mnyakyusayoung man were refused work simply because of his tribe - when he is capable and there is no other Tanzanian with the qualifications - then we would be practising a very stupid and very evil kind of tribalism such as that which caused the establishment of Biafra. I beg you, my brothers, avoid ANYTHING WHICH COULD BRING OUR COUNTRY INTO THIS KIND OF DISGRACE" (emphasis mine)
(From: Uhuru na Maendeleo pp 76,77)
so what say you?
Siamini kama uko justified kutoa conclusions zako kuhusu makabila haya kwa kutumia hiyo experience yako ndogo ya kuhisi (labda na kusikia) na ulipokuwa chuo. Kwanza si kwamba kama ulikuwa A student basi utaweza ku deliver kazini. Elimu yetu yatufunza "kukariri". Huwezi fanya kazi kwa kutumia elimu "uliyokariri", hivyo usitegemee A student wajae ikulu au TRA na kwingineko, maana kule hatukariri hesabu, jiografia n.k. ila tunafanya kazi. Kule hawaangalii kama ulipata A, hizo A nenda nazo chuo kafundishie watu kukariri. Robert Kiyosaki anazungumzia kuhusu kusaidiana katika masomo ambapo wewe wasema ni cheating, lakini ukienda kwenye ajira hutakuwa ukifanya kazi bila ushirikiano na wenzako. Ndio maana A student wengi huwa hawawezi kuwa na team work maana kwao ushirikiano ni cheating, na hii huwafanya dellivery zao kuwa poor. I was an A student, A ya point 7 na point 3, na GPA kubwa chuoni, ila naamini sana katika ushirikiano darasani.
Siamini kama uko justified kutoa conclusions zako kuhusu makabila haya kwa kutumia hiyo experience yako ndogo ya kuhisi (labda na kusikia) na ulipokuwa chuo. Kwanza si kwamba kama ulikuwa A student basi utaweza ku deliver kazini. Elimu yetu yatufunza "kukariri". Huwezi fanya kazi kwa kutumia elimu "uliyokariri", hivyo usitegemee A student wajae ikulu au TRA na kwingineko, maana kule hatukariri hesabu, jiografia n.k. ila tunafanya kazi. Kule hawaangalii kama ulipata A, hizo A nenda nazo chuo kafundishie watu kukariri. Robert Kiyosaki anazungumzia kuhusu kusaidiana katika masomo ambapo wewe wasema ni cheating, lakini ukienda kwenye ajira hutakuwa ukifanya kazi bila ushirikiano na wenzako. Ndio maana A student wengi huwa hawawezi kuwa na team work maana kwao ushirikiano ni cheating, na hii huwafanya dellivery zao kuwa poor. I was an A student, A ya point 7 na point 3, na GPA kubwa chuoni, ila naamini sana katika ushirikiano darasani.
People mnapoteza muda kuongea kuhusu ukabila kwenye ajira in being a dog! or slavery, ajira ni utumwa......
kwanini usijiajiri mwenyewe......! learn to be a master and not a dog. Fanya utafiti mtaani kwako ni kabila gani asilimia kubwa wengi wao wamejiajiri wenyewe kisha utapata jibu ni kabila gani linabaguliwa zaidi kwenye ajira. we uko ukwereni/ uzaramoni lakini maduka mengi mtaani ni ya wachagga au wapemba .....? acheni upuuzi kazi yenu kucheza bao alafu mnataka mpewe ajira serikalini........kwanini msiseme wachagga, wapemba na wakinga wanapendelewa kwenye kumiliki biashara ya mduka kariakoo na kumiliki biashara tz....NAZANI ALIYE ANDIKA MAADA ANGEMAANISHA
WACHAGGA, WAPEMBA NA WAKINGA WANAPENDELEWA KWENYE KUMILIKI MADUKA NA BIASHARA TANZANIA.
walaau angeonyesha kuwa ni mpenda maendeleo na mzalendo wa kweli.
Kama we ni A student basi hamna haja yakusoma ili kupata A duh kwahiyo ni wazi kuwa wewe ulikuwa mtu wakudesa na kuingia na nondo kwenye exams kama unasema eti kusaidia ni vizuri kwenye paper.
Pili ni vizuri kusoma maelezo ya mtu vizuri,jamaa hakumanisha kwamba siyo vizuri kusaidiana bali anasema wakati wa examz yaani in examination. Hii inanipa mashaka na hizo A7,A3..and G.P.A kubwa kama kweli ni halali..!?
Mi si kati ya hayo makabila yeneye akili Tanzania ila nawaambia hivi wale ambao mmeishiwa confidence kuwa hata mkipata nafasi ya kuwa viongozi watu wenu hamuwajali. Fanyeni uchunguzi hivi mkoa wako una shule ngapi za sekondari kijiji chenu kina wasomi wangapi kijiji chenu kina vipaumbele gani juu ya elimu. Leo hii wanafunzi wa kata yako wanasoma au wanaoana tu na kuvuta bangi. Msilalamike wakati elimu mpaka leo hii mnaipiga teke. Hamuwezi kushindana na hao watu ambao hata leo hii mkipewa pamoja shilingi milioni moja baada ya miaka mitano wewe utakuwa na wake watano na watoto ishirini na mwenzako atakuwa na nyumba tano na magari kibao. U deserve kunyanyapaliwa unless mubadilike. hatuwezi kuwa na jamii amabazo zimeparanganyika hazina misingi ya maendeleo na upendo zinabaki kulalamika kwenye key board. Anayebisha aniambie amesomesha ndugu zake wangapi mpaka anabonyeza kibodi amabo siku moja wataomba kazi huko TRA BOT nk na watapata kwa merit za Competence?
Jamani tusome,hakuna njia za mkato kwenye ajira za kisasa. Mi nipo kabila dogo tu lakini namshukuru Mungu kwamba kichwa changu na vyeti vyangu ndio huwa vinanisaidia kupata ajira sehemu ninazotaka. Sijawahi kuulizwa kabila kwenye interview,huwa sijuani na mkubwa yeyote na kazi huwa napata. Makabila hayo matatu mliyoyataja kweli yapo serious kufuatilia elimu za watoto wao,niliwahi kufanya kazi Mbeya,nilikuwa mpangaji wa mzee mmoja anaitwa Kibona,kuna wakati alikosa ada ya mtoto wake aliekuwa chuo. Aliuza sehemu ya shamba lake ili mtoto akalipe ada!. Kuna makabila kwenye hali hiyo huwa wanamwambia mtoto rudi nyumbani fungua biashara kisha oa mke muanze maisha! Tusiwe waongeaji sana wa tanzania. Jitahdi u meet qualification for the job,the rest will be taken care.
Jamani kuhusu ukabila upo sana kuna IDARA kama MAHAKAMA kuna ukabila sana hapa watu wanaothaminiwa ni WAHAYA,sisi wengine ni Third Class human being,ubaguzi si wakificho tumechoka,na waziri wa sheria na katiba analijua hilo
Idara ya Elimu (Waalimu), hasa shule ya msingi na sekondari huko utawapata Wangoni wengi saana.Na sisg wangoni tumejaa idara gani wajameni..? Naomba mnijuze mwenzenu hata sijui.?
Mswahili said:Mama Mkapa alipokuwa Ikulu alifanya kila linalowezekana kuhakikisha anaingiza wachagga kila kona, na hata deal za rada na ndege ni wafanyabiashara wa kichagga wana mikono yao.