Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

samvulechole... hakuna hoja ambayo ni ngeni hapa.. madai ya makabila hayo kupendelewa hayakuanza leo! tangu mara tu baada ya uhuru kulikuwa na tuhuma hizo hizo.. so.. there is nothing there..! Hata hivyo hatari unayoweza kuleta siyo ukabila bali ubaguzi, kuwa kama mtu anatoka kwenye makabila hayo basi asipewe nafasi fulani kwa vile watu fulani wanadhani kuna ukabila! Nitakupa mfano, kuna wanasheria watatu wote ni maprofesa... kuna Prof. Mwakalindile (Sheria, uzoefu miaka 30), Prof. Mtimba (mmakua, uzoefu miaka 10, sheria), na Prof. Chanda (Mzigua, sheria uzoefu miaka 5). Assuming maeneo ya fani zao ni sawa, ceteris paribus Rais anataka kumteua mshauri wa kisheria.. nani apewe kwa haki? Wengi watasema prof. Mwakalindile! Sasa kwa kufanya hivyo hata hivyo kuna wanyakyusa wawili tayari hapo ikulu ambao wameshapata nafasi zao, je tumnyime Mwakalindile kwa vile itaonesha ukabila?

Kabla hatujafikia hapo pa kudai ukabila tujiulize: "Kwanini inaonekana kuna wasomi wengi wa makabila hayo matatu Wachaga, Wahaya, na Wanyakyusa"? Je, tupunguze wanafunzi wanaotoka kwenye makabila hayo na kuwapa nafasi watu wa makabila mengine ili kuleta uwiano (parity)? Je tukiamua kufanya hivyo hatutakuwa tunaanza ubaguzi wa kikabila?

Tarehe 9 Disemba 1968 Nyerere alitumia siku ya Jamhuri kuzungumzia "Vitu ambavyo ni lazima Tuvisahihishe", vitu ambavyo baada ya uhuru havikwenda vilivyotarajiwa. Alizungumzia ukabila; kwanza alisema hivi:

"the man who talks about tribalism being practised without having any evidence for his statement is often a man who wants to stir up tribalism. Even if that is not his purpose, the result can be just the same. People will begin to think that there is tribalism, and, once people begin to think in these terms, then tribalism has begun to enter tinto our society"

Kuhusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachaga kupata nafasi nyingi katika serikali, Mwalimu alisema hivi miaka karibu 30 iliyopita:

"..the work of the civil servants and people in the parastatal organizations does require education..it so happened that the Tanzanians who had the opportunity for higher education under the colonialists were mostly Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa. And because most of the education was provided by missionaries, most of these people are also Christians. That was our inheritance. These conditions will change, but they have not changed yet. And for these reasons, when we get rid of the Europeans who were doing responsible jobs, and give these jobs to Tanzanians, the people who get them come mostly from one or other of these three tribes".

Akaongeza pia,

"Therefore, if you ask me why Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa have most of the jobs which require higher education, the answer is very obvious. They were the ones who received higher education during colonial times. I'd say: investigate the position in politics where a man is not asked about his educational qualifications. Look at the Parliament, the National Executive and Central Committee of TANU, and at the Cabinet. How many Wanyakyusa, Wahaya, or Wachagga are members? You will find that perhaps there aren't any, or there are one or two. This is the truth"

kwa umahiri wake wa maneno JKN akatoboa ukweli huu

"Anyone who refuses to accept a very obvious truth like this, and says that the reason is tribalism, must provide us with the evidence for his statement. If he cannot provide any evidence, we must conclude either that he is a fool, or that he is strirring up tribalism deliberately. He is the sort of (a) person who begs work on a tribal basis, and when he is refused because he does not have the capabilities, he pretends he was refused on tribal grounds."

Akasema pia ni jukumu la serikali kusaidia sehemu ambazo bado ziko nyuma kielimu. Na alimaliza kwa kusema:

".. if a Mchagga, a Mhaya, or a Mnyakyusayoung man were refused work simply because of his tribe - when he is capable and there is no other Tanzanian with the qualifications - then we would be practising a very stupid and very evil kind of tribalism such as that which caused the establishment of Biafra. I beg you, my brothers, avoid ANYTHING WHICH COULD BRING OUR COUNTRY INTO THIS KIND OF DISGRACE" (emphasis mine)
(From: Uhuru na Maendeleo pp 76,77)

so what say you?
yeah..ni mtu asiyekua na upeo mkubwa wa kufikiri ama ni uvivu tu wa kufikiri utamfanya mtu aache mambo ya msingi yanayolitafuna taifa hili na kurudi nyuma kuangalia mambo ya ukabila..haina mantiki kumwacha mtu mwenye sifa na kumpachika asiyekidhi simply kwa kua unataka kuwaridhisha watu fulani fulani kua huna ukabila..
 
tanzania no ukabila
ubaguzi uko kwenye elimu.
hujasoma unategemea kuwa ikulu?
miji yote iliyoendelea ina maduka ya wachaga.
fanya utafiti
 
MMM, I like the way you put your arguments!
Lets not talk of ethnicity while we know the obvious reasons for the cause! The cause is history and we learn from history and create a different future by creating enbaling strategies to the less opportunities groups so that they can also be accommodated in the systems as time come and go!
 
unajua mtu usipojua historia yako.. kuna hatari ya kujaribu kuiandika upya! Ili kuelewa hapa tulipo sometimes we have to look back where we are coming from. Historia yetu haikuanza jana au juzi (kama baadhi wanavyotaka tuamini) matatizo tuliyonayo leo hayakuanza jana (isipokuwa haya ya kina Richmonduli!) lakini mengi yana msingi toka huko nyuma. Binafsi, nitashtuka zaidi kama kwenye nafasi fulani kwenye taasisi kumejaa Wakerewe, Wanyali, au Watindiga.. kwa sababu hakuna jibu zuri la kihistoria linaloweza kuonesha kujaa huko!!

La maana ni kuongeza jitihada ili baadaye hali ielekee uwiano kwani Waha na Wamang'ati na wenyewe watakuwa na shule nyingi na wanapata nafasi nyingi za kusoma.. kwani hata hivi sasa bado Uchagani, Mbeya n.k wanaendelea kuwa na shule nyingi na zenye kutoa wanafunzi wengi (angalia matokeo ya hivi karibuni!)..

Do we need some kind of affirmative action which would not be translated as reverse discrimination?

Mbaya zaidi ni kwamba hayo makabila unayosema yana upendeleo ., pia ndo wanapenda kuzaa kwelili kweli. Sasa wanaoa mpaka mikoa ya huko kwenu, na punde wataleta majina yao huko. Je wakizaliwa Wanyakyusa, Wachaga, na Wahaya kwa dada wa Kizigua, Kizaramo au Kimbulu, halafu wakasoma bado uatasema ni ukabila?
Kazana mzee, elimu bila werevu pia sio merit ya kazi! Tuna wanasheria wengi tu waliograduate , lakini tunasikia majina machache tu...Lamwai, Marando, Mawalla nk..... hivyo on top of education, comes merits, experience and ability to execute! Achana na maneno ya ukabila hapa.....
 
Kwa kweli mimi sina shaka na ukweli kwamba hayo makabila yanaongoza kwa kuwa na idadi kubwa hasa wachaga kwenye maeneo yaliyotajwa. Lakini nina maswali madogo tu kwamba inakuwaje watu hawajajiuliza idadi ya wachaga ambao wana baa karibu nchi nzima.....hawajauliza wanaofanya umachinga wachaga ni wangapi? ....madereva wa daladala wachaga ni wangapi?....Wanaochoma mbuzi, mishikaki, wachaga wako wangapi? ...wezi wa magari wachaga ni wangapi? ... wanaomiliki nyumba za kulala wageni wachaga ni wangapi? wenye maduka wachaga ni wangapi? na mengine mengi ....Ukimaliza hapo utajua suala la hawa watu si historia ya elimu tu bali kuna kitu zaidi ya hapo.....aggressive....
 
Sipendi,
umezungumza ukweli kuhusu aggressve!
but mtu kuwa hivyo ni lazima upate elimu ya kupenda kujaribu kufanya kitu na kuto kata tamaa ya kupata mafanikio!
hiyo elimu ya kuwa na tabia ya kupenda kujaribu na kutokata tamaa ni elimu ambayo mtu huipata kupitia malezi katika familia zao, marafiki, shule n.k
hakuna kulala mpaka kieleweke!!
 
Ninahisi hapa mnaimply kuwa mwenye kigoda anaachia mambo ya ukabila. Ndugu zangu think back kwenye seventies na eighties ikulu, jeshini,nbc, nic na sehemu nyingine nyeti . ilifikia kipindi ukiingia NIC lugha ya taifa haikuwa kiingereza wala kiswahili. Hata vyeo NBC na NIC vingi vilikuwa kwa watu wa kabila fulani. Mambo haya yalikuwa yakitendeka wakati mzee yu hai na mwenye afya.
 
Tukipita kila ofisi serikalini,binafsi,uwiiiii
wachaga tena wako post za juu jamani
inatia moyo lakini ndugu zetu tuwaachie na wengine naona watu wameanza kukasirika najua tofauti za shule ndio sababu basi msisome sana wengine tuingie huko.....wasije wakawalalia bagamoyo dunia mbaya hii..
Wakwe mmenisikia lakini
 
Hii naitazama kwa jicho la 3, ina maana kubwa zaidi ya hivyo uionavyo!
OK..na tuijadili!
 
huu ni ubaguzi wa wazi kabisa haya ndo nyerere alokuwa akipinga usiku na mchana matabaka yasiwepo ya ukabila na udini leo hii tunayaanzisha kidogo kidogo mkuu niwie radhi kama nimekukosea ila sijaona jb au neno sahihi la kujib zaidi ya kusema ni ubaguzi na ninakanusha kauli yako kwamba si kweli wachaga wamejazana kwenye maofisi
 
Tukipita kila ofisi serikalini,binafsi,uwiiiii
wachaga tena wako post za juu jamani
inatia moyo lakini ndugu zetu tuwaachie na wengine naona watu wameanza kukasirika najua tofauti za shule ndio sababu basi msisome sana wengine tuingie huko.....wasije wakawalalia bagamoyo dunia mbaya hii..
Wakwe mmenisikia lakini
hapo kwenye RED umeniacha Hoi lol!
 
utafiti wako umetumia kigezo gani?......si kweli kuwa wachagga ni wengi....rudia tena huo utafiti
 
Tupeleke watoto zetu shule jamani. wezetu kule uchagani walipeleka sana watoto wao shule na sasa matunda yanaonekana. Kule Songea shule nyingi zilikuwa seminari, wangoni wengi wameishia kuwa mapadri. Hata Mbeya wamekwenda shule sana ukifika maofisini utakuta akina MWA MWA kibao. Na miaka ya themanini watu wengi sana walipeleka watoto shule za Mbeya kule Lutengano, na nyinginezo, so hata hawa viongozi wetu nao wanachangia sana kuna watu wapo siriaz kusaidia jamii zao lkn, wengine wakija Dar wakipata Nyadhifa baaaasi wanaongeza nyumba ndogo hata kwao hawarudi.
 
Sasa unataka wenzako wasisome wakusubiri wewe uende shule? Hizo si ndizo sera za awamu ya kwanza za kuweka average marks za kupasi kwenda Form ! kwa Wachagga kuwa kubwa kuliko Mikoa mengine. Matokeo yake wale ndio wakawa wana akili zaidi na kupasi zaidi kwenda Form V na hatimae Chuo Kikuu.

Walipobaniwa na Serikali kutokuingia government schools, Wachagga vile vile walijitahidi kujenga private schools ili wale walioachwa wapate fursa ya kwenda Sekondari. Mimi sio Mchaga lakini niliwahi kusikia wakati nilipokuwa Chuo Kikuu mwalimu mmoja akielezea huo mkasa.

Cha msingi ni hayo makabila mengine kujitahidi ili nao wapasi zaidi na kupata fursa zaidi za kwenda Chuo Kikuu.
 
lakini kama wanasoma waacheni wapate ajira ......tatizo hakuna kama makabila mengine tunahitaji mabadiriko basi tuingie darasani na tusome kwa bidii.
 
Back
Top Bottom