Ukali na intelligence: Kipi kigezo bora anachopaswa kuwa nacho Kiongozi?

Ukali na intelligence: Kipi kigezo bora anachopaswa kuwa nacho Kiongozi?

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,817
Kwa nini Watanzania wanavutiwa na mtu mkali? Mara nyingi nimekuwa nikisikia watu wakimwagia sifa Kiongozi fulani kwa kuwa ni mkali, nimesikia watu wakisema kwa mfano ka Jafo kanafaa sana kuwa Rais kakali sana'', ukali unahusiana nini na Uongozi mzuri na makini wa nchi ? Vipi kuhusu intelligence?

Au ni jinsi tunavyolelewa labda kwa maana hata Shuleni Mwalimu anayesifiwa ni yule mkali na katili anayechapa watoto viboko bila ya huruma.

Hakuna correleration au uhusiano wowote ule kati ya ukali, intelligence na maendeleo ya jamii, mtoto hajifunzi vizuri kwa viboko ingekuwa hivyo Shule za private ambazo watoto hawachapwi zisingeongoza matokeo, leo hii kila mtu anaota kupeleka mtoto wake IST Shule ya kimataifa ambapo hakuna viboko kwa nini kama bila ya viboko mtoto haendi? Au asienda bila ya viboko ni mtoto wa wengine tu?

Ukali au intelligence kipi muhimu? Binafsi nachagua intelligence, sijawahi kusikia nobel laureate yoyote ambaye amewahi kusema siri ya mafanikio yake ni viboko alivyopigwa alipokuwa mtoto, kama ukatili dhidi ya wengine ungekuwa unajenga nchi Dunia nzima wangekuwa wanachapana viboko, lkn sijawahi ona nchi yoyote ile iliyoendelea na tajiri wakiwafanyia ukatili raia wao wenyewe.
 
Kiasili Mimi Ni mkali, lakini nimegundua ukali Ni ufala. Saizi nipo napambana nijirekebishe niwe na intelligence katika kuendesha maisha.

Kuna vitu nilishafeli kuvifanikisha au kuvigundua kisa nimetanguliza ukali wahusika wakaficha makucha.
 
Utilitarians wanaangalia matokeo, intelligence au ukali, vyovyote iwe Ila matokeo ndio kitu ya mwisho watu wanaangalia. Sometime badala ya kumuwaza Sana huyu mkali, ni vema kujiset tu.
 
Kiasili Mimi Ni mkali, lakini nimegundua ukali Ni ufala. Saizi nipo napambana nijirekebishe niwe na intelligence katika kuendesha maisha.

Kuna vitu nilishafeli kuvifanikisha au kuvigundua kisa nimetanguliza ukali wahusika wakaficha makucha.
Umenena ukali ni ujinga kabisa busara nizur zaid kwani utaweza kupata uhalisia wa kitu unachokifanya hasa kinachohusu mwanadamu. Asante mleta mada
 
Unaongelea wale watoto walosingiziwa kuiba madawati?
 
Ukali na Busara katika uongozi ni mtu na mdogo wake.

Ukali unatumika endapo watu ni waelewa lakini wanakuwa wakaidi kufuata taratibu/sheria, kama vile endapo watu ni wavivu/wazembe. wakorofi n.k

Busara hutumika kufundisha, kuelekeza, kushauri, kupatanisha....endapo vyote hivyo vitashindikana ukali unachukua nafasi. Ukali ukishindwa basi sheria inachukua nafasi yake(tena kali).

Ukiona watz wanataka watu/viongozi wakali, basi ni wazi watz wengi ni 'Ma-lazy' na vichwamaji 😅
 
Vyote vinahitajika na kila kimoja kinasehemu yake sasa wewe tumia busara pekee au ukali pekee ile kwako, tumia vyote kulingana na mazingira
 
Ukali ni upuuzi. Mara nyingi wakali hukurupuka na kuharibu kila kitu.

Mnamkumbuka yule mzee aliyekua anafanya kazi zoote za Latra Dar nzima mpaka akaleta sanity kwenye daladala, yes Mwaibula. Yule alikua anatumia intelligence. Sasa ona Hawa wakali wa Latra wa sasa wanaoshikia madereva mapanga.
 
Kila kimoja kina nafasi yake katika uongozi lakini kitumike kwa usahihi na wakati sahihi.
 
Ila nadhani kuna aina nyingi sana za ukali. (My perception!)

Let’s say ; 1)Ukali wa uso wa mbuzi (Huu ni ule muhusika haangalii Sura anapotoa maelekezo ama anapotoa adhabu , ila kwa kiasi chake anazingatia matokeo kadiri ya ufahamu wake!)

2)Ukali wa ukatili (Huu ni ule muhusika hajali matokeo yoyote yatakanayo na maelekezo yake ama adhabu zake, yawe matokeo positive ama negative, humwambii kitu!)

Bahati mbaya sana hapo kwenye “Intelligence “, sio wengi wetu tumejaaliwa kuitambua iliyopo ndani yetu na kuitumia ilivyokusudiwa!

Nafikiri kwa sauti!
 
Muulize DC aliyepokea kipigo toka kwa binti wa shule!
 
Kuna tofauti ya ukali na ukichaa, nani amefanya kazi na Mamvi? Yule jamaa ni mkali hasa na hataki masihara, mara nyingi sana kazi chini yake huwa zinatoa matokeo chanya. Bahati mbaya sana weak systems za nchi hii zinazotengeneza loopholes zimempekelekea kuwa fisadi papa.

Haya mtajua mkali ni yupi na Kichaa ni yupi.
 
Ukali hauna effect yoyote instead unaleta fake effect results kwenye kila kitu.

Kuwa serious and intelligent ndio nguzo ya uongozi even effects zitakuwa real.

Kuwa mkali ni sawasawa na mbuzi aliyejificha huku akitoa mlio wa simba.
 
Scientifically na Psychologically hakuna Uhusiano kati ya Ukali na Akili kwani wapo ambao ni Wakali ila Wapumbavu na wapo wa Kinyume chake.
 
kiongozi hapaswi kuwa mkali,mkorofi,zoba,muongeaji sana,anayejifanya anajua zaidi nk.

kiongozi anapaswa kuongoza.
 
Back
Top Bottom