Ikikukumba unaweza ukamkula hata mkeo [literally π].
Sina uhakika na vyakula vya huko kusini mwa Afrika.
Labda nyama ya tembo ni moja ya delicacies pande hizo.
Kutokana na ukame ulioikumba nchi hiyo, serikali yake imetoa ruhusa ya kuchinjwa kwa tembo 200 ili wananchi wapate chakula.
Zimbabwe inapanga kuwaondoa ndovu 200 ili kulisha raia wake ambao wanakabiliwa na njaa kali huku kukiwa na uhaba wa chakula kutokana na ukame.
Zimbabwe inakumbwa na ukame mbaya zaidi katika miongo minne. Kwa hivyo, serikali inataka kusambaza nyama ya tembo miongoni mwa jamii zenye njaa. Zimbabwe inafuata uamuzi wa hivi majuzi wa Namibia.
Mwezi uliopita, waliamua kuwaua wanyama pori 700 wakati wa ukame. Wahifadhi na wanaharakati wamekosoa mauaji hayo ya halaiki, lakini nchi bado hazijakata tamaa. Je, uondoaji huu wenye utata unaweza kutatua matatizo yao?