Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Mkuu ngoja niendelee kujaribu kuweka kivuko kinachotumika kisiwa cha Mafia unaweza kulia machozi.
 
Huyu ni muhuni kabisa, under normal circumstances huwezi kunusurika ajali ile na leo uko busy mtandaoni
 
Sasa hapa kuna haja ya kuzifanyia maboresho sheria zetu ili vyombo hivi vya serikali viwe vinakaguliwa na watu wa tasac
 
Vivuko ni ngumu kujua wangapi wamepanda
Hivyo kuna wengine wanaweza wasiwekwe kwenye orodha
Yaani karne ya 21 bado ishindikane kujua na kudhibiti IDADI ya wapanda vivuko. Kwani si wanakatiwa tiketi na idadi ya tiketi inajulikana.

Vipi wenye mabasi nao hawajui idadi ya tiketi wanazouza.

Kwa fikra hizi tutaendelea kufa kizembe kwa karne kumi zijazo.
 
Watu zaidi ya 150 walilala majini na kumalizia kukata roho kutokana na kauli ya kijinga ya RC.

RC awajibike kwa kauli yake japo nasikia amekana
 
Sasa hapa kuna haja ya kuzifanyia maboresho sheria zetu ili vyombo hivi vya serikali viwe vinakaguliwa na watu wa tasac

Ni kweli tena wahusika inabidi wafanye hili immediately na ikiwezekana kazi ya ukaguzi wa vivuko vyote uanze mara moja pamoja na meli zote za abiria tena isiwe zima moto iwe routine ili kuondoka na mambo kama haya. Azam marine pale sidhnai kama leo ukimuuliza idadi ya abiria wake na majina yao wote atakosa, ila hatua chache tu pale kigamboni zipo ferry zinakwenda na kurudi watu wanakatishwa tiketi wanajazwa kwenye lile jengo ferry ikija wanapandishwa ikionekana kwa macho imejaa wengine wanazuiwa sasa mziki unakuja umepandisha idadi kiasi gani na majina yao? HIVI VITU VINATAKA USIMAMIZI WA KARIBU KABISA NA WATU WENYE UELEWA NA SIO KUWAACHIA WATU WASIOJUA KITU..
 
Samaki wanavuliwa usiku na makarabai,
Binadamu hawezi kuokolewa giza linapoingia kwa amri ya Mkuu wa mkoa.
"Mongela awe wa kwanza kujitafakari"
 
Pamoja na kosa la kujaza kupita kiasi. Tabia ya kila mtu kutaka kuwa wa kwanza kuteremka imechangia hii TRAGEDY.

Tabia hii ipo katika vyombo vyote vya usafiri wa umma iwe ndege au basi. Yaani basi likifika kwenye kituo cha mwisho abiria hudhindana kudhuka. Hata ndege ikitua tu kila mtu anataka kushuka wa kwanza utaona wanahangaika kushusha mizigo HATA KAMA WAMETANGAZIWA WAENDELEE KUKETI KWENYE VITI.
 
Nguvu kubwa tumeelekeza kwenye demokrasia, namaanisha uchaguzi wa marudio, by elections.

Mungu ingilia kati mambo ya Africa
 
Hao waliyoruhusu kivuko kuanza safari wawajibishwe!
Alafu sjui kama kivuko Hicho kina Bima

Ova
 
Tukienda unavyoshauri bila kufanya uchunguzi tutakosea .Ngoja uchunguzi ukamilike Kwanza manake tume itaundwa.
 
binasi nimekuelewa sana hoja yako
 
Wakati mwingine muwemnatumia kidogo akili za kuzaliwa watu 500 waende Ukara hali itakuaje huko? Jaribu hata ku google ili uelewe ukubwa wa kisiwa chenyewe pia wanaenda kufanya nini? Lazima serikali icontrol uingiaji wa kisiwa cha ukara la sivyo tunaweza ongeza majanga zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…