Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Sipingani na utaratibu wa kawaida wa kuchangiana na kuwafairiji wenzetu waliopatwa na huu msiba mkubwa...
Ila serikali yetu badala ya kuongeza nguvu kwenye uokoaji wa watu wanakimbilia kuchangisha rambi rambi...
Hatujasahau
1.rambirambi za luck vicent iliyouaa watoto wetu
2. Rambirambi za tetemeko la ardhi
Je na hizi zitawafikia walengwa???
 
Hadi sasa idadi ni zaidi ya mara mbili ya uwezo uliotajwa wa abiria 100.
Naweza kunyamaza kwa kuniuliza sehemu ya ajali. Naomba nikueleze kwamba Bugolola napafahamu, bwisya napafahamu, hata lubaga napafahamu. Ziwa hilo nalifahamu vizuri sana!! Muhimu ni uwezo wangu wa kutafakari. Zaidi ya kufahamu maeneo hata elimu ya ubaharia ninayo kiasi kidogo. Ndo maana naweza kuuliza kama cabin ya abiria ilikuwa water tight, sababu ambayo ingeweza kuwaokoa baadhi yao kama ilivyotokea kwa huyo fundi mkuu.
 
Nasikia inasemekana serikali imekiri kuwa nahodha hakuwa na mafunzo ya kuendesha chombo kile.

Hayo ndo makosa ya kimfumo.
Kama mfumo husika ilikuwa dhaifu na matokeo yake nahodha hakuwa amepata mafunzo basi serikali lazima iwajibike katika ngazi zinazohusika. Hakuna udhuru utakaotosha kuzuia uwajibikaji
 
Una umri gani tuanzie hapo kwanza? Naweza nikawa nawasiliana na mtu ambaye yuko darasa la 7 kwa sasa hivyo nikimweleza maendeleo ya miaka 30 iliyopita nitakuwa na mwonea tu inawezakawa hata mimba yake ilikuwa haijatungwa!
Nina miaka mitano!!
 
Wazee wa kupiga rambirambi katika ubora wao hahahahaha!!
 
Swala la kujaza mara kwa mara sio guarantee ya kutopata ajali.Hata huko barabarani magari huwa yanakimbia sana lkn siku dereva akikosa timing tu chali.
Kwhyo tunafanya kawaida ila cku ajal ikitokea tunakuja na sababu hyo hyo?

Tuishi kwa mazoez ili tuje kusema n mapenzi ya Mungu?
 
wendawazimu tu ndio watapeleka pesa kwenye hiyo akaunt
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…