Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ilimradi tu utetee
 
Tuna tatizo la kutokujifunza.Hatukujifunza ilipotokea mv bukoba,hatukujifunza ilipotokea ajali ya ile meli kule zanzibar.Katika maswala ya uokoaji tunaishi kwenye karne ya 19,ni lazima serikali ijifunze kuyakabili majanga kama haya.Wasiishi kusubiri majanga yatokee ndiyo waanze kujipanga bali wajipange kwanza kabla ya majanga.
 
hao waokoaji umewaona, hawana zana zozote za kuokolea, yani bare body, wameshindwa kuwa na mitungi ya gesi wakazama chini jamani, nimeshangaa sana maiti zinashikwa with bare hands kweli, daah
Ah mkuu hapa kweli imesikitisha, yaani nimewaonea huruma waokoaji, nahisi hata nchi zilizoendelea zitashangazwa na hili, kwani ni Aibu kwa taifa kutokuwa hata na vifaa vyoyote vya uokoaji, hata groves tu shida kweli? ??
 
Ni wakati wa majanga pekee ndipo tunapata fursa ya kujifunza umadhubuti (strengths) na udhaifu (weaknesses) wetu. Majanga kama haya ndio fursa pekee ya kuipima serikali na taasisi zake kama kweli zinafanya kazi kwa maslahi mapana ya wananchi maskini au wanafanya kutafuta sifa. Kuna dhana inayoonekana kuwa serikali inajilazimisha kukimbilia kwenye vitu vichache zinavyookena kama madaraja, reli, ndege nk, huku ikisahau yale mambo ya huku chini yanayomgusa mwananchi wa chini moja kwa moja, mfano mishahara ya wafanyakazi, huduma za afya, elimu bora, huduma bora za usafiri, kuchochea ukuaji wa biashara ndogongogo na za kati, ajira kwa vijana, uhakiki wa ubora wa huduma anazopata mtumiaji wa mwisho nk.

Janga hili limeonyesha udhaifu mkubwa sana kwenye haya mambo ya chini ya kawaida ambayo ni haki ya msingi ya mwananchi yeyote kuzipata. Sina ujuzi wa taratibu zinazotakiwa kufuatwa katika haya mambo, ila akili yangu inanituma kuwa inatakiwa tume ya bunge kuchunguza hili tukio na mambo yote yanayohusiana na usafiri wa majini kwa ujumla. Hasa kwenye kipengele cha usalama, udhibiti wa ubora wa huduma, uchakavu wa vyombo vyote na kama bado vinafaa kuwa majini, taratibu za matengenezo na services, udhibiti wa uwezo wa kuchukua mizigo (loading capacity), mahitaji ya kila eneo lenye chombo yaani uwezo wa vyombo vs mahitaji (demand) na mengineyo ambayo wataalam wanaweza kuyashauri kwa uziri zaidi.

Ripoti kama hizi zitafaa sana kuwajibisha watendaji na kutoa mwongozo wa jinsi tutakavyoenda siku za mbeleni. Pia ripoti kama hizi zitalisaidia sana bunge kupanga bajeti zinazoendana na mahitaji husika kuliko kuiachia serikai ijipangie tu kutokana na matakwa yao na malengo ya kisiasa zaidi.

PARLIAMENT HAS TO ACT. SERIKALI KWA MAANA YA WAZIRI AMESHASHINDWA, LAZIMA BUNGE LIMSAIDIE HAPA.
 
Kwanza huyo mkuu wa mkoa ana ujuzi wa rescure Opss??
Tragedy inakupa muda eti usiku??
Kwa nini wasilete boats na vivuko toka Mwz wakawasha taa na opss zikaendelea??
Kuna Polisi Marine kuna Navy ya JWTZ wote hao wanafanya nini??
Tabia za kizembe hizo kama huwezi kazi waachie wenye uwezo wafanye!!
Huyo aliyetoa amri watu waachwe wafe majini achukuliwe hatua.
Serikali hailali ni 24hrs aende akalale kwao atuachie kazi zetu!!
Watz tumekuwa mandondocha au misukule nini hii??
 
Na wakati mwanza ndo mkoa pendwa wa mkulu, vyombo vya ulinzi na usalama vinaenda kulala kwamba uokoaji utaendelea kesho dah!
 
umeandika vizuri sana lakini ulipotaja raisi umeharibu,umefananisha fikra zako chanya na kitu kichafu.pole sana mkuu poleni watanzania.
 
Nilimsikia mkuu wa mkoa wa Mara anahojiwa anaongea kabisa kwamba hapa ndo tunajiandaa kukusanya vikosi na kuelekea huko kutoa msaada, tutaondoka na jeshi la polisi blah blah anajipanga utafikiri ni safari na yuko cool kabisa kama vile yuko ofisin!
 
umeandika vizuri sana lakini ulipotaja raisi umeharibu,umefananisha fikra zako chanya na kitu kichafu.pole sana mkuu poleni watanzania.
Nashukuru ila nimetoa mfano maana yeye alishawahi kutuaminisha hivyo kipindi yuko kwenye uteuzi japo sijui kama ni kweli ndugu yangu
 
Nashukuru ila nimetoa mfano maana yeye alishawahi kutuaminisha hivyo kipindi yuko kwenye uteuzi japo sijui kama ni kweli ndugu yangu
sisi watanzania husikiliza na kuamini sana maneno,ila mkuu binti yako akipewa mimba akiwa shuleni ni tatizo lako kama baba.tatizo la nchi hii ni kuu sana.
 
hivi vivuko vyetu vya serikali vinasimamiwa na temesa au marine service?
halafu ningependa kufahamu kama sumatra pia wanasimamia na hivi vivuko.
nilishasafiri na hivi vivuko vya serikali , utaratibu wao ni mbovu sana.
mfano kwenye hii ishu hakuna manifest ya watu waliopanda kwenye hicho chombo mambo ya ajabu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…