Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Mkuu,
Kwa vijijini siku ya mnada najua unajua usafiri tunavyojazana. Ukizingatia wamiliki wanataka pesa tu bila kutoa elimu kwa abiria. Just imagine overloading ya watu na mizigo wakimbilie upande mmoja, yale yale ya MV Bukoba watu kukimbilia upande na kutoboa meli watoke kumbe ndo disaster.
Kwa ufupi hatujifunzi hata 2012 MV. Spice highlander.
Tunahitaji uwajibikaji kwa mamlaka husika.
 
Sidhani hata kama kuna abiria hata mmoja aliyeandika jina lake wakati wa kupanda, hata idadi kamili ya watu unaweza usijue mana kuna tiketi zao na za serikali
 
Kama yanawapa credit mbona wanaiba kura badala ya kupewa kura? Nenda kamdanganye mumeo!
Basi dada, isikukwaze sana hii coment yangu najua huwa hampendi kuambiwa ukweli.
 

Uzuri wenyewe hao wananchi wa sasa hivi wanauelewa wa kutosha, hakuna fala wa kwenda kumuuzia face wakati wanajua hela zinatumika kurudia chaguzi za kishenzi. Nani anashoboka na face ya mwanaccm wakati mbunge wao alishaongelea suala la kivuko huko bungeni?
 
Mbona simuoni akiokoa au ndiyo kutafuta sifa kwenye msiba kisisiemusisiemu! Tutaona nguo za kijani zimejaa kando ya ziwa wakijisefii.
Tuelezwe ujuzi wake kwenye uogeleaji na uokoaji.
 

Unapokata tiketi kwenye safari kama hizo lazima manifest isome jina lako, namba ya simu, immediate contact na unapotoka.
Nchi zilizoendelea wao huswap card ambayo inadetails zote za mwenye card.
Kwa Tanzania tunapaswa kuwa na manifest kama ile ya nyumba za wageni inayoeleza details za mtu ili ikitokea dharura iwe rahisi kutrack na kutambua, Mabasi ya mikoani Ubungo huwa tunaandika namba za simu na majina ila inabidi waongeze na hiyo ya immediate contact incase of emergency, Ulaya walianza hivi baada ya kuendelea ndio wanatumia Card yenye full details.
Mbona kwenye ndege watu hubeba ID au Passport, huu ni utamaduni lazima tuwe nao..
 
Kwa hiyo kivuko kikizama, Watanzania wakafa, serikali ya jiwe ikasitisha uokoaji na mwenyekiti wa uvccm akienda kuopoa maiti za Watanzania chama pendwa CCM kinapata credit dhidi ya CHADEMA?
 
Sidhani hata kama kuna abiria hata mmoja aliyeandika jina lake wakati wa kupanda, hata idadi kamili ya watu unaweza usijue mana kuna tiketi zao na za serikali

Ndio hapa tunapoongelea kila siku uwepo wa system imara itakayokuwa inasimamia mambo kama haya na kumaliza maujinga kama haya ili watu makini na maisha ya watu. Tuna mawaziri, makatibu, RC's ,DC's, DED, RAS nk woote hawa wanafanya nini kushindwa kusimamia mambo serious kama haya?
 
Mwaka 1996 MV Bukoba ilizama na kuua mamia ya raia, inasemekana chanzo kilikuwa ni kujaza abiria kupita kiwango.
Mwaka 2011, miaka 16 baadaye, Meli ya MV Spice Islander I ilizama, pia inasemekana ilibeba abiria na mizigo kupita uwezo wake.
Jana tena kivuko cha MV Nyerere nacho kimezama, pia tunaambiwa kilijaza abiria kupita kiasi.
Hivyo inaonekana pamoja na majanga yote haya, mamlaka zinazohusika zimeshindwa kudhibiti upakiaji wa abiria katika vyombo vya majini.
Mbona mabasi tunaweza kudhibiti, mbona kwenye ndege hakuna overloading? Kwa nini vyombo vya majini tunashindwa kudhibiti idadi ya abiria? Naamini kila chombo kinakuja na idadi ya abiria ambayo ni salama, kwa nini hazifuatwi? Watu wa TEMESA au SUMATRA wawajibike kwa kushindwa kudhibiti upakiaji wa abiria kwenye vyombo vya majini
Ifikie wakati tujifunze.
Yanapotokea majanga kwa mara ya kwanza inatakiwa ndio liwe fundisho la kubadili au kutunga upya kanuni za jambo husika.
 
Kudos
Hatujifunzi kabisa mkuu ya 1996, 2012 Zanzibar.
Kama basi la abiria tu majina yanaandikwa kuhifadhi kumbukumbu za abiria leo kivuko cha majini SUMATRA hawana rekodi ya idadi wala majina ya abiria.
Yaani ni uzembe mkubwa sana.
Wamiliki wa vyombo wazembe sana.
Mbona ATCL hawazidishi abiria, jibu ni kwamba usafiri majini umejaa non professional personnel ambao hawajui au wana makusudi.
Kutoa elimu ya usalama kwa abiria awapo majini napo hakuna.
Watu 400 wamezidi na wakimbilie upande mmoja kwa sababu hakuambiwa risk za kufanya hivyo kabla ya safari.
Yaani nchi zetu hizi ni tupo Ujima.
 
Sawa sawa ile sehemu ya dharura ndo muhimu kwa contacts kuliko zote ..... mimi nilikuwa na wazo labda kama kitambulisho cha taifa kinakuwa na chip ambayo sehemu kama airport,stand za magari,stesheni kwa train,bandalini au kwenye vivuko kunakuwa na mashine una swap inarecord mtu fulani anaenda kuboard unalipa unakwenda na usafiri unao tumia ukifika unaswap umetoka inakuwa na in and out ....hii ingekaa poa kwa kutumia kitambulisho cha taifa na wasio kuwa navyo as hao below 18 wanatumia manual normal receipt
 
Na Hapa juzi Siasa iliingilia pale ambapo abiria wasio na vitambulisho walipokataliwa kukatiwa tiketi, sababu ya umuhimu wa kuweka kumbukumbu
Abiria wenyewe walilalamika kudaiwa vitambulisho. Jana majibu yakapatikana.
 
Hawa ccm wanatia hasira sana maana wakiambiwa matatizo kama ya meli chakavu wanapiga risasi wapinzani
 
Mkuu
Hakuna rekodi ya watu walioingia. Naskia ni kupanga tu mstari unaingia chomboni.
Ukisikia statistics za 400 (yaani takwimu za sufuri mbele) huwa ni makadirio ya siyo na uhalisia.
Pathetic agencies!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…