Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Zitaliwa, msitoe. Waombeeni tu waliofiwa, waliokufa , majeruhi Mungu awape kila lililo jema kwa kila kundi. Mambo ya rambi rambi achana nayo, zitaliwa au kupelekwa kusikojulikana.
Mungu wasaidie wote kwa faraja inayowafaa. AMEN
Hela ya tetemeko imetuvunja moyo sana !
 
Kwani Jimbo la Ukelewe lina Mbunge wa chama gani? "AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO MBAYUWAYU"
Mbona mnataka kuleta siasa mpaka misibani, sasa mbunge angekuwa wa chama kingingine angezuia ajali isitokee.
 
Jamaa yupo magogoni anazisubir rambirambi aanze kuzila badala ya kwenda ukerewe
 
Msiba wa MV Nyerere umepoteza watu zaidi ya 137 ( kizembe zembe kabisa ). Hakika ni msiba mkubwa sana. Ila sasa ni lazima hawa marehemu waondoke na watu wengine walio hai hapa duniani. Lazima wawajibike.

Niipongeze serikali imeanza kuchukua hatua.Mh. Rais tayari kamtuma Waziri Mkuu huko Mwanza.Nawapongeza sana.


Bendera zitapepea nusu mlingoti kwa siku 4 . Sijajua kama kazini hatuendi. Na kama ndivyo sijajua mshahara wa mwezi huu utatoka lini maana utaathirowa na siku ya j3 ( watu hawatafanya kazi ipasavyo ).

RIP kwa wote.

Tuje kwenye mada: TBC1 na maombolezo :-



TBC 1 wamekuwa wakiomboleza misiba ya kitaifa kwa nyimbo za dini ( za kila aina ) muda karibu wote wakiwa hewani.

Kwa kuwa Channels zingine kama ITV , Star TV, etc zilipata pata shida hivi karibuni… tumekuwa watu wa kukomaa na TBC 1 tu muda mwingi.

Maombolezo maombolezo maombolezo TBC 1 kila sekunde, kila dakika ukiwasha runinga yako!
 
Mbwiga hapa namzungumzia Mbowe kama KUB...........siyo yule wa Bills use unaelewa!
 
Nampongeza Mwita Waitara kwa kufanya maamuzi sahihi!
 
Acheni kukandamiza maoni mbadala.Hivi kukosekana uokoaji kwa zaidi ya masaa sita huku jeshi,polisi,zimamoto vikiwepo ni siasa?.Hivi kusitisha uokoaji na kusubiri uopoaji ni siasa?.Tunahaki ya kulinganisha umakini wa serikali kwenye ziara za Rais,Uchaguzi,mikutano au matukio ya wapinzani na hili la maafa
 
Umeshapanic!!.......Ukerewe ni jumbo linaloongozwa na mbunge wa Chadema mbona hamumpi ushirikiano. Mbona wakati Sugu anatoka jela KUB alikuwepo!
Wewe nakufundisha kila wakati jinsi ya kujenga hoja lakini una kichwa kigumu kisichoelewa kama chama unachoshabikia! Kwanini uwabague waliopoteza ndugu zao kwa uzembe wa serikali kwa kutumia itikadi za vyama?
Hivi ninyi ccm, ni lini mtaacha kuitumia misiba kama uwanja wa siasa zenu za kibaguzi?
Au maana yenu ni kuwa raia akiwa na itikadi tofauti anapoteza uraia wake? Hebu acheni siasa hizi za kijinga za kibaguzi kwani hazitujengi na kutuunganisha katika kuwafariji waliopoteza ndugu zai badala yake zinatufanya tuonekane mahayawani mbele ya majirani zetu na watoto wetu ambao wanatakiwa kujifunza kwetu! Badilikeni ccm!
 
Anaongea Leo alikuwa wapi siku zote mbili hizi
Lazima liongelewe kisiasa kwani pesa za kununua ferry na mengineyo kwa ajili ya maendeleo ya walipa kodi mnarudia chaguzi zisizo na tija
Hapa huchomoki hata usemeje
Haya sasa mnaanza kuunda tume watu wale posho za bure badala ya kurekebisha miundo mbinu
Hii nchi imelogwa kupitiliza
Siasa mumo kwa mumo mpaka muwaelewe walipa kodi na dharau zenu
 
haisaidii hata ikiwekwa chini ya mlingoti
Ndugu yangu kuomboleza ni MILA NA DESTURI, DUNIANI KOTE, hata Marekani kila mwaka ikifika September 11, wanaombieza "Airplane bomming of WTO!!??!!, Kwahiyo Serikali yetu kupeperusha nusu Mlingoti ni ishara ya kuomboleza kwa wa Tz waliofariki ajalini, kwenye majanga kama haya usiingize itikadi za Vyama!!!??!
 
Watu 40 wameokolewa. Kama waokoaji wangekuwa na akili kama zako basi baada ya dakika 25 tuu wangetangaza watu wote waliokuwa kwenye kivuko wamekufa.
 
Jibu swali, kwanini mmemtenga mbunge Mkundi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…