Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Amani iwe nanyi wapendwa.

Rais wetu mpendwa Dr Magufuli jana ametoa salamu za pole kwa wote waliofikwa na msiba kutokana na ajali ya Mv Nyerere, pia salamu hizo zimelengwa kwa watanzania wote kwa ujumla ndiyo maana akatangaza siku nne za maombolezo na bendera za taifa kupepea nusu mlingoti nchi nzima.

Jambo la pili amewashukia kama mwewe baadhi ya wanasiasa viherehere waliofilisika kichwani ,ambao kwao ajali ya Mv Nyerere wameigeuza kuwa fursa ya kupata kiki kisiasa.
Ikumbukwe kuwa mara baada ya kutokea ajali hiyo mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe aliitisha vyombo vya habari na kuanza kutafuta kiki kwa kujigeuza mahakama na kuanza kushutumu na kuhukumu watu kwa mambo asiyoyajua vizuri.

Pia Zito Kabwe na James Mbatia hawakuwa nyuma katika kutumia msiba huu kama mitaji yao ya kiki za kisiasa .
Inasikitisha sana viongozi wa vyama vya upinzani badala ya kuwahi eneo la ajali kwenda kutoa msaada kwa wapiga kura wao ,wanabaki twiter kukejeli wafiwa na kujijenga binafsi kisiasa bila kutoa msaada wowote!!!

Hongera sana Rais Magufuli kwa kuwavua nguo hawa wanasiasa uchwara ,wachumia tumbo na wanafiki ,ambao wao muda wote wanawaza siasa tu huku vyama vyao vikiwafia kwa kukimbiwa na wananchi..
Pathetic
 
Wakati zoezi la uopoaji miili ya wahanga wa ajali ya maji iliyotokana na kivuko cha Mv Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi amesema kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati.

Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.

“Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni, ilifanyiwa kazi ambapo tulikuwa tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna gani tunaweza kubadilisha idadi ya safari”, amesema Mkundi

Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
 
poleni wafiwa wote sisi sote ni ndugu tunawaombea faraja!

waliokufa sio wasukuma pekee au wakara pekee ni watanzania wa makabila mbalimbali tuweke ukanda pembeni tulie na yaliyoyukuta
 
Wewe kuna kitu hutuambii kuhusu Mbowe na Chadema. Huenda ulitaka kupewa nae ila kakutosa. Haiwezekani uweweseke nae hivyo. Wewe na yule Mramba ni naona mmepewa special assignment ya kudeal na Mbowe. Kila siku unaanzisha uzushi kwa Mbowe na Chadema Baada ya kujifanya mwanachama watu wanakuchora tu. Pole maBwana wapo sema wanaoa waliotulia, vicheche hutumiwa na kuachwa
 
We ndugu

Mbowe alimtaka Rais aongee na sio Msigwa Kutoa Twite kwamba Rais amesikitishwa hatimaye Rais kazungumza, je ndio kuvuliwa nguo huko?

Pili lawama kwa serikali haiepukiki kwa sababu zilizo wazi. Moja ndio yenye jeshi la uokozi sio vyama vya siasa. Pili serikali ndio mmiliki wa kivuko, tatu serikali kupitia Sumatra ndio mkaguzi maswala ya usalama wa vyombo vya usafiri na mwisho ndio operator wa kivuko hicho sasa lawama apewe nani?

Tumeona wavuvi ndio wamefanya kazi ya uokozi na uopoaji wa maiti je jeshi letu la uokozi lipo wapi inafika usiku wanasimamisha kazi ilihali watu bado wamenasa ndani ya meli.

Kwa muktadha huo huoni aibu kwa uliyoyaandika. Tusifie pale panapostahili na tukosoe pale inapohitajika. Sio kila kitu kusifia natamani upate janga kama hilo ndio akili ikukae vizuri.

Roho za marehemu wote waliokufa kwenye ajali Mungu azipe pumziko la milele
 
Amani iwe nanyi wapendwa.

Rais wetu mpendwa Dr Magufuli jana ametoa salamu za pole kwa wote waliofikwa na msiba kutokana na ajali ya Mv Nyerere, pia salamu hizo zimelengwa kwa watanzania wote kwa ujumla ndiyo maana akatangaza siku nne za maombolezo na bendera za taifa kupepea nusu mlingoti nchi nzima.

Jambo la pili amewashukia kama mwewe baadhi ya wanasiasa viherehere waliofilisika kichwani ,ambao kwao ajali ya Mv Nyerere wameigeuza kuwa fursa ya kupata kiki kisiasa.
Ikumbukwe kuwa mara baada ya kutokea ajali hiyo mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe aliitisha vyombo vya habari na kuanza kutafuta kiki kwa kujigeuza mahakama na kuanza kushutumu na kuhukumu watu kwa mambo asiyoyajua vizuri.

Pia Zito Kabwe na James Mbatia hawakuwa nyuma katika kutumia msiba huu kama mitaji yao ya kiki za kisiasa .
Inasikitisha sana viongozi wa vyama vya upinzani badala ya kuwahi eneo la ajali kwenda kutoa msaada kwa wapiga kura wao ,wanabaki twiter kukejeli wafiwa na kujijenga binafsi kisiasa bila kutoa msaada wowote!!!

Hongera sana Rais Magufuli kwa kuwavua nguo hawa wanasiasa uchwara ,wachumia tumbo na wanafiki ,ambao wao muda wote wanawaza siasa tu huku vyama vyao vikiwafia kwa kukimbiwa na wananchi..
Utafikiri sisi wote hatuna akili.Hao ni wanasiasa maarufu sana ndani na nje ya Tanzania.Ni wabunge na wanaeleweka.Hawahitaji msiba kuwa mtaji wao,mtaji tayari wanao ndiyo maana ni wabunge.Lengo ni kuzua watu wasihoji uzembe wa namna uokoaji ulivyofanyika,ukosefu wa vipaumbele na usitishaji uokoaji eti sababu ya giza.Hata wanasiasa wasipoongea,picha zinaongea pia.
 
Kwa kweli ni habari ya masikitiko kwa Taifa letu! Mungu atuongezee nguvu na kukabili hili janga la msiba wa kitaifa!
 
SUMATRA ni hovyo kabisa, ukitaka kuamini nenda kwenye mabasi ya abiria utachoka! Mbaya zaidi ukiwapigia simu kwenye namba zao za bure walizoandika kwenye mabango yaliyotengenezwa kwa gharama kubwa kabisa, wanakuambia sisi tupo HQ, wasiliana na ofisi ya Mkoa ulipo, na wakati mwingine wanakujibu sisi hatufanyii kazi taarifa za simu, fika mwenyewe ofisini kwetu. Imagine kwa hali kama hiyo utasema SUMATRA ipo kwa kazi gani?
SUMATRA ni watozaji wa fedha tu usimamizi mbovu sana.
 
Maboya ya kujiokoa yalikuwa yamefungiwa stoo kwa kufuli kubwa!....This is Africa!
 
Safari hii kipaumbele ni dirimu laina, maswala ya vivuko yasubiri tufikishe idadi angalau 4 tuweze kumfunika jirani
 
Wakati zoezi la uopoaji miili ya wahanga wa ajali ya maji iliyotokana na kivuko cha Mv Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi amesema kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati.

Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.

“Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni, ilifanyiwa kazi ambapo tulikuwa tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna gani tunaweza kubadilisha idadi ya safari”, amesema Mkundi

Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
Mbunge kamuumbua mwenyekiti wake Mbowe....... hii ni Aibu kubwa kwa KUB!
 
Back
Top Bottom