Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Nijaribu kukisia tu ni km Km 50-60
Omnabuzegwe, Unakisia au uko hapo visiwani ?, na kama ndio hivyo how come umbali wa kilometer 50-60 yatumike masaa mawili ?
au ndio kivuko kilikuwa kibovu kinajikokota tu humo majini ?, usafiri wa majini kama ulivyo wa angani unatakiwa for sure chombo kiwe smart, na naamini ifike wakati meli na Vivuko viondolewe chini ya usimamizi wa Sumatra, either wapewe mamlaka ya anga (aviation authority) au kiundwe chombo kingine, waha Sumatra kuna maeneo mengi wameonesha kushindwa kutimiza majukumu yao
 
I hope umemaanisha MV nyerere..
Tatizo ni kwamba serikali haikujipanga kwenye kuzuia majanga kama haya..na tatzo linaweza kuwa kwny serikali kuu na si mtu mmojammoja..
 
Hapo kwa nahodha bado kuna utata, mara anashikiliwa na jeshi la police mara amefariki yupo chini....sasa ipi sahihi??. Watulie hadi mwisho na kama hawamjui nahodha bado wafunge vinywa vyao tu
 
I hope umemaanisha MV nyerere..
Tatizo ni kwamba serikali haikujipanga kwenye kuzuia majanga kama haya..na tatzo linaweza kuwa kwny serikali kuu na si mtu mmojammoja..
Serikali iko busy na ujenzi wa viwanda, kwa sasa vinakaribia 4,000. Wacha tupate taabu
 
Wakati zoezi la uopoaji miili ya wahanga wa ajali ya maji iliyotokana na kivuko cha Mv Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi amesema kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati.

Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.

“Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni, ilifanyiwa kazi ambapo tulikuwa tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna gani tunaweza kubadilisha idadi ya safari”, amesema Mkundi

Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
Huu uzi huwezi waona ufipa wakija.
 
"Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni ilifanyiwa kazi na Serikali kwa haraka sana na vizuri ambapo tulikuwa Tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa vizuri labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna ya kupunguza idadi ya safari Mengine tumuachie Mungu"

Joseph Mkundi.
Mbunge wa Ukerewe chadema.
IMG-20180922-WA0067.jpeg
 
Back
Top Bottom