Kwa sasa Taifa linaomboleza kutokana na Kilichotokea huko Mwanza.
Wengi wetu tumekuwa na Kasumba za Kuchukulia Vitu kwa kawaida(Mazoea), ajali hiyo imetokana na Uzembe wa Wathirika, kushindwa kugundua na kuthamini Maisha yao kutokana na tatizo la mazoea "(HUWA) tunapanda usafiri hivi" , Lazima jamii zetu ziweze kugundua kuwa Maisha hayana spare hivyo Hatuna budi kuchukua tahadhali na Kujithamini sisi na Wenzetu. Kama chombo cha Usafiri kimejaa ni vyema ukavuta Subira ukapata kheri kuliko Harakaharaka Isiyo na Baraka. Kama watu wangalikuwa wanalijua hili vifo vya kizembe kama vile Visingalitokea.
Mamlaka za Usafiri pia zinapashwa kutoa Elimu kwa raia na Kuwaajibisha Wavunja Sheria
Kama hizi mamlaka zingalikuwa makini basi wangaliweza kuzuia hili lisitokee, kwq vile watumishi wa hizi mamlaka ni wanajami wenzetu ambao wamezoea kuchukulia mambo kirahisi .
Maeneo kama ya Kariakoo na kwingineko watu wamezoea kupanda Usafiri kwa fujo ama kukimbilia Gari inakuja, nionavyo zile tabia za Mazoea zitakuja kemewa endapo watu wakipoteza maisha. Tahadhali ni Bora kuliko Tiba kama tukiendelea na Tabia hizi tulizojijengea tutaendelea kupoteza ndugu zetu na Kuishia Kubandika picha za Mishumaa Mitandaoni.