Ukarabati wa Barabara ya Tegeta A (Kwa Bedui)

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Ukarabati wa Barabara ya Tegeta A (Kwa Bedui) umeanza baada ya Wananchi kulalamika Ubovu wa Barabara hiyo ambayo imekuwa kero kwa Watumiaji kwa zaidi ya Miezi mitano

Viongozi wetu mpaka tuwashtue kidogo ndio wakumbuke kwamba tumewaajiri


========

Malalamiko ya Awali: KERO - Barabara Tegete A ni kero, kama wameshindwa kuboresha watuambie Wananchi tujichange

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Hongereni kwa jitihada mlizofanya
Jitahidini kufatilia kwa karibu utekelezaji pia ili kuhakikisha mkandarasi anatekeleza kwa ufanisi
Nyinyi watumiaji ndiyo wasimamizi wa kwanza kwa kuwa mnaitumia barabara mara kwa mara
 
Hiyo barabara ni kipengele sana, hapo hadi wajenge lami ndio watakuwa wametatua jambo.

Kulikuwaga na Daladala(Coaster) kutoka Mbezi Mwisho hadi Goba Mpakani kupitia huyo njia ila ziliacha sababu kubwa ni ubovu wa barabara.

Sasahivi zimebaki Bajaj kuanzia hapo kwenye Lami hadi kwa Bedui, chache zinafika Goba Mpakani. Bajaj zinajipigia nauli za juu na watu hawana jinsi sababu kubwa ni ubovu wa barabara.
 
Baada ya malalamiko kuletwa hapa na wadau mbali mbali kuhusu hali ya barabara ya goba tegeta A wakorea road kua mbovu kupitiliza hatimae leo asubuhi barabara imeanza kuchongwa. Shukran za dhati ziwaendee Tarura kwa kusikia malalamiko yetu na pia jamii forums kwa ujumla kwa kupaza sauti zetu Nawasilisha.....
 
Vizuri hakika jamii forum inakua ni sehemu sahihi ya kuwasilisha malalamiko ila tatizo ukarabati unaofanyika pia unakua ni WA kiwango Cha chini sana mvua ikinyesha Tena inarudi kule kule ni vyema mamlaka husika zifanye jambo linalodumu.
 
Mkuu haya maelezo yana ukweli ndani yake??
 
Mkuu haya maelezo yana ukweli ndani yake??
100%

Bajeti ya serikali kwenye hiyo barabara ni kuweka lami, na wananchi hawajui ni lini hiyo lami itawekwa, hivyo wameamua kujiongeza kwa kuunda task force na kukusanya michango!
 
Kazi kazi Meneja wa Tarura Dsm Ni Mtu msikivu na mtu anaefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa sana na Jamii

Heko kwake Eng Mkinga
 
U
Uwezi Jenga barabara ya serikali bila tarura Wala Tanroad ndugu

Ndio umeingia dar Leo na treni la Kigoma au?
 
Weka vizuri ndugu. Wananchi wamechanga fully Hela kurekebisha barabara.
 
Ukisikia kuupiga mwingi ndio huku. Kelele kidogo tu kwa muda mfupi. Tingatinga ndani ya nyumba
 
Waulize hao watu kama hamna mkono wa Tarura hapo

Barabara ya serikali uwezi igusa bila kibali acha ubwege

Kuna miundombinu kama maji, nk chini ya ardhi kima wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…