UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Nguruvi3,

..mazingira ya siasa za Tanzania ni magumu kwelikweli.

..kwanza kuna uthubutu wa kikatili wa CCM.

..halafu kuna wananchi ambao wamezoea kufanyiwa ukatili na wamekubaliana na hali hiyo.

..kwa hiyo vyama vya upinzani vina kibarua kikubwa kwelikweli kupambana ktk mazingira hayo.
Kubwa zaidi ni hili la wananchi kukubali kufanyiwa ukatili na kudhani ni haki yao kutendewa uovu.
Hili ni tatizo kubwa sana.

CCM kufanya ukatili si tatizo kubwa, wanajua wananchi wamekubali kufanyiwa ukatili. Wananchi wakikataa kufanyiwa ukatili CCM itaelekea kule walipopumzika KANU na UNIP.

Swali, ni njia gani itumike ili wananchi watambue kuwa ukatili ni unyama wala si haki wanayopaswa kupewa na CCM?
 
Nguruvi3,

..mazingira ya siasa za Tanzania ni magumu kwelikweli.

..kwanza kuna uthubutu wa kikatili wa CCM.

..halafu kuna wananchi ambao wamezoea kufanyiwa ukatili na wamekubaliana na hali hiyo.

..kwa hiyo vyama vya upinzani vina kibarua kikubwa kwelikweli kupambana ktk mazingira hayo.

Mkuu JokaKuu ndio maana nimesema hapo awali kwamba katika mazingira haya tusitegemee sana Upinzani au UKAWA kwamba wanaweza kutuongoza katika mabadiliko ya njia za amani na kistaarabu kama maandamano, mikutano n.k. Watawala hawako tayari kwa hilo na wameonyesha kuwa wako tayari kufanya lolote ikiwamo kumwaga damu kulinda himaya yao. Wamewapa watendaji wao (Polisi etc) mamlaka ya kugaragaza yeyote atakayejaribu kupiga kelele (kumbuka kauli ya "wapigwe tu")

Tumeona mfano mdogo tu kilichotokea Mbowe alipoitwa makao makuu ya polisi akisindikizwa na wafuasi wake ambao hawakuwa na silaha yoyote wala hawakuonyesha dalili za kufanya vurugu. Lakini polisi waliamua kuact kama wamevuta bangi vile na kutembeza kichapo kwa kila aliyesimama mbele yao ikiwemo waandishi wa habari!

Huu ni ujumbe tosha kwamba mabadiliko tunayoyataka yana gharama kubwa hata ikibidi damu ambayo lazima sisi wote (wananchi na vyama vya upinzani) tuwe tayari kugharamia. Swali ni; Je tuko tayari kuingia gharama hii??
 
Mkuu JokaKuu ndio maana nimesema hapo awali kwamba katika mazingira haya tusitegemee sana Upinzani au UKAWA kwamba wanaweza kutuongoza katika mabadiliko ya njia za amani na kistaarabu kama maandamano, mikutano n.k. Watawala hawako tayari kwa hilo na wameonyesha kuwa wako tayari kufanya lolote ikiwamo kumwaga damu kulinda himaya yao. Wamewapa watendaji wao (Polisi etc) mamlaka ya kugaragaza yeyote atakayejaribu kupiga kelele (kumbuka kauli ya "wapigwe tu")

Tumeona mfano mdogo tu kilichotokea Mbowe alipoitwa makao makuu ya polisi akisindikizwa na wafuasi wake ambao hawakuwa na silaha yoyote wala hawakuonyesha dalili za kufanya vurugu. Lakini polisi waliamua kuact kama wamevuta bangi vile na kutembeza kichapo kwa kila aliyesimama mbele yao ikiwemo waandishi wa habari!

Huu ni ujumbe tosha kwamba mabadiliko tunayoyataka yana gharama kubwa hata ikibidi damu ambayo lazima sisi wote (wananchi na vyama vya upinzani) tuwe tayari kugharamia. Swali ni; Je tuko tayari kuingia gharama hii??
Mwalimu, hatari ninayoiona ni 'fatique''

Hatuwezi kuamini Wananchi watabaki kama walivyo, ipo siku wata react na hapo itakuwa mbaya sana.

Nikubaliane nawe kuwa kwasasa wananchi hawajawa tayari kusimamia haki zao. Ni kama wamekubali kutendewa ukatili ni haki yao. Hata hivyo hiyo isichukuliwe for granted. Gaddaf aliongoza kwa mkono wa chuma, reaction ya wananchi ilipopata msukumo kidogo tu kutoka nje ya nchi, leo hayupo.

Kenya tunafanana kiasi katika utamaduni ingawa wao wapo mbele kupigania haki zao.
Ilipofika tipping point tunajua kilichotokea.

My point ni kuwa kama watawala wangekuwa makini, basi ilikuwa kuwasikiliza wananchi. Kudhani wananchi watakaa kimya kwasababu wamekubali ukatili ni kutengeneza mazingira mazuri ya kuwafanya wapinge ukatili kwa njia zisizo na kizuizi tena zenye gharama.
 
MKAKATI WA KUHALALISHA RASIMU HARAMU
NI DODOMA, NI KUJENGA MAZINGIRA YA MZOGA KUPATA UHALALI
WATATUMIA WELEDI FINYU WA WANANCHI

TULIONYA, MKUU NI NDUMILA KUWILI SASA YANATIMIA
JK NA KIWEWE CHA HOFU YA KIMATAIFA. kUWAALIKA MABALOZI KATIKA UHARAMU NI KOSA


Coming soon
 


Bunge la Sitta limemaliza mazingaombwe. Ni mazingaombwe kwasababu wapowaliokaa nyumbani,wakapewa nafasi ya kupiga kura wala hatudhani kulikuwa nahaja ya kuwa na bunge la katiba.

Jitihada za Sitta zilikuwa kupata2/3. Pamoja na kukosa uhalali, ushawishi na msisimko ,Sitta aliamini katika2/3. Imani ikampeleka kuchakachua, kununua kura na kila aina ya upuuziusiolingana na umri. Ni udanganyifu wa kitoto sana

Mkakati uliopo ni kujenga uhalalikatika haramu ili
igeuke kuwa halali. Sitta na CCM wanaona rasimu yao isivyojadilikakwa watu wenye akili zao.


Tumeona katika mitandao washabikiwaliopewa ‘kazi'' wakihubiri katiba ya Sitta hali ya kudororakama si kususiwa kabisa.


Wananchi wanachotakiwa kufanya nikukaa kimya ili Chenge,Sitta na wenzao wajadili rasimu, wakimaliza tuanzekujadili namna ya kuendelea na rasimu husika.

Katika kujenga uhalali wa haram,CCM na Sitta wameandaa sherehe ya kukaidhi rasimu . Sherehe zitafanyika uwanjawa jamhuri kwa lengo moja tu '' kuwavuta watu'' to rally people ili waanzekuongelea rasimu ya Sitta.

Hakukuwa na sababu za kuwa nasherehe itakayogharimu mamilioni yafedha. Rasimu ya Sitta wangewezakukabishiana ndani ya ofisi za chama Dodoma.Wanajua, mitaani wataungwa mkono ndiohasa sababu ya sherehe

Sitta amealika mbalozi kupitiaserikali ya Tanzania. Hilo ni ushahidi kuwa Serikali ya JK japo inajifanyakukaa pembeni, wao ndio wanaoendesha.

Rais anatarajiwa kukabidhi vyetikwa wabunge. Hiki nacho ni kituko! Wabunge wa CCM walikuwa Dodoma si kwamafunzo au semina, bali kufanya kazi.


Leo Rais anakwenda kukabidhi vyeti, vya ninina ili iweje. Huu ni sehemu ya umasikini wa Afrika.

Lakini pia Rais yule yulealiyekutana na wapinzani na kukubaliana waahirishe mchakato hadi mwakani, ndiyehuyo huyo anarudi upande mwingine kutenda walichokubaliana wakiahirishe.

Kauli ya Kikwete wakati anafunguabunge '' S3 hadi niondoke'' ilikuwa na maana sana.JK alikuwa anaapa hilohalitatokea. Pili, alikuwa anawaelekeza CCM kuhusu msimamo wake. Tatu, alikuwaanapigia chapuo rasimu ya CCM

Hapa tunarudi kusema, undumilakuwili wa mzee si surprise ni mazoea. Wakati UKAWA wakisema anayeweza kukwamuamchakato ni JK, hapa jamvini tulisema (rejea mabandiko) UKAWA wanawezajekumwamini JK aliyesema S3 hadi aondoke, aliyeivuruga tume yake mwenyewe? Naiweje ampe Sitta pesa kama anaamini yale waliyokubaliana? n.k.

Tulionya mikutano kupitia TCD yaakina Cheyo waliomo bungeni ni mtego. Siku atakapohutubia, JK atatumia mkutanowa TCD kuwananga. Tuteleza kuhusu hotuba yake kwa undani.

Tumalizie kwa kusema, mkakati wakualika mabalozi Sitta na CCM wameucheza vibaya. Kwa maneno mengine wamefungua Pandorabox.

Hao mabalozi wana ufahamu mkubwa wa siasa za nchi. Kuwadanganya kwa kura zakununua ni kujidanganya. Hata kama watakuwepo, tayari la kuvunda halina ubani.Sitta anawapa kusema, na watasema.


Tusemezane
 
Nchi nyingi zilizojaa vurugu leo zilikuwa na wananchi wenye hulka kama za Watanzania lakini msukumo kidogo ukageuza kabisa kile kilichofikiriwa kwa miaka mingi na mfano hai ni Ivory Coast ......System inawajibu wa kuhakikisha kipindi hiki cha amani tuna transform mabadiliko ya msingi kwa maridhiano kabla hatujafika pa kuulizana nini kinatokea.....maadui wa ndani na nje ya taifa hili wanazidi kuongezeka kiasi ambacho system pekee bila umoja wa kitaifa hawataweza kuzuia ubaya unaoweza kufanywa ili tuwe Congo ya pili ......
 
Nchi nyingi zilizojaa vurugu leo zilikuwa na wananchi wenye hulka kama za Watanzania lakini msukumo kidogo ukageuza kabisa kile kilichofikiriwa kwa miaka mingi na mfano hai ni Ivory Coast ......System inawajibu wa kuhakikisha kipindi hiki cha amani tuna transform mabadiliko ya msingi kwa maridhiano kabla hatujafika pa kuulizana nini kinatokea.....maadui wa ndani na nje ya taifa hili wanazidi kuongezeka kiasi ambacho system pekee bila umoja wa kitaifa hawataweza kuzuia ubaya unaoweza kufanywa ili tuwe Congo ya pili ......
Kwa bahati mbaya sana fursa za kuleta taifa pamojazinaachwa, kinachoendekezwa ni kugawa wananchi. Hakika kama usemavyo akitokeaadui sasa we're vulnerable. Bunge la katiba lilitakiwa liwe mfano wa Watanzaniakukaa pamsoja na kutengeneza kitu chao.

Kwasasa hilo halipo tena, hakuna kuaminiana kati ya viongoziwa nchi, iwe ndani ya chama au nje. Hakuna kuaminiana katika viongozi waserikali na wapinzani.
Hakuna kuelewana miongoni mwa wananchi.
Tumegawanywa katika misingi ya itikadi za siasa.

Hakuna wa kurekebisha hali hiyo. Kiongozi wa nchi anapokuwa kinyonga ni dalili njema kuwa tumeparaganyika sana.
 
UPINZANI: KINACHOTAKIWA NI VITENDO(ACTION) SIYO HAMAKI(REACTION)

MAALIMU SEIF, UNAJUA UNACHOZUNGUMZA NA MADHARA YAKE?


Inafuata.....
 
UPINZANI: KINACHOTAKIWA NI VITENDO(ACTION) SIYO HAMAKI(REACTION)

MAALIMU SEIF, UNAJUA UNACHOZUNGUMZA NA MADHARA YAKE?


Mara kadhaa wapinzani wamekuwa na hamaki ya kutenda mambo na si maono.
Hili tunalisema kwasababu kila mara wakiambiwa ima hawajifunzi au hawataki kujifunza.

Tumeeleza katika mabandiko mengi ulaghai wa CCM na Rais JK.Hawakutuelewa, leo wanaona kila kilichosemwa ndicho kimetokea.

Tuliwaeleza,mara baada ya kutoka bungeni, ilikuwa muda muafaka kufikisha hoja zao mbele ya mahakama ya wananchi kwa kueleza nini na uhuni gani unaonelezwa na mzee Sitta na genge la CCM.
Hawakusikiliza, wakaonda kwenda kukutana na JK .
Leo CCM wapo barabarani wakinadi rasimu ya Sitta/Chenge.

Kinachofuata ni wapinzani kwenda kukabiliana na CCM wakati fursa hiyo walikuwa nayo hawakuitumia
Katika kukubaliana na CCM wanajikuta wakijadili kisichotakiwa kujadiliwa, ambacho ni kura ya maoni yua ndio au hapana.

Haiwezekani kujadili ndio au hapana katika suala lililojaa uharamu.
Katiba nzima imejaa uharamu na ilikuwa muafaka kwao kuonyesha kwanini kuna uharamu.

1. Ubabe wa wingi na si hoja uliotumika
2. Kubadili kanuni ili kukidhi haja za CCM
3. Kufutwa kwa rasimu ya Warioba yenye maoni ya wananchi na kuingizwa rasimu ya CCM aliyoandaa Chenge.
4. Kigeu geu cha mwenyekiti wa CCM katika suala zima la mchakato, mufaka na majadiliano
5. Uhuni uliotumiwa kupitisha rasimu ya CCM wakiwa wenyewe
6. Kuonyesha mifano ya Zakhia meghji na wabunge wa UKAWA wa siri waliopiga kura za maruhani, mwingine akisingiziwa kupiga kura
7. Kuonyesha jinsi maoni ya wananchi yalivypopuuzwa na kuchukuliwa maoni ya Chenge na Sitta
8. Kuonyesha jinsi Warioba na tume walivyosumangwa kwa takwimu huku Sitta akiwasilisha takwimu za watu 37
9. Kuonyesha jinsi Rasimu ya Warioba ilivyojibu matatizo na kuleta matamanio kwa siku za usoni
10.Na kuonyesha mpasuko wa taifa kutokana na suala la kitaifa kuwa suala la CCM

Kinachotokea ni wapinzania kuhamaki (Reaction) badala ya kuwa na maono (vision) ya kile wanachokusudia kufanya.

MAALIM SEIF ANAJUA ANACHOZUNGUMZA?

Maalim Seif mwenye ushawishi mkubwa kwa siasa za znz ameitisha mkutano siku za karibuni.
Miongoni mwa mengi aliyouzungumza ni kuhusu kuhamasisha umma kupiga kura ya hapana.
Hapa ndipo tunamuuliza kama Maalim anajua anachozungumza!

Kama tulivyoeleza awali, suala si kura ya maoni wala ndiyo au hapana.
Suala zima ni uharamu wa mchakato mzima wa kuandika katiba.
Katiba iliyopendekezwa na wananchi ni ile ya maoni ya tume ya Warioba.

Kwa namna yoyote ile, rasimu ya Warioba ina maelezo, inajadilika na inaweza kukosolewa lakini yapo majibu sahihi kwa mujibu wao.

Rasimu ya Chenge, haina maoni ya wananchi, wala haijajibu hoja za wananchi, maswali, matatizo wala kuweka dira ya taifa.

Rasimu ya Chenge/Sitta haina takwimu, imeandikwa kutokana na maoni ya Sitta/Chenge na wala haina uwakilishi wa wananchi kwasababu sehemu kubwa ya wawakilishi haipo.

Kwa kila kigezo ni rasimu binafsi ya Chenge/Sitta iliyopewa baraka na CCM.

Hivyo, suala zima ni kuhusu rasimu ya Warioba na wala si ya Chenge/Sitta waliodiriki hata kubadilika kanuni na kuiba kura kwa kumtumia Hamad Rashid na Zakhia meghji.

Gazeti la serikali lianonyesha Zakhia ni mjumbe wa kundi la 201 kutoka Tanganyika.
Lakini amepiga kura znz. Hiyo tu ilipaswa kuwa silaha ya wapinzani kuonyesha kuwa hata wanapobaki wenyewe, bado CCM wanalazimika kuiba kura zao.

Maalimu anapojadili kuhusu kura ya maoni ni sawa na kutoa baraka kwa mzoga.
Inapofikia mahali watu wanajadili uzuri na ubaya wa mzogo basi mzoga huo unaanza kupata uhalali.
Maalimu hapaswi kabisa kuhamasisha kuhusu kura ya maoni.

Na hata kura ya maoni lazima ajiulize kama ana uwezo wa kuzia CCM kufanya mambo yao.
Wakiwa 600 wameweza kuiba, huku katibu wa bunge akiendelea kuhesabau kura hadi leo, vipi Maalim anadhani anaweza kuwazuia kuiba kura?

Na kujadili katiba ya Chenge/Sitta kwa kura ya maoni kunawapa CCM nguvu ya kuficha dhambi zao.

Leo wanataka wananchi waanze kujadili kura ya maoni ili wasahau uhuni waliofanya.

Haipaswi kabisa kujadili kura ya maoni, mjadala ulitakiwa uwe kuhusu kukosekana muafaka wa kitaifa, hatari iliyopo hasa upande wa znz, hatima ya muungano siku za baadaye na jinsi ya kuandika katiba nyingine.

Pengine Maalim angeeleweka na duru kama angesema atapiga kampeni ya kuzuia watu wasijadili kura ya maoni au hata kutuhubutu kujiandikisha. Hilo lingeleta maana zaidi kuliko kuanza kuzungumzia kura ya ndiyo au hapana ambazo, kwa kuanzia tu ni haramu.

Tunarudia, kuupa mzoga mjadala wa ndiyo au hapana ni kutaka baadhi ya wananchi waelewe kuwa mzogoa huo una sehemu nzuri na sehemu kubwa ni mbaya.

Huu ni mkakati hafifu sana na sijui kama Maalimu na wapinzani wanauona

Tusemezane
 
KAULI ZA HASSAN NASOR MOYO KUHUSU UCHAGUZI 2010
MWAGA UGALI, NAMWAGA MBOGA
DUKU DUKU LA KATIBA LAZIZIMA TARATIBU VISIWANI

WAPO WAZITO NYUMA YAKE, MWANZO WA HALI TETE VISIWANI


Coming soon
 
KAULI ZA HASSAN NASOR MOYO KUHUSU UCHAGUZI 2010
MWAGA UGALI, NAMWAGA MBOGA
DUKU DUKU LA KATIBA LAZIZIMA TARATIBU VISIWANI

WAPO WAZITO NYUMA YAKE, MWANZO WA HALI TETE VISIWANI

Hivi karibuni mzee Hassan Moyo ameeleza matukio ya uchaguzi 2010.
Habari alizosema hazikanushwa na chombo chochote na inabaki kuwa ndivyo.

Kauli za Hassan Nasor Moyo,mmoja wa wazee waliobaki wenye heshima visiwani haziwezi kupuuzwa.
Ni kauli nzito zinazoashiri mtafaruku mbele ya safari.

Mzee Moyo ni mwenyekiti wa kamati ya maridhiano kule visiwani.
Katika mambo anayosimimia kwa maoni yake, ni msimamo wa serikali 3 na znz yenye mamlaka kamili.
Siku za karibuni amekuwa karibu na viongozi wa tume ya Warioba na wznz wanaopenda mfumo mbadala wa muungano.

Moyo pia anatajwa kuhusika na uandikaji wa katiba ya znz ya 2010 kwa ushawishi ingawa si kiongozi.

Kauli zake za majuzi kuhusu uchaguzi wa CCM na jinsi CCM walivyoshindwa hadi kuombwa Maalim akubali matokeo ni nzito. Amewataja akina Riyami na Karume katika maelezo yake.

Kuwataja kuna maana moja, kwamba walitoa ridhaa ya yeye kusema lolote kuhusiana na uchaguzi kwa kutaja majina yao. Tunakumbuka Aman Karume ndiye aliyesaini katiba ya znz 2010, katiba inayokinzana na ya JMT na pengine ni chagizo la kufanyia mabadiliko katiba ya JMT yaliyokwama.

Kauli ya Mzee Moyo inakuja katika hali mbali mbali

  1. Kuchukizwa na jinsi mchakato wa kihuni wa Sitta/Chenge ulivyomalizika kwa kuungwa mkono na baadhi ya wawakilishi wa znz.
  2. Kutoridhishwa na kitendo cha Mansour Himid ambaye ni mshirika wake kuwa na kesi mahakamani ambayo inamfunga mdomo wa kutetea kile wanachokion sahihi
  3. Kuona ile znz waliyoitaka sasa haitakuwepo tena kwa mkono wa wazanzibar wenyewe

Ni kwa mantiki hiyo, Mzee Moyo ameamua ''mwaga mboga namwaga ugali'' kwamba hana cha kuficha na haielekei siku za usoni atakuwa msuluhishi katika mazingira tata kama yale ya 2010.

Yote hayo yanatokana na uhuni wa mchakato uliomalizika Dodoma kwa CCM kufanya mambo yao ili yawe mambo ya taifa.

Kwa mtazamo mwingine, Moyo anaonyesha jinsi gani hali itakavyokuwa tete mwakani huko znz.
Na alichokisema ni ujumbe kuwa hamkani si shwari tena.

Kauli za Moyo zisichukuliwe kwa wepesi kama ''loser'' bali kwa weledi na uangalifu.

Wazee wenye ushawishi wanapojitokeza hadharani na kumwaga siri zilizokuwa hazijulikani ni jambo la kufikirisha.

Pamoja na hayo, Moyo anaungwa mkono na wazito ambao kwa namna moja au nyingine hawakuridhishwa na uhuni uliokamilika Dodoma. Hivyo si Moyo peke yake nyuma yake kuna wazito.

Wazito hao wana duku duku na pengine wanachelea kujitokeza yasije wakuta yaliyomkuta Manosur Himid.
Moyo ni kigingi ambacho CCM haikiwezi hata kidogo. Ingalikuwa CCM wana uwezo, basi wangeshamuondoa uanachama.

Hivyo katika duku duku la katiba, Mzee Moyo ni kipaza sauti cha wazito wengi walio nyuma ya znz na duku duku.
Hilo tu limeshawagawa wazanzibar na mwakani au kabla ya hapo lazima yatatokea mambo mazito.
Mambo kama yale ya siku za nyuma.

Uhasama miongoni mwao sasa unafikia hatua ya juu. Ni hali inayozimama kichini chini, ni suala la muda kutalipuka tena.

Kama JK alidhani anaweza kuwafurhisha wznz kwa namna anavyofanya, basi anaweza kujikuta anamaliza muda wake akiwa na madoa kama yale ya Mkapa.

Tusemezane
 
Nguruvi3 kwani unafikiri hayo ulioyasema hapo juu hawayajui. Wanayajua sana lakini wanaona kwani wana kitu gani cha kupoteza ikiwa mambo yataharibika. Wanajua kwamba wanauwezo wa hata kuhama nchi.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Nguruvi3,

Ni wewe siyo muda mrefu ulikuwa unawananga Wazanzibari na kusema ni waongo, vigeugeu, wanafiki, etcetera, etcetera.

Umegeuka tena, hapa unakuja na hoja eti kauli zao tuzichukulie kwa weledi na uangalifu!.

Yaani unataka kauli za waongo, wanafiki na vigeugeu kama ulivyo wahukumu tuzichukulie kwa weledi na uangalifu kwa vile kile wamekisema kile unapenda kukisikia, kwa sababu kinapendezesha fikra na mtazamo wako.

Mtu wenye fikra pevu hawezi kuchukulia kauli ya muongo, mnafiki na kigeugeu kwa weledi na uangalifu. Labda utueleze kile ulichokisema siyo hali halisi ya Wazanzibari.

Wewe umeleta hoja katika thread hii,
Ukasema hivi,
3.Unafiki
Hawa wznz ndio walikuwa vinara wa kukataa muungano, kuukata Utanzania na kufanya uhuni wa kihaini kwa vile hawana heshima na Utanzania.

Mwaka 2010 akina Pandu Kificho, Seif Khatibu, Nahodha, Mohamed Aboud na wengine walikuwemo ndani ya BLW kuhalalisha katiba yao kwa kuondoa mammbo ya muungano, kudharau katiba tena bila kujadiliana na Watanganyika.

Ni hao hao wamerudi Dodoma na kutenda kinyume ya kile walichotenda siku za nyuma.
Huu ni unafiki na haujibiwi bali kusemwa watu wana chuki na wznz.

Hapa wenye chuki na znz ni wanz wenyewe kwa koti la unafiki.
Kama huo ni utamaduni wao hatutaupaka rangi, tutawaeleza ni wanafiki wakubwa.

4. Vigeuge
Ni hao wznz waliosema Tanganyika imevaa koti la muungano. Leo wanahalilisha uhuni kwa koti lile lile wanalosema ni la Muungano. Wakairudi znz wanakana yale yale waliyoyatenda Dodoma.

Huku ni kuwa vigeu, si chuki. Kama ni chuki tuonyeshwe wapi ni uongo umesemwa.
Ukweli unabaki kuwa ni vigeugeu na hatuna neno jingine zaidi ya hilo

5. Waongo
Tabia ya uongo nayo ni sehemu ya uzanzibar. Leo namba zinaonyesha bila kificho kuwa hakuna mahali znz inanyonywa.
Kinyume chake ipo mgongoni kwa raha zao kwa gharama za kodi za Mtanganyika.

Ule uongo wa kunyonywa, kuonewa sasa umekwisha.
Tukisema ni waongo wazuri sana tunaambiwa tuna chuki. Hebu tuelezwe neno gani litumike kwa mwongo kama mznz.

Hayo ni kwa uchache tu, lakini muhimu sana ni Watanganyika kubaini kuwa huu muungano unawaumiza.
Kodi zao ndizo zinatumika kuhudumia Rais, na makamu 2 wa visiwa vyenye uchumi kama znz.

Ndizo zinatumika katika ulinzi na usalama, mambo ya ndani, taasisi kama elimu na kufidia bajeti ya znz huku znz ikitoa misamaha ya kodi hovyo, ikiacha kukusanya kodi. Wote huo ni mzigo alioubeba Mtanganyika katika pay cheque yake kila mwezi. Ni mzigo anaoulipia Mtanganyika katika bidhaa anazonunua.

Haya lazima yasemwe, na anayedhani ni chuki aje aonyeshe chuki ipo wapi.
Kwa watu wasiofuatilia hoja zako hapa Jamiiforums hawawezi kuelewa nini kilichoko nyuma ya hoja zako ambazo zinabadilika kulingana na mazingira kama ilivyokuwa kwa hoja za kikundi kinachojiita UKAWA.

Mpaka uchaguzi mkuu upite, tutasoma na kusikia mengi kutoka kwenu ''wataalam wetu'' wa mambo ya kisiasa!.
 
Ndugu Nguruvi3,

Ni wewe siyo muda mrefu ulikuwa unawananga Wazanzibari na kusema ni waongo, vigeugeu, wanafiki, etcetera, etcetera.

Umegeuka tena, hapa unakuja na hoja eti kauli zao tuzichukulie kwa weledi na uangalifu!.

Yaani unataka kauli za waongo, wanafiki na vigeugeu kama ulivyo wahukumu tuzichukulie kwa weledi na uangalifu kwa vile kile wamekisema kile unapenda kukisikia, kwa sababu kinapendezesha fikra na mtazamo wako.

Mtu wenye fikra pevu hawezi kuchukulia kauli ya muongo, mnafiki na kigeugeu kwa weledi na uangalifu. Labda utueleze kile ulichokisema siyo hali halisi ya Wazanzibari.

Wewe umeleta hoja katika thread hii,

Ukasema hivi,

Kwa watu wasiofuatilia hoja zako hapa Jamiiforums hawawezi kuelewa nini kilichoko nyuma ya hoja zako ambazo zinabadilika kulingana na mazingira kama ilivyokuwa kwa hoja za kikundi kinachojiita UKAWA.

Mpaka uchaguzi mkuu upite, tutasoma na kusikia mengi kutoka kwenu ''wataalam wetu'' wa mambo ya kisiasa!.
Marehemu baba yangu aliwahi kuniambia kuwa ukimsikia mwendawazimu anaongea msikilize, huenda ukapata neno. Ni mgonjwa lakini ana ufahamu na mazingira yake. Haongei lugha nyingine anaongea kilichopo.

Nimesema wznz ni vigeuge na waongo. Na nikasisitiza kuwa ni wanafiki. Hayo yanabaki kama yalivyo.
Tulichokifanya ni kupima na tathmini ya maneno ya Mzee Moyo.

Hatukusema hivyo bila kuonyesha wasifu wake.
Hatkusema alichosema ni ukweli au uongo, tulichosema huyu ni mzee mwenye ushawishi, ameshiriki siasa za znz kuanzia enzi.

Pia ameshiriki maridhiano yaliyozaa utangamano uliopo na pia kubadili katiba. Kauli na ushawishi wake lazima viangaliwe kwa jicho pevu.Hiyo ni raia yetu na wala hatusemi au kulazaimisha mtu kukubaliana nayo.

Unachokifanya ni kupinda tahmini ili kupata ubaya wa duru na kuusema.
Tafadhali angalia mada, nini kinaongelewa na kwa mukatadha gani halafu changia.

Hapa hakuna spinning bali hoja. Nilitegemea ujibu hoja kuwa yeye si CCM na wala hajasema.
Midhali umekubali kasema, basi hiyo uliyosoma ndiyo tathmini yetu. Je, tathmini yako ni ipi?
 
Ndugu Nguruvi3,
Kwa watu wasiofuatilia hoja zako hapa Jamiiforums hawawezi kuelewa nini kilichoko nyuma ya hoja zako ambazo zinabadilika kulingana na mazingira kama ilivyokuwa kwa hoja za kikundi kinachojiita UKAWA.

Mpaka uchaguzi mkuu upite, tutasoma na kusikia mengi kutoka kwenu ''wataalam wetu'' wa mambo ya kisiasa!.
Nashukuru unafuatilia JF. Nimefarijika kumbe unasoma pia. Ahsante

Duru tunasimama katika hoja. Nilitegemea ungeonyesha wapi zinabadilika. Hakuna
Kwasa kazi yako kubwa ni kutafuta mistari ufanye spinning. Kwakweli si njia njema maana kadri unavyotafuta mistari unataupa nafasi zaidi ya kufafanua. Kama ndio kusudio umefanikiwa, vingenvyo utakuwa umeingia forum isiyokuhusu.

Najua kuwa hoja za duru ni mwiba sana. Sitegemei na wala nsingependa CCM yoyote anipende. Nchi yangu inanipenda zaidi ya CCM.Tutaweka ukweli uwe unachoma au kuunguza.

Huko nyuma ulisema probability, nadhani umeridhika si probability.
Tuliandika hata kabla ya bunge kuwa Sitta atavuruga mchakato, sasa ni hadithi, yametokea
Tukasema Chenge ana rasimu yake mfukoni, sasa ni hadithi, imetokea.

Sitegemei wewe au Chenge wafurahie mabandiko ya duru.

Endelea kujifunza, maana elimu ni dhamana, wenyewe wakiihitaji unawapa ( Mohamed Said)
 
KAULI ZA HASSAN NASOR MOYO KUHUSU UCHAGUZI 2010
MWAGA UGALI, NAMWAGA MBOGA
DUKU DUKU LA KATIBA LAZIZIMA TARATIBU VISIWANI

WAPO WAZITO NYUMA YAKE, MWANZO WA HALI TETE VISIWANI

Hivi karibuni mzee Hassan Moyo ameeleza matukio ya uchaguzi 2010.
Habari alizosema hazikanushwa na chombo chochote na inabaki kuwa ndivyo.

Kauli za Hassan Nasor Moyo,mmoja wa wazee waliobaki wenye heshima visiwani haziwezi kupuuzwa.
Ni kauli nzito zinazoashiri mtafaruku mbele ya safari.

Mzee Moyo ni mwenyekiti wa kamati ya maridhiano kule visiwani.
Katika mambo anayosimimia kwa maoni yake, ni msimamo wa serikali 3 na znz yenye mamlaka kamili.
Siku za karibuni amekuwa karibu na viongozi wa tume ya Warioba na wznz wanaopenda mfumo mbadala wa muungano.

Moyo pia anatajwa kuhusika na uandikaji wa katiba ya znz ya 2010 kwa ushawishi ingawa si kiongozi.

Kauli zake za majuzi kuhusu uchaguzi wa CCM na jinsi CCM walivyoshindwa hadi kuombwa Maalim akubali matokeo ni nzito. Amewataja akina Riyami na Karume katika maelezo yake.

Kuwataja kuna maana moja, kwamba walitoa ridhaa ya yeye kusema lolote kuhusiana na uchaguzi kwa kutaja majina yao. Tunakumbuka Aman Karume ndiye aliyesaini katiba ya znz 2010, katiba inayokinzana na ya JMT na pengine ni chagizo la kufanyia mabadiliko katiba ya JMT yaliyokwama.

Kauli ya Mzee Moyo inakuja katika hali mbali mbali

  1. Kuchukizwa na jinsi mchakato wa kihuni wa Sitta/Chenge ulivyomalizika kwa kuungwa mkono na baadhi ya wawakilishi wa znz.
  2. Kutoridhishwa na kitendo cha Mansour Himid ambaye ni mshirika wake kuwa na kesi mahakamani ambayo inamfunga mdomo wa kutetea kile wanachokion sahihi
  3. Kuona ile znz waliyoitaka sasa haitakuwepo tena kwa mkono wa wazanzibar wenyewe

Ni kwa mantiki hiyo, Mzee Moyo ameamua ''mwaga mboga namwaga ugali'' kwamba hana cha kuficha na haielekei siku za usoni atakuwa msuluhishi katika mazingira tata kama yale ya 2010.

Yote hayo yanatokana na uhuni wa mchakato uliomalizika Dodoma kwa CCM kufanya mambo yao ili yawe mambo ya taifa.

Kwa mtazamo mwingine, Moyo anaonyesha jinsi gani hali itakavyokuwa tete mwakani huko znz.
Na alichokisema ni ujumbe kuwa hamkani si shwari tena.

Kauli za Moyo zisichukuliwe kwa wepesi kama ''loser'' bali kwa weledi na uangalifu.

Wazee wenye ushawishi wanapojitokeza hadharani na kumwaga siri zilizokuwa hazijulikani ni jambo la kufikirisha.

Pamoja na hayo, Moyo anaungwa mkono na wazito ambao kwa namna moja au nyingine hawakuridhishwa na uhuni uliokamilika Dodoma. Hivyo si Moyo peke yake nyuma yake kuna wazito.

Wazito hao wana duku duku na pengine wanachelea kujitokeza yasije wakuta yaliyomkuta Manosur Himid.
Moyo ni kigingi ambacho CCM haikiwezi hata kidogo. Ingalikuwa CCM wana uwezo, basi wangeshamuondoa uanachama.

Hivyo katika duku duku la katiba, Mzee Moyo ni kipaza sauti cha wazito wengi walio nyuma ya znz na duku duku.
Hilo tu limeshawagawa wazanzibar na mwakani au kabla ya hapo lazima yatatokea mambo mazito.
Mambo kama yale ya siku za nyuma.

Uhasama miongoni mwao sasa unafikia hatua ya juu. Ni hali inayozimama kichini chini, ni suala la muda kutalipuka tena.

Kama JK alidhani anaweza kuwafurhisha wznz kwa namna anavyofanya, basi anaweza kujikuta anamaliza muda wake akiwa na madoa kama yale ya Mkapa.

Tusemezane

CCM WAMJIBU NASOR MOYO KIMYA KIMYA
DALILI YA MANENO MAZITO KUWAINGIA

RAIS WA ZNZ ATAMBA HADHARANI, TUMEPATA FURSA ZAIDI TANGANYIKA
WATANGANYIKA KUENDELEA KUBEBA MZIGO WA MUUNGANO, FARAJA NI ZANZIBAR

Bandiko hapo juu tumeeleza jinsi Moyo alivyo na ushawishi wa siasa za znz.
Katika mkutano wa Kibanda maiti, Rais Shein amemualika mwanapinduzi mzee Himid Ameir ili azungumze kuhusu mapinduzi.
Hii ilikuwa katika kampeni za kura za maoni za CCM ingawa haijulikani katika CCM ni utaratibu gani unaotumika.

Kinachoweza kukubalika ni kuwa CCM wana uhuru wa kufanya jambo bila ridhaa ya wananchi wa itikadi zingine za kisiasa au wasio na itikadi.

Hivyo mkutano wa Dr ni halali na wala hauna shaka kwavile ameenda kunadi katiba ya CCM iliyoandikwa na Chenge/Sitta

Mzee Ameir hajulikani katika siasa za znz. Katika hali ya kuogopa maneno mazito ya Mzee Moyo na hali tete ya kisiasa, CCM wameamua kutafuta watu wa umri ili kuja kuzungumzia mapinduzi na katiba yao.

Mzee Ameri ameitwa ili kumjibu Mzee Moyo kwasababu ndani ya CCM hakuna anayeweza kumgusa achilia mbali kumjadili.
Hawa akina Nape na Mwanadiwani, walikuwa hawajazaliwa wakati Moyo akiwa madarakani.

Hawana ubavu wa kumwita na kwa kuzingatia sana ushawishi wake. Kumtisha kama walivyofanya kwa Mansour Himid haiwezekani.

Ni kwa muktadha huo, wameamua kumjibu kwa kumtumia wazee wengine.

Katika mkutano huo, Rais SHein amesema znz imeshiriki kikamilifu kuandika katiba ya Chenge na Sitta.
Hapa ndipo tunasema kuna unafiki na kigeugeu au uongo.

Ilikuwaje wakati wanabadili katiba ya znz 2010, Rais Shein hajalizungumzia hilo.
Inakuwaje wadai kushiriki katika maamuzi ya mambo ya Tanganyika ikiwa wao hawaitambui katiba ya JMT tena kwa dharau.

Lakini pia kauli zake zinashangaza sana. Rais Shein anasema wananchi wa znz waamue.
Katika mkutano huo ulikokuwa wa CCM ni jambo la kushangaza Rais wa znz akiongelea suala la wananchi wote wakati anaongea na wana CCM.Hizo zote ni jitihada za kuipa shamra shamra katiba ya Chenge na Sitta iliyo dorora na kukosa mashiko.

Miongoni mwa mambo aliyosema Shein ni suala la mafuta na gesi kuondolewa katika muungano.
Hapa ndipo anapowaambia Watanganyika jambo wasilojua.

Mafuta na gesi ya Tanganyika itatumika katika muungano. Kwamba, badala ya kuwanufaisha Watanganyika, rasilimali hiyo itakwenda znz kuziba pengo la bajeti, kulipa mishahara ya SMZ na kulipia gharama za Rais na makamu lukuki wa kisiwa chenye uchumi wa bilioni 400 kwa mwaka.

Watanganyika wangeuliza, endapo wznz wameondoa gesi na mafuta ili wajinufaishe, kwanini gesi na mafuta ya Tanganyika itumike kubeba muungano? Kwanini liwe jambo la muungano ikiwa upande wa znz jhawataki.

Jibu la swali hilo ni rahisi sana, kama huna Tanganyika basi una Tanzania ambayo znz imo na hivyo wao kuja kuchukua chako ni halali. Wewe si mzanzibar ni Mtanzania hivyo huwezi kudai chao.

Ni kwa muktadha huo, kila siku tunawakumbusha Watanganyika kuwa wznz huja katika muungano kwa jina na pale penye masilahi.Mumemsikia Rais wa zanzibar akitamba jinsi wanavyonufaika na fursa akimaanisha rasilimali za Tanganyika.

Bila Tanganyika, wznz wataendelea kwafanya Watanganyika shamba la bili.
Hili ndilo Watanganyika wanapaswa kujiuliza na kufikiri na si kufikiri kura za maoni za CCM.

Kura ya maoni inawekewa shamara shamra kuwasahulisha Watanganyika kuwa suala zima halina uhalali.
Ni uhuni uliofanywa kuchukua rasimu iliyoandikwa na Chenge ambaye si tu maadili yake yanatia shaka bali pia ameshiriki kuiba hata kura za CCM wenzake akishirikaiana na Sitta(Megji na wengine)

Wananchi lazima watafute majibu ya maswali magumu kuhusu muungano na wala waasifikirie kuhusu katiba ya CCM na Chenge/Sitta. Hiyo ni katiba yao hivyo waachwe waendelee na katiba yao.

Wananchi waulize
1. Matatizo ya miaka 50 yamepatiwa ufumbuzi gani
2. Suala la gharama kwa mujibu wa rasimu ya CCM inayotaka kufanywa ya taifa limepungua ukilinganisha na Warioba?
3. Muundo wa muungano unatoa haki kwa pande moja, je pande ya pili ambayoni Tanganyika ipo wapi?
4. Kwanini Mtanganyika alipe kodi, atumie raislimali zake kwa ajili ya nchi jirani ya znz?
5. Utegemezi wa znz na uwekezaji wa Tanganyika una manufaa gani kwa walipa kodi wa Tanganyika
6. Je, suala la znz kuwajibika katika muungano limepatiwa majibu?

Bila kujiuliza maswali hayo, tutaendelea kuwasikia wznz wakitamba na fursa kama alivyotamba Shein.
Kwamba mdudu kupe yupo mgongoni na bado anadai fursa za kumnyonya ng'ombe tena kama haki yake.

Bila kuamka, Watanganyika wataamka kila asubuhi kung'ang'ania dala dala ili kwenda kulipa kodi zaidi kwa nchi jirani ya znz.

Wakati huo huo wznz wanatoa misamaha ya ndugu zao, wanaacha kukusanya kodi wakijua shamba la bibi ni Tanganyika.

Huko Tanganyika wanapata 4.5% ya kodi ya Mtanganyika, wanasoma bure, wametengewa fursa kama ajira zao peke yao bila formula. Wao kila jambo wameliwekea uzio tena mahususi kukabiliana na Mtanganyika.

Tusemezane
 
Back
Top Bottom