UKAWA Wapuuzwe!

mlengo wa Kati simama hapo Kati Kati usiegemee CCM wala UKAWA chombo cha Habari kazi yake ni kubalance Habari , yaani kinachukua pande zote si kuegemea upande mmoja.
 
Tena sio Millard tu, hiyo radio Clouds yote ni wana CCM, kiongozi wao ndio alipata tenda ya kuaandaa venue ya kufanyia mkutano Mkuu wa CCM uliopita kwa hiyo nyimbo zao ni CCM. Watangazaji karibu wote wako biased sana na wanafagilia sana CCM hawa wanatumiwa hawa na ukizingatia wengi wao ni ma radio DJs sasa sijui kama wanajua ethics za utangazaji kama inavyotakiwa
 

huyu dogo huwa namfatilia sana.nyenendo zake katika kutumia vyombo vya habari kuadres issues mbalimbali hasa za kisiasa ni biased kwa upandewa ccm.anakera sana sana.pamoja na ujana wake anakosa weledi japo wa kung'amua.nimetokea kumchukia hamna mfano.
 
Hivi huyu jamaa alisharudisha ipad ya mdada aliyoikomba kule mjengoni?
 

Hii ni aibu kwa taifa. Cjui mfumo wa kutoa vibal vya uwindaji uki vip maana kinachofanyika pale loliondo ni aibu kwa taifa. Ila ipo siku
 
...most of you guys need to go for 'Head' checkup. Hivi mnadhani mtabaki madarakani milele? Katiba siyo ya CCM, kama mnataka kutunga ilani yenu watu wa Lumumba haina sababu ya kutumia 'National Resources' kufanya hivyo. Mmejisahau sana.
 

Mimim mwenyewe nilitaka nimjibu kama wewe! Nikatulia kwanza, nikarudia kusoma uzi wake. Nikarudi kuangalia title yake, nikaamua kumwacha kama alivyo!!
 
MKUU makonda nimepitia uzi wako, kisha nikapitia kwenye hadhara ya watu uliowaita wakusikilize yaani Jf members, nashindwa kuelewa kwa nini karibia wote wamejibu kwa matusi kama ulivoandika kwa matusi.
Mkuu inafaa nyie kama ccm mkae mtafakari je mnapowaruhusu watanzania waanze kuhoji kwa nini viongozi wa taifa ili mnaanza kutukana matusi ni dalili ya kutimiza miiko ya utawala au ni kuchanganikiwa au ni kejeli kwa watanzania?

Nyie mna dola, au kwa ufupi niseme tu mnao uwezo wa kuunda au kubomoa,je kwa nini muanze kutaja matusi sijui bwana za cuf, nccr ,cdm , tume zoote za akina kisanga, warioba na wasomi kuwa wanawatukimia mabwana zao ni hekima? je nyie mnawatumikia mabwana wapi?au wao wana mabwana ila nyie mna nini?

Kiukweli siasa za taifa ili ni za ovyo kabisa. Mkuu makonda, unaridhishwa na tabia za bunge lenu za kutaja matusi mfano kumuita raia mwenzio SHETANI, mara MABWANA, mara KUUKALIA, mara BUSHA, je unahisi watanzania wanasubiri kauli izi kwa hamu?

Mkuu, rais kikwete alizindua rasimu, akakabidhibiwa kwa hafla nzito ya kutumia mamilioni , ikachapishwa na taasisi ya kiserikali kwa gharama za walipa kodi, akawateua nyie mkale kodi zetu, leo hii mnasema alichopokea kwa shangwe na sifa kedekede kilikuwa kiini macho?
Juzi nilikuta cd moja mtaani watu wanasikiliza, ikawekwa kipande cha video jk anahutubia wakati anazindua tume, kikachomekwa kipengele anapokea taarifa na rasimu ya tume, wakakata wakaweka kipengele cha kuzindua bunge ambako anakana sifa zooote alizoimwagia tume...huwezi kuamini kama ni mtu mmoja aliongea matamshi ayo...yaani ya kwanza ni kinume cha ya mwanzo!

Mkuu, sina budi kukufikirisha au kukuudhi, kwa matusi uliyoleta sio ya kujenga bali matusi, ndio maana watu badala ya kukujibu wakatukana pia. mimi siwezi kukutukana ili kujibu ayo matusi ila kiujumla hamjengi taifa mnalioboma.
Niliwahi kuwaambia apo nyuma, kama hamuitaji vyama vya siasa, rais kikwete anao uwezo wa kuamuru vifutwe, turudi kwenye udikteta, ila kama mkikubali ivi vyama viwepo basi wasikilize maana ni wenzenu.binafsi natamani siku moja ivi vyama vyoote ccm, cdm , nk nk vifutwe nchi itulie...udini umeletwa na nyie wanasiasa, ukabila, ukaskazini , uchaga, mfumo kristo, uislamu, ughaidi nk nk ni nyie wanasiasa mnaleta!

Mkuu sitaweza kuendelea kuchangia kwa kuwa apa hatujengi tunabomoa...izi kauli za kuongozwa na jeshi, nk nk ni kama zile za BORA TUKOSE WOTE, hatuachii, wala hatuchukui.
MKUU, kwa ujumla awa wapinzani ni wachache alafu sio wakorofi, wanaongea sana ila vitendo vibaya hawana, nakushauri tu badala ya kuanza ligi na kujiandaa kuua watu kama ulivotangaza kuwa green guard wajiandae, msifike uko, fanya mpango mkae nao muyamalize, uku uraiani wengi hawako na nyinyi , pitia mtaani msikilize mawazo huru, ila mkitaka yale ya kusifiana tu ...mjue mnasifiwa kinafiki ila watu wako katikati na wengi upande wa kushoto.
Ni ayo kwa leo!
 
Mkuu acha kubabaisha watu wewe umeandika nini sasa ni sawa na zero kabisa makonda kaweka andiko lenye mashiko na hoja ndani yake wewe na ubavicha wako unaleta porojo.

Sikushangai kwa hiki ulichoandika hapa. Uwezo wako wa kufikiri umeishia hapo.
 
Wakumbuke hakuna cha milele, wengi walikuwepo leo wako wapi, na wakae wakijua kuna kizazi hakitakuwa na nidhamu ya woga, tutegemee nini??? Ni mtazamo tu.
 
tuanze kuwapuuza watu wa siasa kama wewe ndipo tufanye tathimini ya wanachofanya ukawa.
 
Nimepuuza huu uzi Nimeishia aya ya pili Kama mkuu hajui hata buffoon dah! Hajaangaika hata 'ku-google'.....................naisikitikia Tanzania.
 
Hivi ndugu yangu umesoma shule gani wewe?! Hujui hata chama kinachoongoza Kenya kilikuwa cha upinzani enzi ya KANU madarakani sasa je hivi vyama vilivyopo madarakani Kenya vinanufaisha nchi za nje? Acha kufikiri na kuandika kwa kuwa unataka madaraka, andika kwa kuwa unaelewa usemalo na ni sahihi. UKAWA itapuuzwa na wanaccm waliopo madarakani kimkandamkanda tu, ila wenye kujielewa hawataipuuza kamwe.
 
Hapa naona Bwana Makonda ameteleza. Katika kiingereza hakuna neno BAPHOON bali kuna neno BUFFOON. Ni bora atumie lugha anayo iweza!

A buffoon is someone whose ridiculous behavior is a source of amusement to others. People you might call a buffoon are a political rival or the guy at work who tells silly jokes at office parties.
 
Paul Makonda ni kichwa sana. Hongera sana. Vijana tumekuelewa hawana lao wanafiki hawa
 
Makonda atawasumbua sana kwenye siasa za taifa hili dogo anahoja sana.

Nimefurahi kuwa ulimtambua tangu enzi za enzi. 😀

Mimi nilianza kumfatilia zamani kwa kumsoma humu na kula kobisi.

Makonda oyeeee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…