Ukiachana na kondomu, neti na dawa za kufubaza makali ya UKIMWI; aina gani ya msaada mingine kutoka USAID?

Ukiachana na kondomu, neti na dawa za kufubaza makali ya UKIMWI; aina gani ya msaada mingine kutoka USAID?

Wabongo sie ku&mme hizo data za hayo ma usd bilioni mbona hatuzioni kwenye takwimu za hao wafadhili wenyew , nyie mnazitoa wapi au ndo na hao wafadhili nao wanaficha kias halisi Cha pesa wanachotupa kama msaada
Kwa sababu hamna freedom of information act (FOI) kama wenzenu basi huwezi kupata
Labda wapitishe hiyo sheria ya kuwa yeyote anaweza kupata taarifa zozote za Umma mda wowote akihitaji
Hakuna anaetaka hii kwenye serikali zetu nyingi maana ni kuweka wizi wao hadharani
 
  • Thanks
Reactions: apk
Japo gharama za kupata ARV zipo juu Ila sifikirii Kama tutashindwa kulipia hizo dawa.

Je kwann mnamlaani trump?
Kama wewe unaweza, si watu wote wenye HIV wanaweza. Ajabu unakuja na sweeping statement kuwa hufikirii kama tutashindwa kulipa!. Wanaolipa na walioathirika na ni wa ngazi zote toka matajiri mpaka maskini.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Hivi kuna misaada ya bure kwel wakuu au kuna namna tunalipia indirect, siamini wana mahela yamekaa tu kusaidia supposedly vitukuu vyaa zinjathropas huku.. fort knox yenyewe inasemekana hamna kitu gold yote walipurura kwenye mavita
 
  • Thanks
Reactions: apk
kuna wajinga wanaona hamna tatizo USAID kuondoka ila kiama chake tutafurahi

US anataka kuwa kama mchina, baada ya kuona watu wanatukana misaada yake....
wasamehe mkuu sio kosa lao. tatizo wengi hawajui haya mambo yanavoenda wanafikiri hii misaada inawagusa wa maofisini na wanywa ARV tu na ivyo misaada ikikata basi hao tu ndo wahanga.

ukitembelea uko fesibuku na insta uko ndo wamejaa wa mawazo km hayo. cha ajabu hata humu jF ambako ulitegemea kuna watu wenye uelewa mkubwa na wao wanafanya makosa yaleyale kama wale wa fesibuku.

apo ni ishu ya uelewa tu. watu inabidi waelewe yuesi wanachangia pakukwa sana kwenye maendeleo yetu. hata hizi barabara tunazopita nyingi ni pesa za hao yuesi.

miradi ya umeme maji elimu uko shule kibao zimejengwa kwa mtonyo wao. sasa ni ajabu leo unasikia mtu anashangilia nchi kukosa misaada.😳apoapo mtu uyu unakuta ana watoto anasomesha sasa unategemea uyo mtoto akimaliza shule anaenda wapi atajiliwa wapi km hatuna izo shule. unaona huyu mtu hajitambui

madhara ya kujitoa hawa jamaa ni makubwa sana na yanaweza kukufata ukouko kwenu uliko tusiwe wa kushangilia tusichokijua.
 
Wanasaidia mambo mengi sana ambayo mwananchi wa kawaida haambiwi kabisa
Na kama kila kitu wanachotoa kingewafikia walengwa basi kusingekuwa na shule isiyokuwa na vitabu na madawati na vyoo
Wafadhili wanatoa hela na vifaa kwa Elimu, kilimo, afya na hata chakula
Kwa hiyo sio condom tu
Kwani hatuwezi kuanzisha vyondom vyetu vya asili?
 
ni kweli kuna namna na wao wanafaidika ila pia ujue hao jamaa hawana roho mbaya kama sisi.
Kabisa misaada ya bure labda ya mashoga ili waendeleze kampeni yao na machanjo(vaccine) ambayo ya athari kifupi misaada sio mizuri hasa unapoigeuza kua haki yako
 
Kwn bi ushungi hawez kwnd kujitongozesha kwa dingi mbn ana 👀 ya kushawishi angalau na yeye atusaidie kwa hilo
 
Japo gharama za kupata ARV zipo juu Ila sifikirii Kama tutashindwa kulipia hizo dawa.

Je kwann mnamlaani trump?
ARV, VITENANISHI, MASHINE ZA UCHUNGUZI PAMOJA, MISHAHARA NA MAINTANCENCE, MAGARI, nia vikolokolo vingiii, kumbuka hizo gharama hazikuwekwa kwa bJETI YA 2024/25
 
Google ingekusaidia

USAID (United States Agency for International Development) ni shirika la misaada la Marekani linalotoa msaada wa maendeleo kwa nchi mbalimbali duniani, ikiwemo Tanzania. Kazi kuu za USAID ni:

1. Maendeleo ya Uchumi – Inasaidia kukuza uchumi kwa kuwekeza katika biashara ndogo, kilimo, na ujasiriamali.


2. Afya – Hutoa msaada kwa miradi ya afya, kama vile kupambana na malaria, VVU/UKIMWI, lishe bora, na afya ya mama na mtoto.


3. Elimu – Inasaidia upatikanaji wa elimu bora, hasa kwa watoto wa kike na jamii zilizo pembezoni.


4. Utawala Bora na Demokrasia – Inasaidia kuimarisha demokrasia, haki za binadamu, na utawala wa sheria.


5. Misaada ya Dharura – Hutoa msaada wa kibinadamu wakati wa majanga kama vile mafuriko, njaa, na migogoro ya kivita.


6. Mazingira na Nishati – Inasaidia miradi ya uhifadhi wa mazingira, nishati mbadala, na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.



USAID inashirikiana na serikali, mashirika ya kiraia, na sekta binafsi ili kuhakikisha maendeleo endelevu. Tanzania ni moja ya nchi zinazopokea msaada mkubwa kutoka USAID, hasa katika sekta za afya, elimu, na kilimo.
Kuuliza si ujinga washika dau,,, kama hivyo ndivyo misaada yote hiyo wanayotoa je ni return gani wanayopata kutoka kwetu,, siwezi amini kama mamilion ya dollar wanayagawa tu bure, au kwa kuwa dollar wanachapisha wao?
 
Kwa sababu hamna freedom of information act (FOI) kama wenzenu basi huwezi kupata
Labda wapitishe hiyo sheria ya kuwa yeyote anaweza kupata taarifa zozote za Umma mda wowote akihitaji
Hakuna anaetaka hii kwenye serikali zetu nyingi maana ni kuweka wizi wao hadharani
Sijasema huku kwetu mkuu..nasemea huko pesa inapotoka especially US kila kitu kipo wazi na kila cent inayoletwa uku kwetu kama msada inajulikana,ingia website ya USAID kila kit kipo wazi vingine story za vijiweni tu..
May b labda Kuna nyingne wanapeana Kwa siri Kwa makubaliano Yao wanayoyajua wao
 
Ukiwa na Mradi wowote ambao wao wanaona ni kwa Manufaa ya Taifa basi wanaweza wakakupa Mkopo wa Mradi huo (Hio ni theoretical) sasa practical you can argue huenda pesa zinapigwa; na vilevile you can argue kwamba hio miradi tunaweza kuifanya; And sio kweli kwamba USA hanufaiki na Miradi kama hii Indirectly ilikuwa ni good publicity na vilevile kuna mambo kama yanatoka kwao (producers) hivyo ni njia nyingine ya kujitafutia masoko ya excess au future customers...

Swali kubwa zaidi nilishauliza.... (Achana na hii Misaada) Je ?

 
Sijasema huku kwetu mkuu..nasemea huko pesa inapotoka especially US kila kitu kipo wazi na kila cent inayoletwa uku kwetu kama msada inajulikana,ingia website ya USAID kila kit kipo wazi vingine story za vijiweni tu..
May b labda Kuna nyingne wanapeana Kwa siri Kwa makubaliano Yao wanayoyajua wao
Nimekuelewa Mkuu
Ndio maana anasitisha misaada kwa sababu haiwafikii walengwa
Kuna ulaji mkubwa sana kwenye hizi taasisi na wapiga haswa
Watu wanauza mpaka maturubali ya Tents za UN na nembo kabisa zimeandikwa
Unakuta wanaanikia mahindi
 
Japo gharama za kupata ARV zipo juu Ila sifikirii Kama tutashindwa kulipia hizo dawa.

Je kwann mnamlaani trump?
Hizo dawa kwani zimeanza kuuzwa ....kama ni kwel8 basi hii itskuwa habari njema sana kwangu na kwa taifa na kwa africa
 
Did you know that USAID, using YOUR tax dollars, funded bioweapon research, including COVID-19, that killed millions of people? x.com

— Elon Musk (ElonMusk) February 2, 2025
 

Attachments

  • 20250206_232658.jpg
    20250206_232658.jpg
    286.1 KB · Views: 1
Back
Top Bottom