Sawa Mkuu.Hilo sio suluhisho la kikristo, Ukristo ueweka wazi muishi pamoja mpaka kifo..
Sio Tatizo langu, nataka tujuzane wakristo kwamba ndoa zetu hizi za kikristo zimekaa kimchongo sana, sheria hazijajitosheleza.Sawa Mkuu.
Dawa yako wewe kulogwa tu.
1 Timotheo 4:3Ukristo hauruhusu
Hata zile ndoa ambazo Mungu hajaziunganisha?bali mmefunga kwa tamaa zenu!Kitu cha kuvunja ndoa ni kifo na uzinzi nje ya ndoa, Ni vitu viwili tu!!
Maandiko yanaruhusu na hili wengi tunalijua.1 Timotheo 4:3
wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
1 Tim 4:3 SUV
1 Tim 4:3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli. | Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV) | Download The Bible App Now
wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.bible.com
Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.
1 Tim 3:2, 12 SUV
1 Tim 3:2-12 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu | Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitw
Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtubible.com
Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.
1 Tim 3:12 SUV
1 Tim 3:12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao. | Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV) | Download The Bible App Now
Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.bible.com
Kama unasoma Biblia, hayo ndiyo maandiko, wake wengi wameruhusiwa. Usisikilize maneno ya manabii wa uongo wanaokukataza usio mke mwingine
Hata sheria ya nchi inatambua ndoa za wake wengi zitazofungwa kwa imani ya dini ya kikristo. Mchawi wako ni kipengele ulichokata kwenye cheti cha ndoa, kama ulisema ndoa itakuwa ya mke mmoja ndio ujilaumu hapo. Biblia imesema ishi nao kwa akili, mnyooshe kisaikolojia na kifizikiaSio Tatizo langu, nataka tujuzane wakristo kwamba ndoa zetu hizi za kikristo zimekaa kimchongo sana, sheria hazijajitosheleza.
Hivi kweli uishi na mke anawatukana na kuwadharau ndugu na wazazi wako halafu mnasisitizwa muendelee kuishi pamoja,, kuna tofauti kati ya uvumilivu na upumbavu
Sasa kama mnalijua mnasita sita nini kufuata maandiko? Yaani unaacha kufuata biblia na unaanza kufuata katiba za kanisa?? Hivi ni vichekeshoMaandiko yanaruhusu na hili wengi tunalijua.
Ishu inapokuja ni kwmba, Je kuna kanisa lolote la kiksristo linayafata haya maandiko ??
Uwe unaongea kwa ushahidi tafadhali, Ni makanisa yapi hayo ??Sasa kama mnalijua mnasita sita nini kufuata maandiko? Yaani unaacha kufuata biblia na unaanza kufuata katiba za kanisa?? Hivi ni vichekesho
Kuhusu uwepo wa makanisa ya kikristo yanayotekeleza hilo, yapo. Moja lipo kihesa kilolo iringa na lingine lipo makabe mbezi, yana waumini wasiozidi 10
Tatizo ni kuwa unataka ligi na sio msaada. Anyways, kama upo tayari kujifunza ili unapoweka ligi kwingine uwe konki, nakufunzaNenda kasome upya sheria ya ndoa ya Tanzania..( Marriage act)
Ndoa za kikristo ni mke mmoja tu
Nilitegemea hili swali lingefuata, yaani unauliza swali huku tayari una jibu lako kichwani.Uwe unaongea kwa ushahidi tafadhali, Ni makanisa yapi hayo ??
Mkuu umechanganya kiingereza tuTatizo ni kuwa unataka ligi na sio msaada. Anyways, kama upo tayari kujifunza ili unapoweka ligi kwingine uwe konki, nakufunza
Ukisoma kifungu husika kwenye sheria ya ndoa kinasema kuwa
S. 10 (2) (b) in any other case, be presumed to be monogamous, unless the contrary is proved
Kwa tafsiri ya kuwa wakati wa kuoana, hata kama ilikuwa ni ndoa ya kikristo ila parties wakaamua kuwa itakuwa ya wake wengi, kwa kukata zile zisizohusika, basi ndoa itakuwa ya wake wengi na kutambulika kisheria.
Kaangalie hicho kifungu na ueleze wewe hiyo ya kuwa ukristo unataka mke mmoja imeandikwa wapi.
Kwenye a na b kote kuna neno PRESUMED, lakini kwenye tafsiri ya Kiswahili uliyoweka, hilo neno umelitumia kwenye (a) tu, kuwa 'ITACHUKULIWA' halafu kwenye (b) ukaamua kutoliweka hilo neno, na hilo ndio msingi wa TAFSIRI NZIMA, liweke halafu uone maana yake kama inabaki hiyo unayoamini.Mkuu umechanganya kiingereza tu
Tafsiri sahihi ya hapo ni kwamba,
Ndoa yoyote iliyofungwa Tanzania kabla au baada ya sheria ya ndoa kutungwa.
a. kama ni ya kiislamu au ya mila za Tanzania, itachukuliwa ni ndoa inayomruhusu mwanaume kuongeza mke
b.kwa ndoa za aina nyingine (ikiwemo ya ukristo), itakuwa ni ya mwanaume kutoruhusiwa kuongeza mke.
Kwa lugha nyepesi, hata serikali hairuhusu mwanaume kuwa na zaidi ya mke moja wenye ndoa ya kikristo
(2) A marriage contracted in Tanzania whether contracted before or after the commencement of this Act, shall–
(a) if contracted in Islamic form or according to rites recognised by customary law in Tanzania, be presumed, unless the contrary is proved, to be polygamous or potentially polygamous; and
(b) in any other case, be presumed to be monogamous, unless the contrary is proved.
Kifungu a kinahusisha ndoa za kiislamu na zile za mila za Tanzania, Sheria inapresume hizi ndoa mwanaume anaweza kuongeza mkeKwenye a na b kote kuna neno PRESUMED, lakini kwenye tafsiri ya Kiswahili uliyoweka, hilo neno umelitumia kwenye (a) tu, kuwa 'ITACHUKULIWA' halafu kwenye (b) ukaamua kutoliweka hilo neno, na hilo ndio msingi wa TAFSIRI NZIMA.
Ukristo ni zaidi ya kujulikana wewe unaamini nini, ukristo ni maisha. Ukristo unamfundisha mtu kuwa na mahusiano kibinafsi na Mungu, Kama mtu alikuwa anajifanyisha kuwa ana tabia nzuri kumbe sio, maana yake kabla ya kuingia kwenye ndoa inatakiwa Mungu awe amekuonesha hicho kitu.nataka tujuzane wakristo kwamba ndoa zetu hizi za kikristo zimekaa kinadharia sana kuliko kiuhalisia, sheria hazijajitosheleza na ndio maana watu hukimbilia mahakamani maana wanaona kabisa sheria za kikristo bado haziwezi kutatua hali zao.
Ukristo unaweza kutatua tatizo hili bila kutegemea sheria za mahakamani? Inatokea kwamba kwenye uchumba hata wa zaidi ya mwaka mzima mwanamke alikuwa na adabu ya hali ya juu, anawapenda ndugu zako, na tabia nyingine nzuri kumbe ni kujifanyisha tu ili umuoe.
Baada ya kunasa kwenye mtego wake mambo ya nabadilika.
~ Anaanza kuwa na kiburi.
~ Anaanza kuchukia na kuwatukana wazazi na ndugu zako.
~ Unakuja kupata stori huko kwao ni washirikina, ila kujificha huwa anaenda kanisani (wapo washirikina wengi sana wanatumia hii style)
Hapo mmeshakula kiapo kwamba mtaishi kwenye shida na raha mpaka kifo. Ngoma chambire moto!
Hii hali inatatuliwaje?
Maneno haya mengi hayatatui matatizo ya kwenye ndoa za kikristo,Ukristo ni zaidi ya kujulikana wewe unaamini nini, ukristo ni maisha. Ukristo unamfundisha mtu kuwa na mahusiano kibinafsi na Mungu, Kama mtu alikuwa anajifanyisha kuwa ana tabia nzuri kumbe sio, maana yake kabla ya kuingia kwenye ndoa inatakiwa Mungu awe amekuonesha hicho kitu.
Nakuhakikishia Mungu anaongea na watu katika dunia hii hii iliyojaa uovu, na hata ukiwa na mahusiano naye hata kidogo tu, kama ukimpa nafasi anaweza kuzuia usiingie kwenye huo mtego.
Shida ni kwamba wengi hawana mahusiano na Mungu lakini wakiingia kwenye matatizo ndo wanataka Mungu awajibike.
Ila ikitokea huyo mtu hakuwa amejifanyisha na kwamba Mungu kwa mapenzi yake kamili aliruhusu uingie na huyo mtu kwenye ndoa, basi hakika jua tu kwamba Mungu mwenyewe atalimaliza hilo muda si muda. Ni suala la kuwa mwombaji, kuwa mstahimilivu na kukaa karibu na uwepo wake kila wakati.
1Wakorintho 10:13 "Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili."