Ukikutana na Shabiki wa Mpira mwenye Kauli zifuatazo jua Hospitali ya Mirembe kunamuhusu

Ukikutana na Shabiki wa Mpira mwenye Kauli zifuatazo jua Hospitali ya Mirembe kunamuhusu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
1. Tunaenda kupindua meza kwao.

2. Mungu ni wa wote.

3. Wao wamewezaje na sisi tushindwe?

4. Mpira unadunda kokote pale.

5. Iwe jua iwe mvua.

6. Kikubwa ni kumuomba tu Mwenyezi Mungu.

7. Wamewezaje kupata alama kwetu na sisi tushindwe kuipata kwao?

GENTAMYCINE nasisitiza, ukibahatika tu kukutana na shabiki wa aina hii popote pale kwanza anza kumcheka, pili muonee huruma na Tatu mwambie awahi haraka sana tiba yake Hospitali ya Mirembe mkoani Dodoma.

Ambapo ili apone atapewa vidonge vizuri vya kumtibu akili na kupona kabisa viitwavyo ChamaPhiriMwenda ambavyo atatakiwa kumeza 3 X 1 (yaani vidonge vitatu kwa siku moja) tu.
 
Sawa ,ila mbona Ulaya yanatokea ?,Mwaka jana tuliona simba alichofanyiwa kwa mkapa
 
Na wakousoma huu uzi utawasababishia maradhi hayo ya akili kuwa mlipuko rasmi...
 
Namba 5.

wanaamini manara Ana 60% ya ushindi wakicheza mechi YOYOTE na 40% wachezaji wanaocheza.

Yaani wao bila manara kuongea kitu hawajacheza mpira.

Wanajua manara kafungiwa lakini wamemfuata akatoa hyo IWE MVUA IWE JUA.
 
Ni huzuni sana wazee wa timu nzuri yenye Aziz Ki ila hii wiki kwao imekua ndefu sana. Hawaamini macho yao jinsi ghafla mambo yamebadilika from kua wababe wa nchi to wanyonge wa nchi.
 
Yanga inashambuliwa walinzi wamebaki golini wawili au watu

wakicheza na Simba huwa wanakuwa wako idadi kubwa golini kwao kulinda compactly.

Wakasahau kuwa marasta wa Al Hilal sio akina Rasta Kibu Denga.
 
Back
Top Bottom