Problems are simply part of the curriculum that appear and fade away like algebra class but the lessons you learn will last a lifetime.
this got me thinking....
Ndio maana Mungu anatupa matatizo hapa na pale, masomo tunayojifunza baada ya hayo matatizo yanadumu maisha yetu yote...
mkuu naamini nia ya mleta mada ilikuwa hiyo
sasa huku Ally anakoelekea kunapelekea zaidi kuingia kwenye lile jukwaa la stress ambalo naamini pia sio lengo la mleta mada hapa
Mnakosea kabisa kudhani kuwa nataka niipeleke mada huko kwenye mastress. Maswali yote ambayo nimeuliza hapa ni halali na mleta mada hakuweka vikomo vya maswali ya kuulizwa. Au aliweka? Sasa sijui haya yote ya kusema mimi nataka sijui kuipeleka hii mada kwenye mastress yanatoka wapi?
Haya bana naona kuna maswali mengine kumbe ni kufuru hata kuuliza. Nawaachia mada yenu mfurahie bila mastress. Mimi nasepa zangu kule kwenye kutongozana na kina Lizzy na Ma Jerry.
<br />Upendo na amani na vitawale katika hii sredi. Na Husninyo popote pale ulipo, nakuhitaji huku PM.
Wapendwa marafiki salamu,
Jana nlimpigia simu rafiki yangu. Alipokea akiwa na simanzi kubwa. Kumbe ndio alikuwa kapokea habari ya msiba wa kaka yake. Alikuwa analia na kuongea kwa shida. Nilihuzunika kwa niaba yake..........kama si nguvu ya Tusker Malt labda nami ningemwaga chozi. Mnywaji mwenzangu akashangaa kwanini nimepata simanzi ya ghafla, nikamsimulia.
Huyu mtu akaniambia neno ambalo limenifanya nitafakari kwa kina usiku kucha......... Namnukuu: "Ndugu yangu, Mwache Mungu aitwe Mungu na aendelee kukaa hukohuko aliko maana ningepata nafasi ya kukutana naye sasa hivi ningemuuliza KWANINI ULIMCHUKUA BABA YANGU nikiwa bado mdogo nikataabika namna ile?"........ Nilichoka na mpaka sasa nimechoka.....Jamaa alivyonisimulia maisha yake, jinsi mama yake alivyohangaika.......Kweli kila mtu ana swali lake.....Dah!
Nami najiuliza.... Hivi ningepata nafasi ya kukutana na Mungu akanipa nafasi ya kumuuliza au kumwambia chochote ningemwambia na kumuuliza nini?.....
Kwanza ningeanza na shukrani:
Ahsante kwa kuniumba Mwanaume..... manake angeniumba mwanamke ningemuuliza kwanini ameniumba mwanamke.
Ahsante kwa kunipa mke mzuri (japo kwa ubinadamu wangu huwa natelezaga) na mabinti wawili wazuri.
Ahsante kwa kunipa wazazi wanaonipenda na kunijali sana
Ahsante kwa kunipa ndugu, marafiki, majirani tunaoheshimiana na kupendana sana.
Then lazima ningemuuliza;
Kwanini tatizo hili limetokea kwenye familia yetu?..... Kwanini kwetu?......... Ningemuuliza mbona kila siku tunakuomba kwenye maombi/sala utuondolee hili tatizo lakini huliondoi?........Lazima ningemuuliza...Niape?
Kuna mtu mwingine huku angekuwa na Swali kama angekutana na Mungu na kupewa nafasi ya kumuuliza?
Kama alivyonambia ndugu yangu, mwacheni Mungu aitwe Mungu......... Na aendelee kukaa huko aliko.
AMINA.
Leo ODM yuko kimajonzi zaidi.
Harudi kitandani wala nini. Anajiuliza tu.
Nitakufuata hukohuko uliko!<br />
<br />
nimesusa, sikupm wala siquote posts zako hadi sikukuu ipite.
Una bahati sana ndugu yangu, Mshike sana Mungu wako, usimwache kamwe!Mie nisingemwuliza kitu zaidi ya kumshukuru tu, yote nimwombayo anayatekeleza
Hahahahaha..... unafikiri atakuwa na muda mrefu hivyo? Mungu ana watu wengi sana!Nitaongea mpaka aseme baaasi
Swali:
Lini mafisadi wa Tz wataisha au
wataadabiswa na nchi iwe nzuri
wananchi wafaidi?
Nitashukuru:
kwa yote aliyonitendea mimi na familia yangu
ikiwa ni pamoja na kuniwezesha kuwa hivi nilivyo,
Nitaomba:
abariki uzao wangu wote
aniepushe na vishawishi vya kuiibia nchi yangu
anibariki niwe na utajiri wa kutisha
anizuie nisiingie ktk siasa
Ningekutana nae uso kwa uso ningemwambia .
Eeh mungu Nashukuru kwa matendo yako makuu Kwangu
Nashukuru kwa kunipa familia Njema na yenye upendo
Nashukuru kwa kunipa wazazi wenye hekina na busara za kutusikilia watoto wao
na kutuongoza katika maisha haya yaliyojaa tabu
Nashukuru kwa kunipa dada na wadogo zangu wenye upendo wa agape
Ningemuomba anipe mapito yaliyo mema siku zote
Ningemuomba anipe hekima kama za mfalme Suleiman ,
Pia ningemwambia nakushukuru kwa yote yaliyotokea katika maisha yangu
kwani najua ni moja ya mapito yangu
.
Nyie wasichana wawili hapo juuHii post nimeisoma na kunifanya nisikie imani na huruma....
BUT kusoma kwangu hii thread badala ya kusikitika nimecheka mno... Dah!
(i hope nimesamehewa...)... Saizi tupo very comfy.. for Kumtaja Mungu
in vain ilikua issue hapo kati...
On a serious note.
Nikipata nafasi ya kuonana na Mwenyezi Mungu na kupata nafasi ya kumuuliza
suali ama kumuambia lolote... Naamini nitakua Speechless na kuishia kumshukuru
kwa Neema zoote alizo nijalia, familia alonipatia, watu alonijalia, na Maisha niloishi....
Nyie wasichana wawili hapo juu
Mna bahati sana....
Mshikeni sana Mungu wenu
Msimuache kwa kuwa anawapenda sana.
Kuna wengine wanamwomba mpaka wanafikia hatua ya kukufuru kwa kuwa hawajibiwi maombi yao.
<br />
<br />
nimesusa, sikupm wala siquote posts zako hadi sikukuu ipite.
Oh.... avatar ilinidanganya, samahani mvulana.Babu nani kakwambia mie ni msichana ???shikamoo babu
Kweli mwacheni Mungu akae hukohuko mbinguni aliko, kumbe akijitokeza atakuwa na maswali mengi sana ya kuulizwa..... Pole sana rafiki, kwa kumpoteza mama yako mpendwa......mie naogopa kukufuru babu odm. kwa sababu,mh! ngoja tu nijifunze kuhesabu baraka zangu! mama yangu alipofariki miaka 7 iliyopita, dadangu alisema "muacheni Mungu aitwe Mungu. kama alisema Yesu ni mwanae mpendwa, tumsikilize, na akamuacha aangikwe msalabani!basi bana, imeshakua!''. tuliishia kumshukuru Mungu kwa muda aliompa mama kuwa nasi, na kutuandaa kuwa wanawake ambao tuko hivi leo! na kutupa ujuzi na mtazamo huu! wakati mwingine unaweza kujiuliza, why bother with God? lakini Mungu atusaidie.
Acha kuchakachua sredi, hii ni sredi ya Mungu.una hamu ya kukosa nguo mpya eeh? shauri yako!
babu; shkamoooo! naomba sh buku eeh..
Hasa mafisadi.Watu wanamwogopa Mungu, lakini hawaogopi kutenda dhambi....Hhahaha....
Ee Mungu wanasema kila kitu kitokeacho ni mipango yako, Kweli na huyu Rais ni mpango wako baba?
Au kama ni kisiasa zaidi utamuuliza kwanini umekubali Pinda adhalilike namna hii kwa Jairo kurudishwa kwenye ulaji?