Ukila na kipofu usimshike mkono!

Ukila na kipofu usimshike mkono!

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
Mhadhara - 46:
Upo msemo ambao unasema; "Ukila na kipofu usimshike mkono", lakini pia "Usimnyapie kuku kwenye majani makavu".

Kama umebahatika kujipenyeza kwenye ndoa ya mtu au mahusiano ya mtu kwasababu ya faida zako basi punguza mbwembwe, la sivyo utakatwa mapanga mchana kweupeee au utupiwe majini mabaya.

Ni mbaya kutembea na Mke/ Mume wa mtu, lakini ni mbaya zaidi kujitangaza kuwa una mahusiano na mke/ mume wa mtu, utakatwa mapanga mchana kweupeeee!

Mke/ Mume wa mtu ni kama nguo ya kuazima, muda wowote nguo itarudi kwa mwenye nayo, hivyo wakati wa kuivaa hupaswi kuwatambia watu mtaani.

VIDEO👇KWA MAFUNZO


Right Marker
Dar es salaam​
 
Back
Top Bottom