Ukimuondoa Zamalek Kombe la Shirikisho naomba, wanitajie timu ambayo ingeweza kuichalenge Yanga hii iliyotolewa Klabu Bingwa!

Kwa maana iyo robo klabu bingwa na fainali shirikisho timu zote azikuwa na ubora kwa misimu mitatu mtawalia? Nyie ndio Rage aliwachambua akawapima IQ zenu akatoka na jibu Moja tu!
We umeshatolewa mkuu huna chako fungasha virago vyako kengold anakusubiri kwanini unatusumbua sisi tunasubiri draw ya robo ipangwe?
 
Imekuuma sana eeh!....kaliwe huko
 
Ubora wa timu unajengwa na vitu vingi ikiwemo uongozi Bora,,kama viongozi wako walishindwa kusajili wachezaji Bora basi uwezi kuleta utetezi wa namna iyo hapa
Umelielewa swali?

Swali limeuliza ni kipi kigezo kinachofanya ionekane Club Bingwa ni mashindano magumu kuliko shirikisho.

Hapa tunataka kuipima sababu ya Yanga inayodaiwa wametolewa mashindanoni kwasababu aina ya michuano wanayocheza ni tofauti na shirikisho.

Huo utofauti ni upi?

Je ni ubora wa vilabu shiriki unaotokana na quality ya wachezaji?

Au ni jina tu la mashindano na sio factor nyingine yeyote ya ubora wa timu shiriki?
 
Ubora wa vilabu vilivyopo klabu bingwa ndio tofauti iliyopo hapo
 
mimi ni YOUNG africans, ila kwa hili hapana huu ni ukazaji wa fuvu tu,tumetolewa kizembe sana, yani hata goli moja kwa mkapa lilitushinda daah. naandika haya kwa machungu sana. jukwaa la michezo nimelikimbia sasa nimedili na jukwaa la habari na hoja mchanganyiko kule kuna mambo na topic nyingi za kuchangia. huku jukwaa tuwaachie MWAKAROBO
 
Mbona zipo mbinu nyingi tu za kupunguza maumivu nimeshangaa alivyokuja na porojo za kujifariji za kipuuzi kiasi hiki
Haya kwahiyo tukimwambia hakuna timu inayomzidi yeye ndio anakuwa kavuka robo fainali?
Mwambie p Didi Niko hapa
 
Ubora wa vilabu hapa unaupima kwa rank au kwa quality ya wachezaji?
Vyote vinategemeana, bila ubora wa wachezaji uwezi kupanda kwenye rank na ndio maana ata wewe umeishia robo robo zaidi ya mara 4 ukawa wa 7 kwenye rank kwa kuwa uliangushwa na quality ya wachezaji lakini yanga aliyejipata ndani ya misimu 3 akascore fainali na robo klabu bingwa na sasa kaingia kwenye 10 Bora!
 
Wewe kimbia na usirudi Tena uku yanga hainaga mashabiki dizaini yako kwamba timu ikipoteza sio yako ikishinda ndio mnajileta auna ata kadi ya uanachama,,nyie ndio mnatusumbua kazi kupiga tarumbeta nyingi auna ata mchango wowote kwenye klabu ovyo kabisa!
 
Unao ushahidi kuwa mimi si mwanachama wa YANGA? kwa taarifa yako mimi ni mwanachama wa yanga na ni miongoni mwa wafadhiri wakuu wa clab!ukitaka ushahidi njoo pm. kumbe watu humu mnaona tuko sawa eti?
 
Unaweza kumleta na sasa hivi anipasue? Kwani yanga hii inashika nafasi ya ngapi kwenye caf ranking mpaka sasa? Nijibu alafu utakuwa umejijibu kama yanga imepanda kiubora ama aijapanda!
wewe ni mwanayanga mwenzangu ila umeingia kingi leo,CAF ranking haiwezi kuainisha ubora wa team,ndo mana hata wanayanga wote wanajua simba yuko juu kwenye CAF RANKING kwa ubora aliokuwa nao miaka 5 iliyopita. hata sasa ikiletwa topic ya nani bora kati ya YANGA au simba wewe utaangalia current form ya klabu simba wataleta CAF RANKING
 
Hivi unaweza kuwa na timu mbovu ikapanda kwenye ranking? Unakijua tunachokizungumzia lakini? Unapandaje kwenye rank za caf kama auna ubora wowote? Nani kabishana juu ya Simba kuwa juu ya yanga kwenye rank? Ebu fatilia kwanza mtiririko wa namna tulivyokuwa tunaulizana utaelewa tulikuwa tunamaanisha nini,,ubora wa timu lazima uende sambamba na ranking,,kwanini yanga alikuwa nafasi ya 78? Kwa aina ya usajili aliokuwa anafanya angewezaje kupanda kwenye rank mpaka kufika kwenye kumi Bora Africa! Kikosi Bora ndio kimemfanya apande kwaiyo futa iyo kauli ya kusema eti ranking aiwezi kuainisha ubora wa timu,,kama ingekuwa ivyo basi na Majimaji ya songea ingekuwemo kwenye kumi Bora ya caf!
 
Unao ushahidi kuwa mimi si mwanachama wa YANGA? kwa taarifa yako mimi ni mwanachama wa yanga na ni miongoni mwa wafadhiri wakuu wa clab!ukitaka ushahidi njoo pm. kumbe watu humu mnaona tuko sawa eti?
Sasa mbona una kauli ambazo sio za kimpira? Mwanachama anayejielewa na anayeujua mpira awezi kutoa kauli za ivyo,,kauli hizo utolewa na wale mamluki ndio maana nimekutilia shaka, we unasema tumekosa ata goli kwani wale mamelodi timu Bora kabisa kwenye ukanda wa Africa tulipocheza nao pale kwao walipata goli ndani ya dk 90? Kwani awakutaka wapate goli muhimu? Walishindwa kupata kwakuwa mbinu za kiufundi za kocha wa yanga kipindi icho azikuruhusu apate ilo goli ni the same na mechi ya yanga na Mc alger walikuwa Bora kimbinu kwa aina yao ya uchezaji!
 
shida unatetea kitu ambacho haukijui,na ukielimishwa unajifanya mjuaji.
 
Yanga ni timu ya kijinga tu kimataifa, timu yeyote ile hata Namungo wangeweza kuifunga Yanga. Wakafie mbele huko na uchawi wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…