Ukiniona nipo kwenye ndoa na sijawahi kukupa kadi ya harusi kwa ajili ya mchango; usiniletee kadi yako ya mchango wa harusi

Ukiniona nipo kwenye ndoa na sijawahi kukupa kadi ya harusi kwa ajili ya mchango; usiniletee kadi yako ya mchango wa harusi

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kutokana na ugumu au vipaumbele vya maisha, watu wengi wanajitahidi kupunguza matumizi ya fedha yasiyokuwa ya lazima. Sasa wewe kipato chako hakitoshelezi kufanya sherehe ya harusi kubwa, huku ukitaka sherehe yako ianzie labda milioni 20, wakati wewe kianzio ulichonacho labda milioni 1; hizo zingine unategemea upate kwa watu, kwa njia ya kuchangisha, huo sio uungwana.

Kwa nini ujibebeshe mzigo usioweza, na matokeo yake ni kuwapa wachangiaji majukumu ambayo si ya lazima. Starehe upate wewe, kwa nini usumbue wengine?

Ukiniona nipo kwenye ndoa na sijawahi kukupa kadi ya harusi kwa ajili ya mchango; usiniletee kadi yako ya mchango wa harusi.
 
Huku kijijini kwangu tumeazimia kuchangia mifuko mitatu ya saruji pamoja na nondo pcs 20 kwa ajili ya ujenzi wa sanamu lako pale mjini Kagongwa.
🤣🤣🤣Nitumie hiyo hela ya sanamu nijijengee mimi mwenyewe huku kijijini
 
Halafu cha ajabu unakuta ndugu wanachangia harusi ya siku moja 20m halafu baada ya miaka miwili ndoa inavunjika! Ila kumchangia ndugu mmoja hiyo 20m akasome elimu ya chuo kwa miaka mitatu ambayo itakuja kumsaidia maishani nahi!
 
Halafu cha ajabu unakuta ndugu wanachangia harusi ya siku moja 20m halafu baada ya miaka miwili ndoa inavunjika! Ila kumchangia ndugu mmoja hiyo 20m akasome elimu ya chuo kwa miaka mitatu ambayo itakuja kumsaidia maishani nahi!
Ata ukiwa unaumwa unakaribia kufa,hawakuchangii matibabu
 
Back
Top Bottom