Ukiomba msaada humuoni mtu ila ukifa wanatoa michango ya maana!

Ukiomba msaada humuoni mtu ila ukifa wanatoa michango ya maana!

Ila msiba wako pesa wanayo
Hii ni kwa sababu binadamu wamekosa uaminifu. Watu wanatumia uongo kuomba misaada hata pale ambao hawana shida kubwa. Wewe unaweza ulikuwa na shida ya kweli lakini umekuwa victim kwa sababu ya uongo wa wengine. Mimi katika vitu vilivyonishangaza muda nilioishi hapa duniani ni binadamu kuotokuwa waaminifu kwenye mambo ya fedha. Kwa upande mwingine ukisikia kwenye kufa watu wanakuwa na uhakika ya kuwa ni shida ya kweli. BTW hili ni jambo zuri kwa sababu linafanya watu wajitume na kufanya kazi badala ya kuwa ombaomba. Kazi ni kipimo cha utu.
 
Yani mtu umemkopesha mfano 500k hajakulipa mwaka mzima, afu aje akuombe tena 100k utampa ?
ukiombwa mkopo 500k mpe ambayo hata akipotea nayo haitakuathiri labda 150k,akipotea jumla na usimuulize hatakaa aje kukuomba tena hela.
 
Kipindi chote wanatayarisha msiba ulikuwepo wapi na ulijuwaje kuhusu hiyo michango yote na matumizi bila ya wao kujua kama haujafariki.
Halafu kumbe ulikuwa mfanyakazi kwanini ulishindwa kuomba mkopo kazini!
 
_________________
Nyumba niliyo kuwa nikiishi ilifikia kipindi nilitaka kufukuzwa Ndani kwa kutokulipa kodi. Nikaamua kuwashirikisha marafiki hata na boss wangu pia, wote wakaanza kunikwepa. Nilivyoona hali hii nikaamua kushea na marafiki zangu Tatizo langu kwa kupost Facebook kutafuta msaada, lakini nilicho kipata ni likes 2 "na comment "0."
_
Nikaamua kutuma msg 250 kwa watu wangu wa karibu niliowasave kwenye simu, kuomba mkopo wa Tsh 600,000/=. Wakajibu watu 10 tu. Watu 6 kati ya hao waliniambia pole Sana, 10 walisema hawataweza kunisaidia. Mmoja aliamua kunisaidia kiasi kidogo sana na wengine 3 wakaniahidi, ila baadaye wakawa hawapokei hata simu zangu, mwisho nikafukuzwa kwenye nyumba.

Sikuwa na pakulala. Nikiwa nimechanganyikiwa natembea gizani mitaa ya Manzese, kibaka akanipora kibegi changu kidogo kilicho kuwa na vitambulisho vyangu, vyeti na simu. Akapotelea kwenye vichochoro sikumuona alipoishia. Kumbe huko alipokimbila alijaribu kuvuka barabara, akagongwa na kufa hapohapo.

Wapita njia wakaokota kibegi changu na kukuta vitambulisho na vyeti. Kale kasimu wajanja wakapita nako. Vyombo vya habari vikaripoti nimekufa, na ndugu zangu wakajulishwa kwenda kuchukua vitambulisho na vyeti vyangu.

Watu 300 wakaandika kwenye akaunti yangu ya Facebook jinsi walivyo nifahamu na jinsi nilivyokuwa mtu mzuri sana na mstaarabu. Kamati ya mazishi ikaundwa na rafiki zangu wakachanga Tsh 1,500,000 zakuweza kulisha watu kwenye msiba.

Wafanyakazi wenzangu wakachanga pesa za jeneza, viti na maturubai. Walipanga nizikwe kwenye Jeneza la Heshima la Tsh 3,000,000/=. Walipokwenda kununua, muuza Jeneza akawauzia kwa Tsh 2,800,000/=. Akatoa discount ya laki mbili kama mchango wake kwenye msiba wangu, kwa kuwa alikua rafiki yangu Facebook.

Familia wakakaa kupanga mazishi. Kikao cha kwanza tu wakachanga Tsh 3,000,000/=. Ndugu zangu kila mmoja alitaka kujionyesha kuwa yeye ni mchangiaji mzuri. Wakashindana kutoa mamilioni. Waka print T-shirts kwa Tsh 2,000,000/=.

Fikiria sasa picha iliyotokea nilipoamua kujitokeza siku ya mazishi yangu.

FUNZO:

Hivi ndivyo DUNIA ilivyo kwa sasa. Ni ukweli wa kusikitisha lakini ni moja ya maisha tunayoishi sasa hivi katika Jamii zetu kila siku. Wewe unaye soma hadithi hii badilika sasa na badili tabia yako.

Msaidie rafiki au ndugu yako wakati wa matatizo yake. Usisubirie kifo chake ndipo ukaonyeshe kujali. Haitasaidia kitu.

Mahatma Ghandi aliwahi kusema "The pain of caring is far less than the pain of regret" akimaanisha gharama za kuwajali wengine ni ndogo kuliko gharama za majuto kwa kushindwa kuwajali.

Yani kama mtu anahitaji dawa ya shilingi 5,000/= ili apone, na wewe unaweza kumsaidia lakini ukaacha kwa kuogopa gharama, utapata gharama kubwa zaidi za majuto ikiwa mtu huyo atakufa.!
Kwa hiyo walianza michango na matayarisho ya kukufukia bila kuuona na kuthibitisha mwili wako?Marehemu acha fiksi basi!
 
_________________
Nyumba niliyo kuwa nikiishi ilifikia kipindi nilitaka kufukuzwa Ndani kwa kutokulipa kodi. Nikaamua kuwashirikisha marafiki hata na boss wangu pia, wote wakaanza kunikwepa. Nilivyoona hali hii nikaamua kushea na marafiki zangu Tatizo langu kwa kupost Facebook kutafuta msaada, lakini nilicho kipata ni likes 2 "na comment "0."
_
Nikaamua kutuma msg 250 kwa watu wangu wa karibu niliowasave kwenye simu, kuomba mkopo wa Tsh 600,000/=. Wakajibu watu 10 tu. Watu 6 kati ya hao waliniambia pole Sana, 10 walisema hawataweza kunisaidia. Mmoja aliamua kunisaidia kiasi kidogo sana na wengine 3 wakaniahidi, ila baadaye wakawa hawapokei hata simu zangu, mwisho nikafukuzwa kwenye nyumba.

Sikuwa na pakulala. Nikiwa nimechanganyikiwa natembea gizani mitaa ya Manzese, kibaka akanipora kibegi changu kidogo kilicho kuwa na vitambulisho vyangu, vyeti na simu. Akapotelea kwenye vichochoro sikumuona alipoishia. Kumbe huko alipokimbila alijaribu kuvuka barabara, akagongwa na kufa hapohapo.

Wapita njia wakaokota kibegi changu na kukuta vitambulisho na vyeti. Kale kasimu wajanja wakapita nako. Vyombo vya habari vikaripoti nimekufa, na ndugu zangu wakajulishwa kwenda kuchukua vitambulisho na vyeti vyangu.

Watu 300 wakaandika kwenye akaunti yangu ya Facebook jinsi walivyo nifahamu na jinsi nilivyokuwa mtu mzuri sana na mstaarabu. Kamati ya mazishi ikaundwa na rafiki zangu wakachanga Tsh 1,500,000 zakuweza kulisha watu kwenye msiba.

Wafanyakazi wenzangu wakachanga pesa za jeneza, viti na maturubai. Walipanga nizikwe kwenye Jeneza la Heshima la Tsh 3,000,000/=. Walipokwenda kununua, muuza Jeneza akawauzia kwa Tsh 2,800,000/=. Akatoa discount ya laki mbili kama mchango wake kwenye msiba wangu, kwa kuwa alikua rafiki yangu Facebook.

Familia wakakaa kupanga mazishi. Kikao cha kwanza tu wakachanga Tsh 3,000,000/=. Ndugu zangu kila mmoja alitaka kujionyesha kuwa yeye ni mchangiaji mzuri. Wakashindana kutoa mamilioni. Waka print T-shirts kwa Tsh 2,000,000/=.

Fikiria sasa picha iliyotokea nilipoamua kujitokeza siku ya mazishi yangu.

FUNZO:

Hivi ndivyo DUNIA ilivyo kwa sasa. Ni ukweli wa kusikitisha lakini ni moja ya maisha tunayoishi sasa hivi katika Jamii zetu kila siku. Wewe unaye soma hadithi hii badilika sasa na badili tabia yako.

Msaidie rafiki au ndugu yako wakati wa matatizo yake. Usisubirie kifo chake ndipo ukaonyeshe kujali. Haitasaidia kitu.

Mahatma Ghandi aliwahi kusema "The pain of caring is far less than the pain of regret" akimaanisha gharama za kuwajali wengine ni ndogo kuliko gharama za majuto kwa kushindwa kuwajali.

Yani kama mtu anahitaji dawa ya shilingi 5,000/= ili apone, na wewe unaweza kumsaidia lakini ukaacha kwa kuogopa gharama, utapata gharama kubwa zaidi za majuto ikiwa mtu huyo atakufa.!
Kama uliwahi kushuhudia hilo ilikuwa upambane
 
Hata mimi nimeomba msaada kwa watu 3 wapo kimya ila siku nikifa watatoa mahela kibao.Daaah
 
_________________
Nyumba niliyo kuwa nikiishi ilifikia kipindi nilitaka kufukuzwa Ndani kwa kutokulipa kodi. Nikaamua kuwashirikisha marafiki hata na boss wangu pia, wote wakaanza kunikwepa. Nilivyoona hali hii nikaamua kushea na marafiki zangu Tatizo langu kwa kupost Facebook kutafuta msaada, lakini nilicho kipata ni likes 2 "na comment "0."
_
Nikaamua kutuma msg 250 kwa watu wangu wa karibu niliowasave kwenye simu, kuomba mkopo wa Tsh 600,000/=. Wakajibu watu 10 tu. Watu 6 kati ya hao waliniambia pole Sana, 10 walisema hawataweza kunisaidia. Mmoja aliamua kunisaidia kiasi kidogo sana na wengine 3 wakaniahidi, ila baadaye wakawa hawapokei hata simu zangu, mwisho nikafukuzwa kwenye nyumba.

Sikuwa na pakulala. Nikiwa nimechanganyikiwa natembea gizani mitaa ya Manzese, kibaka akanipora kibegi changu kidogo kilicho kuwa na vitambulisho vyangu, vyeti na simu. Akapotelea kwenye vichochoro sikumuona alipoishia. Kumbe huko alipokimbila alijaribu kuvuka barabara, akagongwa na kufa hapohapo.

Wapita njia wakaokota kibegi changu na kukuta vitambulisho na vyeti. Kale kasimu wajanja wakapita nako. Vyombo vya habari vikaripoti nimekufa, na ndugu zangu wakajulishwa kwenda kuchukua vitambulisho na vyeti vyangu.

Watu 300 wakaandika kwenye akaunti yangu ya Facebook jinsi walivyo nifahamu na jinsi nilivyokuwa mtu mzuri sana na mstaarabu. Kamati ya mazishi ikaundwa na rafiki zangu wakachanga Tsh 1,500,000 zakuweza kulisha watu kwenye msiba.

Wafanyakazi wenzangu wakachanga pesa za jeneza, viti na maturubai. Walipanga nizikwe kwenye Jeneza la Heshima la Tsh 3,000,000/=. Walipokwenda kununua, muuza Jeneza akawauzia kwa Tsh 2,800,000/=. Akatoa discount ya laki mbili kama mchango wake kwenye msiba wangu, kwa kuwa alikua rafiki yangu Facebook.

Familia wakakaa kupanga mazishi. Kikao cha kwanza tu wakachanga Tsh 3,000,000/=. Ndugu zangu kila mmoja alitaka kujionyesha kuwa yeye ni mchangiaji mzuri. Wakashindana kutoa mamilioni. Waka print T-shirts kwa Tsh 2,000,000/=.

Fikiria sasa picha iliyotokea nilipoamua kujitokeza siku ya mazishi yangu.

FUNZO:

Hivi ndivyo DUNIA ilivyo kwa sasa. Ni ukweli wa kusikitisha lakini ni moja ya maisha tunayoishi sasa hivi katika Jamii zetu kila siku. Wewe unaye soma hadithi hii badilika sasa na badili tabia yako.

Msaidie rafiki au ndugu yako wakati wa matatizo yake. Usisubirie kifo chake ndipo ukaonyeshe kujali. Haitasaidia kitu.

Mahatma Ghandi aliwahi kusema "The pain of caring is far less than the pain of regret" akimaanisha gharama za kuwajali wengine ni ndogo kuliko gharama za majuto kwa kushindwa kuwajali.

Yani kama mtu anahitaji dawa ya shilingi 5,000/= ili apone, na wewe unaweza kumsaidia lakini ukaacha kwa kuogopa gharama, utapata gharama kubwa zaidi za majuto ikiwa mtu huyo atakufa.!
Mimi nimekuchangia kwa uwezo wangu kisha wewe unasimama hadharani na kusema "eti nimekuchangia kidogo sana"! Hauna shukurani wewe.
 
Back
Top Bottom