Ukiomba "NIDA ONLINE" kisha uende kwenye ofisi zao wanakurudisha eti ukajaze fomu ya mkono

Ukiomba "NIDA ONLINE" kisha uende kwenye ofisi zao wanakurudisha eti ukajaze fomu ya mkono

Trainee

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2018
Posts
2,660
Reaction score
3,501
Sijui ni kweli au ni wasiwasi wao tu au nini labda... Jamaa watu wakienda na fomu za mtandaoni wanawarudisha huku wakiwaambia eti fomu hizo zinasumbua sana ni bora wakajaze fomu za mkono kwa watendaji

Kama ni hivyo naona kama hii huduma (online) haina maana yoyote ni bora ikaondolewa au ikarekebishwa hapo penye kuleta usumbufu. Na kama hakuna tatizo lolote kwenye huduma ila ni wasiwasi tu wa maafisa wa NIDA basi mola anawaona jinsi wanavyosumbua watu.

Hebu NIDA watupe ufafanuzi zaidi juu ya hili

Soma Pia: Waziri Masauni: NIDA kuna shida ya usimamizi, Uongozi una shida, Watu wanateseka kupata Vitambulisho
 
Nadhani inategemea na mfumo umekaaje, lkn Mimi binafsi niliomba online, nikaprint zile fomu zikapigwa mihuri stahiki na sikurudishwa.
 
Nadhani inategemea na mfumo umekaaje, lkn Mimi binafsi niliomba online, nikaprint zile fomu zikapigwa mihuri stahiki na sikurudishwa.
Ilikuwa ni bahati yako ndugu au basi inategemea na ofisi, ujue tunasukumwa sana kwenda kidijitali lakini ofisi nyingi za serikali kumejaa watu wasioweza hiyo dijitali na wala hawaitaki
 
Online service inapigwa vita na watumishi wa Serikali ili pesa inayopaswa kwenda kwenye mfuko wa Serikali iwanufaishe wao.
Ni ugumu unaotengenezwa makusudi na wahudumu vilaza wa mambo ya IT.
 
Hii nchi ni ya ajabu sana. Mfano pale Airport, mizigo inapita vizuri tu kwenye mashine lakini wakiona umelifunga begi na nailoni unaona TRA hao wanakuambia fungua begi. Huu ujinga uko bongo tu na sehemu nyingine za Africa
Wanakuambia ulipie kodi zawadi ulizonunua. Juzi nimewawakia nikawaambia waache kudhalilisha wateja. Wamekaa kirushwa rushwa tu.
 
Online service inapigwa vita na watumishi wa Serikali ili pesa inayopaswa kwenda kwenye mfuko wa Serikali iwanufaishe wao.
Ni ugumu unaotengenezwa makusudi na wahudumu vilaza wa mambo ya IT.
Nida NI bure nadhani wanataka paper work ajira zao zisipo tee wanarudia Tena kujaza digital....Sasa ikiwa NI online hata wahamiaji haramu wanaweza kupata kirahisialafu kazibtya online anaweza kufanya MTU mmmoja kwa mania ya watu
 
Back
Top Bottom