Ukiona dalili hizi kwa Mgonjwa wako aliyeko Kitandani jua muda wowote ' Israeli ' anafanya yake!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mgonjwa yoyote aliyeko Kitandani kabla ya Kufa husema sana na mara kwa mara haya maneno yafuatayo hivyo kama ukiyasikia jua kuwa maandalizi ya Msiba yanatakiwa yawe ya haraka sana na taratibu zingine za maziko....
  1. Regret ( anakuwa Mtu wa kujutajuta kila mara )
  2. Unfinished Business ( anakuwa anaumia sana kutotimiza malengo )
  3. Missing Someone ( kuna Mtu mmoja atakuwa anamkumbuka mara kwa mara )
  4. Tired ( anakuwa Mtu wa Kuchoka choka muda mrefu )
  5. Hallucinating ( kuna muda anakuwa kama amewehuka / amedata )
  6. Happiness ( anatawaliwa na furaha isiyo na ratiba )
Source: THE DAILYNET.COM

Nawasilisha.
 
ipo hiyo moja yaukweli na uhakika Mara nyingi anakua hawezi kuangalia vizuri kuinua uso anakua ameinamisha kichwa chini macho mazito. Israel anahesabu masaa
 
Wengine unakuta muda mwingi hataki kuwaangalia usoni bali ana angalia ukuta tu.

Huyo anayependa sana kuangalia Ukuta lazima tu atakuwa na Kadi ama ya CHADEMA au CUF au TLP au NCCR-Mageuzi ambao ndiyo ' wamiliki ' Wakuu wa Umoja ' mfu ' wa UKAWA ambao kuna mwaka walikuja na ' Campaign ' yao ya UKUTA.
 
Nikweli kabisa ..nashangaaga sana,kwann siku yakufa mgonjwa anakua na furaha furaha tuuuuu
 
Hahahaah ukipata Mtaalam akazielezea vizuri uta-enjoy Sana!! Nadhani niliwahi kuandika thread yenye hizo five stages kwa kuitaja CCM back then.

Kuna stage mbili au tatu za wazi, kwanza ni Denial, akakataa kwamba haiwezekani kufa, ana mambo ya kufanya, Sio yeye, n.k na Hii sometimes hupelekea hio hallucination

Kisha stage nyingine ambayo ni Nzuri ni Ile ya Acceptance, sasa anakubali kuwa anaumwa, anaikubali Hali yake, kisha stage nyingine ya wazi kabisa ni Ile ya Repentance and Negotiation au Msamaha

Ukishaona au ukisikia, naomba mniitie Mchungaji, au kitubio au sijui naomba Nisamehe saaana au Kule nyumbani chini ya kabati kuna hati za nyumba, Fulani ananidai! Hahahahaha
 
Kifo kimebeba fumbo kubwa snaa kwenye maisha ya mwanadamu.....

Hakuna uhusiano wowote wa kifo na kuugua

Kila mja atakufa kwa wakati wake na kwa style yake.....

No body knows
 
Kifo kimebeba fumbo kubwa snaa kwenye maisha ya mwanadamu.....

Hakuna uhusiano wowote wa kifo na kuugua

Kila mja atakufa kwa wakati wake na kwa style yake.....

No body knows

Na hata ' Uzi ' wangu unawazungumzia sana Wagonjwa na siyo huo ' Upuuzi ' wako uliojitahidi Kuuelezea hapa. Siku nyingine uwe unasoma Kwanza ' thread ' kwa uangalifu na umakini wako mkubwa ili basi ukiwa unajibu tusione tofauti yoyote ya aina ya IQ uliyonayo.
 
Sawa ndugu....

Samahani kama umekwazika na mtazamo wangu!!!!

Uwe na wakati mwema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…