Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Hivi sasa wataalamu wamegundua kwamba wanawake walio kwenye kusongeka kiakili hula sana kuliko wanaume. Katika kula huko, hujikuta wakinenepa kupindukia.
Mwanasaikolojia Robert Jeffery anasema, mwanaume akiwa kwenye msongo hakimbilii kula kama ilivyo kwa mwanamke. Wanawake wengi wakiwa na mawazo mengi yenye kuwasonga hujitafutia nafuu kwa kula sana. Wanawake ambao wamesongeka hushindwa kujizuia kula kila wakati hasa pale wanapoingia kwenye kuwaza sana au hata wanapoona chakula kwenye televisheni au wanapoona chakula ambacho wanaweza kukipata.
Inaelezwa kwamba matatizo ya ndoa au mahusiano ya kimapenzi huwafanya wanawake wengi kuwaza kupita kiasi na kupelekea kupata msongo wa mawazo. Ingawa kazi hususan kwa walioajiriwa inatajwa kama chanzo kizuri kinachowasababishia wanawake msongo wa mawazo lakini matatizo ya ndoa au mahusiano ya kimapenzi hutajwa sana kama chanzo kizuri kinachowasababishia msongo wa mawazo. Tatizo linakuja kwamba wanaponenepa na kujichukia kwa unene wao huongeza kiwango chao cha sononi na hivyo, hula zaidi.
Siyo kwamba hakuna wanaume wanaokula sana kwa sababu ya kusongeka, wapo. Lakini wanawake wenye tatizo hilo ni wengi mara mbili zaidi kuliko wanaume. Kwa hiyo ukikutana na mwanamke ambaye ni mnene kutokana na kula unapaswa kujua kwamba, huyo amesongeka kiakili. Kwa wale wanawake wanene, ambao wanakula sana na wanashindwa kabisa kujizuia kula sana, inabidi wajue kwamba, labda wamesongeka. Ili kujitoa kwenye mashaka hayo, inabidi wapate tiba ya kusongeka ambayo ni pamoja na ushauri na dawa.
Sikuandiki utafiti huu ili kuwakera wanawake wanene, hapana. Lengo ni kuwasaidia kujua kinachowakabili ili waweze kujisaidia. Unene wa ziada ni hatari kwa maisha ya mhusika, bila kujali kama unene huo unakupendeza au unasifiwa kwamba, una fedha, jua tu kwamba, ni hatari tena hatari sana.