Ukipata scholarship unalipiwa nini?

Conq'ueror

Senior Member
Joined
May 13, 2015
Posts
171
Reaction score
131
Mwenye uelewa tafadhari,ukipata scholarship kusoma nchi fulani mfano degree ya kwanza unalipiwa nini na kujilipia nini?
 
Scholarships huwa zinatofautiana sana. hakuna jibu moja ambalo linaweza kuwa jibu. Ila zipo ambazo unapewa ful yaan ada, usafairi wa kutoka nchi yako wakati wa kwenda na kurudi (unapomaliza chuo), pesa ya kujikimu, pesa ya vitabu na utafiti. Hiyo utakua huna haja ya kutafuta pesa ila kwa matakwa yako binafsi ya kujiongezea kipato. Ila kuna nyingine unalipiwa ada ila pesa ya kujikimu unatafuta mwenyewe, unalipiwa usafiri wa kuja na kuondoka. Kwa kweli zipo tofauti sana kila scholarships, ni vizuri kuisoma vyema ili ujue wanakupa nini na nini unatakiwa kuchangia.
 
Inagemea na scholarship yenyewe. Inaweza kuwa full scholarship ambayo utalipiwa kila kitu, ama partial scholarship ambayo watakulipia baadhi ya gharama mf. ada, chakula na malazi, nauli, gharama za usajili, utafuti n.k. Kwa ufupi hakuna utaratibu maalum, usome scholarship yako na uielewe vizuri.
 
walipokupa hawakukwambia wanacover mambo gani?? maana huwa wanaweka wazi wanalipa nini, kabla ya kukupa nafasi ya kuiomba, na kabla ya kuomba pia kuna criterias hua wanaziweka, ukiqualify unapewa, waulize watalipa vitu gani maana wao wapo kwenye nafasi nzuri zaidi kukujibu badala ya kutuuliza sisi
 

Ngoja niwatafti vzuri wafunguke,nakushukuru
 
Naomba kuuliza wadau tuseme labda umepata full scholarship kile kiasi unachopewa utakuja ulipie baada kuwa umepata kazi (kama vile wanavyo fanya bodi ya mikopo) au yenyewe haina kurudisha ?
 
pia jaribu kuwa makini/kufwatilia..matapeli wamekuwa wengi siku hizi
 
pia jaribu kuwa makini/kufwatilia..matapeli wamekuwa wengi siku hizi

Kama ulikuwepo vile,ndiyo maana naweka mikakati niwe na ufahamu wa kutosha nitakapokutana nao ana kwa ana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…