..hapa nani anakuwa mpigaji mana hii inakuwa kama simu ya kifo..Je ni Shetani au malaika mtoa roho?? au mitambo ya simu!?:confused2:Nimepokea message hii toka kwa washikaji zangu mbalimbali
"Ukipigiwa simu kwa private no. au akaandika call kwa red colour usiipokee ni mionzi unaparalise na kufa. Imetokea kenya watu wamekufa. julisha ndugu & jamaa wote."
Kaelimu kangu ka science kananifanya isiniingie kichwani, hebu mabingwa mmeshapokea sms za aina hii?
Dah! Jamaa anaonekana yuko serius kweli!.hakuna lolote.
kisayansi mionzi ya kukuangamiza, hadi ikufikie wewe , ujue Tayari handset imeparanganyika, maana hakuna hANDSET INAYOWEZA KUKABILIANA NA KISHINDO cha mionzi inayoweza kumuangamiza binadamu.
huu ni uvumi, ni umbeya, mtu kakaa kichwani mwake kaamua kuenea ujinga.
hatudanganyiki, acha nirejee jukwaa la siasa, nikajadiri mbinu za kuing'oa ccm na Mafisadi.
we we! Usimtaje huyo khabari yake nzito, shauri yako.Hakuna kitu hapo.isije ikawa ccm wanataka kuzuia watu kuwasiliana.walishasajili namba na mmeshaona voda wanavyohujumu upinzani.hatudanganyiki.au mmeshasahau uzushi wa mtoto mla watu muhimbili,popo bawa na mtu wa manyoya pale ubungo.hizi ni abrakadabra anazosema mjengwa