Ukisema Jini tayari kuna majini miatatu karibu yako. Kila mtoto mchanga huguswa na jini dakika moja bada ya kuzaliwa. Vitabu vya dini vinasemaje?

Uzuri ni kwamba bible inasomwa kwa dot's ila ukisoma litricture ndio unaibuka na quote moja ya kumaliza hitaji lako

Nimesoma na bado nasoma na nitaendelea kusoma Quran na Bible kwa wakati mmoja hivyo Chief najua nilichokiandika kuliko udhaniavyo

Ahsante kwa maarifa yako pia
 
Kwahiyo ni malaika waliyoasi na kwamba wana idadi yao kamili au ni kwamba hadi sasa malaika wengine huwa wanaasi?

Na kwanini hatuwaiti malaika tu kama ambavyo binaadamu hata hata akiasi bado huwa ni binaadamu tu?
 
Kwahiyo sifa ya kutokufa si ya Mungu tu pekee?
 
Kwahiyo sifa ya kutokufa si ya Mungu tu pekee?
Kwa mujibu wa biblia hata sisi wanadamu hatukutakiwa kufa ila kifo kilikuja baada ya uasi wa wazee wetu Adamu na Hawa.
Pia baada ya kufufuliwa kwa ajili ya hukumu ya mwisho hakutakuwa na kifo tena.
 
Kwa mujibu wa biblia hata sisi wanadamu hatukutakiwa kufa ila kifo kilikuja baada ya uasi wa wazee wetu Adamu na Hawa.
Pia baada ya kufufuliwa kwa ajili ya hukumu ya mwisho hakutakuwa na kifo tena.
Ndio mkuu kifo ilikua penalty baada ya ancestor wetu kuanguka dhambini. Ila Mungu anatupenda akatupa neema ya uzima wa milele.
 
Kwahiyo ni malaika waliyoasi na kwamba wana idadi yao kamili au ni kwamba hadi sasa malaika wengine huwa wanaasi?

Na kwanini hatuwaiti malaika tu kama ambavyo binaadamu hata hata akiasi bado huwa ni binaadamu tu?
Umeuliza swali la msingi sana
 
Kwahiyo sifa ya kutokufa si ya Mungu tu pekee?
Ndio mkuu maana vyote vilivyo na roho pekee havifi ikiwemo malaika na Mungu mwenyewe.

Na hata binadamu wanapokufa mwili hili jumba wanabakia rohoni for thousands of years to come alive and immortal.

Kiumbe chochote kinachoishi rohoni ni immortal and eternal. So yes majini kwa vile na wao ni roho then wanaqualify kutokufa then mtu anaposema wanakufa it doesn't make sense at all.. they are energy.

Hata sisi binadamu hatufi... Its fictional.. Its an elusion of the mind... Tunahama tu kutoka mwilini hadi rohoni. That's it!
 
Kwa mujibu wa biblia hata sisi wanadamu hatukutakiwa kufa ila kifo kilikuja baada ya uasi wa wazee wetu Adamu na Hawa.
Pia baada ya kufufuliwa kwa ajili ya hukumu ya mwisho hakutakuwa na kifo tena.
Ukizungumzia masuala ya baada ya hukumu teyari kifo kilishatokea,sasa hoja ya kwamba kuna viumbe ambao hawafi na hivyo hata hiyo Siku ya hukumu itawakuta wakiwa hawajawahi kupatwa na umauti maana wana sifa ya kutokufa.
 
Kwahiyo ni malaika waliyoasi na kwamba wana idadi yao kamili au ni kwamba hadi sasa malaika wengine huwa wanaasi?
Mkuu kulikuwa na maasi ya aina mbili, uasi wa kwanza ni ule alioufanya "Malaika Lusiferi" na kuwashawishi "malaika wenzake" wengine pia wakaasi. Kisha baada ya huo uasi wa kwanza ukatokea tena uasi mwingine, huu ni ule wa wale malaika waliokuja duniani na kuoa mabinti na kuzaa nao.

Kundi hili la malaika waliozaa na wanadamu, baada ya gharika walikamatwa na kufungwa kwenye vilindi vya giza(YUDA 1:6) lakini Lusiferi na kundi lake wao hawakukamatwa mpaka ile siku atakapokuja YESU kwa mara ya pili(UFUNUO 20:1-3).

Baada ya maasi haya kufanyika, hakuna tena uasi utakaofanyika Mbinguni, Malaika wote waliobakia ni Watiifu kwa BWANA MUNGU.
Na kwanini hatuwaiti malaika tu kama ambavyo binaadamu hata hata akiasi bado huwa ni binaadamu tu?
Mkuu ni jina tu, fahamu kwamba wote hawa wanaitwa "wana wa MUNGU"(MWANZO 6:1-2). Unaweza ukawaita "malaika waasi", lakini baada ya kuasi walipewa jina la ujumla ambalo ni "Mashetani" maana yake ni "Maadui". Jina "Shetani" siyo jina lao la asili, wao ni malaika isipokuwa tu wao ni "waasi".

Ni kama vile kikundi cha "uasi" kikitokea katika nchi, utaona jinsi watu wanavyokipa majina ya ajabu ajabu ingawa waasi ni wananchi tu wakawaida.
 
Kwahiyo ni malaika waliyoasi na kwamba wana idadi yao kamili au ni kwamba hadi sasa malaika wengine huwa wanaasi?

Na kwanini hatuwaiti malaika tu kama ambavyo binaadamu hata hata akiasi bado huwa ni binaadamu tu?
Kwa uelewa wangu majini malaika vibwengo nk. Wanatofautiana lakini wote wanamtumikia Lucifer. Ukisoma biblia unaona imeandikwa shetani na jeshi lake kwaiyo ni collection ya viumbe.
 
Ukizungumzia masuala ya baada ya hukumu teyari kifo kilishatokea,sasa hoja ya kwamba kuna viumbe ambao hawafi na hivyo hata hiyo Siku ya hukumu itawakuta wakiwa hawajawahi kupatwa na umauti maana wana sifa ya kutokufa.
Ndivyo ilivyo mkuu kifo na hukumu vinatuhusu sisi wanadamu na shetani na jeshi lake.
Mfano malaika watiifu kama Michael, Gabriel na Rafael Mungu hana sababu ya kuwauwa. Kwa mujibu wa biblia kifo ni adhabu/laana na watakao kufa na kufufuliwa na wakaonekana walijitahidi kumtii Mungu hawatakufa tena.
Hata Yesu kilichomfanya akutane na kifo ni ile yeye kukubali kutumwa na Mungu kutoka mbinguni aje duniani auvae mwili wa kibinaadamu na kuifanya kazi aliyoagizwa kuifanya, otherwise kifo kilikuwa hakumhusu.
 
Kwa hivyo majini(malaika waliyoasi) wana idadi kamili hawaongezeki maana hakutokei tena uasi.

Na kuhusu kuitwa shetani hivyo hata binaadamu nao pia wanaweza kuitwa shetani?kwa jinsi ulivyo elezea hilo neno shetani.
 
Kwa uelewa wangu majini malaika vibwengo nk. Wanatofautiana lakini wote wanamtumikia Lucifer. Ukisoma biblia unaona imeandikwa shetani na jeshi lake kwaiyo ni collection ya viumbe.
Wanatofautiana vp mkuu wakati wote ni malaika tu? hayo ya mapepo au vimbwengo yanakujaje?
 
Hapo sasa sijaelewa,wewe unasema kifo kinatupata kwa sababu in adhabu na wengine wanasema kifo kinatupata kwa sababu ya kuwa na hii miili,kwa maana hivyo wasio na maumbo ambao ni roho hawafi.
 
Kwa hivyo majini(malaika waliyoasi) wana idadi kamili hawaongezeki maana hakutokei tena uasi.
Hawawezi kuongezeka maana wao hawana mfumo wa "uzazi" kama viumbe wengine, malaika hawazaliani kama binadamu. Ukisikia watu wanasema majini wanazaliana huo ni uongo mtupu, ni hadithi tu za "alinacha", mambo ya kufikirika, maana majini ndio hao hao malaika waasi na hawana uwezo wa kuzaliana wao kwa wao. Idadi yao ni kamili, haiongezeki wala haipungui.
Na kuhusu kuitwa shetani hivyo hata binaadamu nao pia wanaweza kuitwa shetani?kwa jinsi ulivyo elezea hilo neno shetani.
Ndiyo binadamu naye anaweza kuitwa "shetani", sababu maana ya shetani ni adui, kama nilivyokuambia malaika waasi jina lao la asili siyo "shetani" bali ni "Malaika" au "Wana wa MUNGU".

Jina lingine ambalo MUNGU alilitumia kuwaita hawa malaika ni "Azazel". YESU alisema hivi; "ukitenda dhambi unakuwa mtoto wa Shetani na baba yako anakuwa ni Shetani, ukitenda mema unakuwa ni mtoto wa MUNGU na BABA yako anakuwa ni MUNGU".
 
Mkuu kila mtu ana alipotoa maelezo yake kuhusu hao viumbe,sasa wewe unadhani maelezo ya kwamba majini kuwa ni malaika yanaendana na uhalisia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…