Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
swali kwako--- kinachokuza lugha ni maneno mapya ama wigo wa uongeaji(matumizi ya ) lugha husika?
kiswahili ni lugha adhimu yenye misamiati ya kutosha ndio maana hata umoja wa mataifa na vyombo mbalimbali vya kimataifa vikiwemo bbc na deuch welle radio na vyuo vya kiswahili mfano beijing china na marekani na uingereza vinakitumia sana, tatizo liko hapa nyumbani kuanzia viongozi wetu wanahabari wetu mpaka watu w kawaida kabisa kuchanganya Kiswahili na kiingereza ili tu waonekane wa kisasa na wasomi
mwishowe wanajikuta hawawezi kuongea kiswahili fasaha wala kiingereza fasaha!
hebu jaribu kusoma magazeti ya udaku na hizi redio za udaku utatamani kutapika jinsi wanavyochanganya kiingereza na kiswahili
tatizo linaanzia bakita wapowapo tu, wakifuatiwa na walimu na wakufunzi kwenye shule na vyuo vya uandishi ni uvundo mtupu mwisho ni wamiliki wa vyombo vya habari
Siyo kwamba ''Daddy what birth do I fall among your kids?Daddy what child number am I among your children?
Sasa ingaliitwa MAWIMBI RUDIA MAWINGU huoni kama watu wangechoka kuitamka, au hata kuiogopa !!
Kujitosheleza ni pamoja na MATUMIZI yake ndugu. Hebu nieleze ipi ni sahihi kati ya 'tunatoa huduma saa 24' au 'tunatoa huduma masaa 24'? Vile vile nipe tafsiri ya 'college, institutes (medical, technical, etc), polytechnic, vocational centers, university na kadhalika.Hoja ninayoizungumzia hapa ni kuwa iwapo unatueleza kuwa Kiswahili hakijitoshelezi (kama ulivyofanya kwenye kichwa cha habari hii), basi huwezi kumlaumu mtumiaji Kiswahili kuchanganya Kiswahili na lugha nyengine
Iwapo unasema Kiswahili kinaweza kujitosheleza (walau kwa kiwango kikubwa zaidi ya inavyoonekana sasa), basi kichwa chako cha habari kimetupoteza.
Neno tosheleza katika uwanja wa lugha si zuri katika kuielezea kwa sababu sidhani kama kuna lugha inayojitosheleza hapa duniani na ndiyo maana mara kwa mara misamiati mipya huibuka.
Ila lugha hukua na kupanuka endapo tu wazungumzaji wake wataamua kuikuza na kuipanua.
Kwa sasa Kiswahili hakinipi matumaini ya kukua na kupanuka.
Kiini cha lugha ni nini? Ni maneno au ishara ambazo watu hutumia kujieleza ama kuelezea mawazo, fikra, na hisia zao baina yao.
Kwa hiyo, kinachokuza lugha ni matumizi ya misamiati ya hiyo lugha lakini uongezekaji wa misamiati mipya nayo hukuza lugha.
Nyongeza yoyote ile ya kitu chochote kile hukuza kitu hicho!
Kwenye kamusi za Kiingereza, kwa mfano, kwenye baadhi ya maneno huwa wanaweka na miaka ambayo neno au msamiati ulianza kutumika/ulipoingizwa kwenye kamusi.
Kwenye Kiswahili hilo sijaliona bado.
Usisikitike hivo ndugu bali LAUMU waliopewa dhamana ya kikikuza. Mie nilielezwa kuwa Wajerumani haswa ndio WALIOKISAMBAZA Kisawhili Tanganyika (na sio Kijerumani lakini alipoingia Mwingereza yeye alitilia maanani lugha yake) wakati wakitutawala ndio maana Baba wa Taifa alipata nafuu ya kukitumia kuwaelewesha wananchi maana ya UHURU.Duuuuuuuuu!!!!!!!!!! NIMESIKITIKA SANA KUSIKIA ETI KISWAHILI LUGHA YENYE THAMANI KUBWA, LUGHA AMBAYO ILITUMIWA NA BAADHI YA WAASISI KAMA MWL. JK NYERERE KUTUUNGANISHA NA KUWA HAPA TULIPO LEO ETI HAIJITOSHELEZI!!!! HUU NI UTATA WA KUTUPOTOSHA KAA CHINI NA UFIKIRI MCHANGO WA KISWAHILI!!!!! LUGHA IPI ILITUMIKA KUTUUNGANISHA TUKAPATA UHURU? SI KISWAHILI? SEMA MBONA KIMYA? TAFAKARI KABLA YA KUWASILISHA HOJA YAKO!!!