KERO Ukitaka kukata tiketi SGR unaambiwa treni imejaa, muda wa kuondoka treni inakuwa wazi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kama wana lipia waendelee kuhujumu tu. Shida ni pale kama hawalipii. Na system inafanya seat reservations
 
Taratibu titazoea. Mtu anakata tiketi.kumbe hana hakika ya safari. Haya ni mapinduzi.makubwa, asante CCM. Ni kama tulivyopata Uhuru toka kwa Mkoloni.
 

Ni vizuri hili jambo limejulikana mapema. ATC walikuwa hivyo. Kule mwanza ulikuwa unaambiwa ofisi za mjini kuwa nafasi hakuna mpaka saa 1 kabla ya kuondoka. Waliokuwa wajanja walienda uwanjani na walipata usafiri na siti nyingi zikawa ziko wazi pia. Enzi za 2009. Kifo kikaikuta. Sasa nashauri ikibaki nusu saa watoe tiketi mpya.Kwa abiria ambao hawajawasili nusu saa kabla treni kuondoka na kuingia ndani nafasi ziuzwe. Na hakuna kurudisha pesa.
 
Kama unafanya booking na unatakiwa kulipa ndani ya 50mn ni rahisi kufanya hujuma. Unaandaa vijana wanaishambulia system. Kila baada ya dk 50 na kila siti inayotokea inabukiwa. Lakini sidhani kama ni njia sustainable.
 
Sisi tupo Simba na Yanga na njozi zetu! Hakuna hata mwandishi mmoja anayeripoti hili. Wao wamebakia Aziz K na Pacome, Mzamiru nk.. Yale ya ATCL na Mwendokasi yanajirudia...
 
Naomba kujua masharti ya kupanda hii SGR. Nisije acha mizigo yangu station.😊😊
 
Kama kweli ni hivyo basi kuna shida kwemye mifumo ya ticket,
Nawashauri wapunguze muda wa kulipia zisiwe dk 45 bali 5., zikipita siti iwe huru kuuzwa kwa mtu mwingine
Hii ya kusubiri dk 45 kama kuna watu wanaeza fanya hujuma treni likaonekana limejaa kila siku
 
Kwani si wanalipa sasa shida ikl wapi unaita hujuma. Kiukweli hapo anaekuwa amehujumiwa ni wao maana wanalipa na huduma hawachukui.

Ila hizi zinaonekana ni baseless allegations tu. Mnapenda sana kutunga vitu ili kuleta taharuki. Mnakosea sana
Kinachofanyika hapo ni dumb reservation, hawalipi!! Ilikuwa inatokea sana Air Tanzania sijui kama bado inaendelea, unakata ticket unaambiwa ni last 3 seats, muda wa safari dege halijajaa
 
Yaani wanafanya booking na kulipia , treni ikienda wazi si wamepata faida au hesabu nyepesi kama hiyo imenishinda?

Lakini kama hawalipi hapo tunakuja kugundua hao wenye mabasi 90% ni wanaccm wanatumia kama scheme ya utakatishaji pesa.
 
Kinachofanyika hapo ni dumb reservation, hawalipi!! Ilikuwa inatokea sana Air Tanzania sijui kama bado inaendelea, unakata ticket unaambiwa ni last 3 seats, muda wa safari dege halijajaa
Umewahi kukata ticket za ndege mkuu kwa kufanya reservation?

Ukifanya booking kama hujalipa wanakupa booking kisha unapewa na deadline ya kulipia usipolipa hadi muda huo seat inarudi sokoni
 
Umewahi kukata ticket za ndege mkuu kwa kufanya reservation?

Ukifanya booking kama hujalipa wanakupa booking kisha unapewa na deadline ya kulipia usipolipa hadi muda huo seat inarudi sokoni
Nimefanya reservations za kutosha na unachosema ndo inatakiwa iwe hivyo,, kwamba baada ya muda fulani unconfirmed ticket zinarudi sokoni, kwa air Tanzania hii ilikuwa ni kera, nadhan lilikuwa ni swala la It
 
Bado Wana akili zile za zamani za TT?

Tukomae serikali itengeneza application/ mfumo rahisi ambao chati itakuwa online na ipigwe marufuku mteja kufika ofisini. Kwamba akishachagua daraja, behewa na namba ya siti, chati inaonyesha online. Mbona rahisi na fedha inaingia Moja kwe Moja serikalini kwa kuwa linked na GEPG?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…