Ukitaka kupima ustaarabu wa jamii husika angalia usafi wa maliwato yao. Hapa tumefeli sana

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Ni bahati mbaya kwamba kwenye jamii yetu sio maofisini, shuleni, vyuoni, majumbani, stendi, filling stations vyoo ni vichafu sana, na kwa baadhi ya jamii zetu vyoo ndio haviingiliki kabisa mfano ukienda Tukuyu mjini vyoo ni vichafu sana hata kwenye miji yetu.

Hali hii inapima kiwango chetu cha ustaarabu. Vyoo visafi ni vichache sana. Na inakuwa bahati mbaya vyoo kwenye vyuo vikuu ndio balaa na hao ndo wasomi. Hata niseme tubadilike sidhani kama tutabadilika ila kwa sehemu kubwa sisi ni wachafu sana.

Soma Pia: Haya mazingira ya Vyoo vya eneo la Kivuko pale Busisi ni hatari sana kwa afya

Hizo picha ni choo cha umma Arusha.


 
Mkuu Choo inayotumiwa na weng unataka ifanane na self contained room mzee??
 
Hicho mbona kisafi ushawahi fika chooni mpaka haja yenyewe inapotea tumboni.
 
Usafi ni jambo lisilohitaji hata kuwa na degree... Lakini unakuta mtu yupo educated kabisa lakini ndio anaacha vyoo vichafu....
 
Ukienda airport, stand zote mpya, ofisi za ma RC, DC hali niyo, kuna mwaka mstaafu mmoja alisema hata ukienda bungeni usione wale wanaulamba vile wapo wanao piga shabaha pembeni, nahiyi hii ni laana
 
Vyoo vikitumiwa na watu wengi lazima kuwe kuchafu. Halafu vingi unakuta maji hakuna,wanatumia yaliyomo kwenye ndoo,huko kwenye kuna wengine wanaingia wananawa huko huko.
 
Nyumba ni choo
 

Attachments

  • IMG_20241013_180319.jpg
    226.2 KB · Views: 4
  • IMG_20241013_180212.jpg
    260.9 KB · Views: 4
  • IMG_20241013_180513.jpg
    305.5 KB · Views: 4
  • IMG_20241013_180446.jpg
    220.5 KB · Views: 4
Asa mbona umepiga vyoo vya bar mkuu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…