DOKEZO Ukiukwaji wa sheria na ukwepaji kodi shule ya sekondari Mrisho Gambo

DOKEZO Ukiukwaji wa sheria na ukwepaji kodi shule ya sekondari Mrisho Gambo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Sir luta

Senior Member
Joined
Nov 28, 2022
Posts
163
Reaction score
221
Habari wana bodi,

Hii ni shule ya serikali inayosimamia na TAMISEMI iliyopo Jiji la Arusha. Sisi wazazi na jamii nzima tunaelewa na tunapewa elimu mara kwa mara na mamlaka mbalimbali za serikali kama vile TRA juu ya ulipaji wa kodi na kudai risiti na tunatambua pia kuwa ktk shule hizi za serikali michango iliyokubaliwa lazima ilipwe kwenye akaunti ya shule.

Cha kusikitisha na kushangaza katika shule hii ya mrisho gambo sekondari, tunalipa fedha mkononi (cash) na kwenye simu ya mwalimu na hakuna risiti!

Hii shule ina mabweni yaliyokamilika ambayo yalijengwa kwa fedha zilizotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha. Sasa sharti la mtoto kupata nafasi ya kulala kwenye haya mabweni lazima awe amelipa michango ifuatayo;

1. TZS 700,000/= kwa mwaka kwa ajili ya hosteli
2. TZS 200,000/= kwa ajili ya kitanda na hizi fedha zimekuwa zinatolewa na mzazi anayehamishia mtoto kwenye hii shule tangu mwaka juzi 2023 lakini hakuna kitanda kinachonunuliwa.
3. TZS 100,000/= kwa ajili ya dawati kwa mwanafunzi anayehamia toka shule nyingine.

Utaratibu wa malipo ya TZS 700,000/= zinalipwa nusu kwa mwl mkononi anakuandika jina na hakuna risiti au unaingiza kwenye namba yake ya simu ambayo ni 0712-473481 na nyingine ya voda.

Utaratibu wa malipo ya TZS 200,000/= na TZS 100,000/= zinalipwa mkononi kwa Mkuu wa shule anakuandika jina hakuna risiti. Hivi kwa wanafunzi 500 ni kiasi kikubwa cha pesa kukusanywa kienyeji bila kupitia kwenye akaunti na zinatumika bila kufuata taratibu za manunuzi.

Hivi serikali ipo macho kweli kwa shule ambayo ipo mjini katika mkoa ambao unasemwa una mkuu wa mkoa mchapakazi? Ina mbunge mchapakazi tena shule ina jina lake? Wizara zinazohusika zichukue hatua ama shule zote nchi nzima ziruhusiwe kufanya hivyo.
 
Hoja ni nini pesa kukusanywa bila risiti au shule kutolopa kodi? Na je kwanini umhamishe mwanao kwenye hiyo shule yenye "mizengwe" ikiwa zingine "safi" zipo?
 
Un
Shule ya serikali ilipe kodi?Acha ujinga mkuu.
Hapo labda kama una hoja ya ubadhirifu lakini sio mambo ya kulipa kodi
Unajua kuna aina ngapi za kodi? Tozo za miamala ya kibenki siyo kodi?
 
Hoja ni nini pesa kukusanywa bila risiti au shule kutolopa kodi? Na je kwanini umhamishe mwanao kwenye hiyo shule yenye "mizengwe" ikiwa zingine "safi" zipo?
Kwahiyo wizi uvumiliwe usiripotiwe hata kama huna mtoto anayesoma hapo?
 
Kichwa cha habari na maudhui ya ndani, hata haviendani! Hapo shida ni kutokuwepo tu na utaratibu mzuri wa kukusanya hiyo michango. Na siyo ukwepajiwa kodi. Shule za serikali na kulipa kodi, wapi na wapi!
 
Kichwa cha habari na maudhui ya ndani, hata haviendani! Hapo shida ni kutokuwepo tu na utaratibu mzuri wa kukusanya hiyo michango. Na siyo ukwepajiwa kodi. Shule za serikali na kulipa kodi, wapi na wapi!
Pesa inapopitia kwenye akaunti serikali inapata kodi kupitia tozo mbalimbali, lakini pesa ikikusanywa mkononi haipati hiyo tozo.
 
Habari wana bodi,

Hii ni shule ya serikali inayosimamia na TAMISEMI iliyopo Jiji la Arusha. Sisi wazazi na jamii nzima tunaelewa na tunapewa elimu mara kwa mara na mamlaka mbalimbali za serikali kama vile TRA juu ya ulipaji wa kodi na kudai risiti na tunatambua pia kuwa ktk shule hizi za serikali michango iliyokubaliwa lazima ilipwe kwenye akaunti ya shule.

Cha kusikitisha na kushangaza katika shule hii ya mrisho gambo sekondari, tunalipa fedha mkononi (cash) na kwenye simu ya mwalimu na hakuna risiti!

Hii shule ina mabweni yaliyokamilika ambayo yalijengwa kwa fedha zilizotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha. Sasa sharti la mtoto kupata nafasi ya kulala kwenye haya mabweni lazima awe amelipa michango ifuatayo;

1. TZS 700,000/= kwa mwaka kwa ajili ya hosteli
2. TZS 200,000/= kwa ajili ya kitanda na hizi fedha zimekuwa zinatolewa na mzazi anayehamishia mtoto kwenye hii shule tangu mwaka juzi 2023 lakini hakuna kitanda kinachonunuliwa.
3. TZS 100,000/= kwa ajili ya dawati kwa mwanafunzi anayehamia toka shule nyingine.

Utaratibu wa malipo ya TZS 700,000/= zinalipwa nusu kwa mwl mkononi anakuandika jina na hakuna risiti au unaingiza kwenye namba yake ya simu ambayo ni 0712-473481 na nyingine ya voda.

Utaratibu wa malipo ya TZS 200,000/= na TZS 100,000/= zinalipwa mkononi kwa Mkuu wa shule anakuandika jina hakuna risiti. Hivi kwa wanafunzi 500 ni kiasi kikubwa cha pesa kukusanywa kienyeji bila kupitia kwenye akaunti na zinatumika bila kufuata taratibu za manunuzi.

Hivi serikali ipo macho kweli kwa shule ambayo ipo mjini katika mkoa ambao unasemwa una mkuu wa mkoa mchapakazi? Ina mbunge mchapakazi tena shule ina jina lake? Wizara zinazohusika zichukue hatua ama shule zote nchi nzima ziruhusiwe kufanya hivyo.
Chuki mbaya sana, lakini roho mbaya pia ni uchawi.. Umeandika kwa personal interest zako na hao wafanyakazi wenzako.
 
Chuki mbaya sana, lakini roho mbaya pia ni uchawi.. Umeandika kwa personal interest zako na hao wafanyakazi wenzako.
Unatetea wezi? Ni sawa michango kukusanywa kienyeji hivyo? Sheria ya fedha inasemaje? Acha hisia tetea maslahi ya taifa
Chuki mbaya sana, lakini roho mbaya pia ni uchawi.. Umeandika kwa personal interest zako na hao wafanyakazi wenzako.
Utaratibu wa kuhifadhi fedha kwenye strong room ulishapitwa na wakati matukio ya wizi ni makubwa. Lakini pia huu ni wizi kama wa yule trafiki aliyekuwa anazikisanya barabarani
 
Back
Top Bottom