Ukiunganisha dot ndo utaelewa: Alitolewa Kakoko bandarini akatolewa Chamriho ujenzi, akatolewa Kalemani Nishati n.k

Ukiunganisha dot ndo utaelewa: Alitolewa Kakoko bandarini akatolewa Chamriho ujenzi, akatolewa Kalemani Nishati n.k

sambulugu

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2021
Posts
4,485
Reaction score
8,562
Nasema hivo kwa sababu zifatazo:

Kwanza mara tu baada ya Rais Samia kuingia alifanya mabadiliko bandarini akidaiwa kuwa Kakoko ni fisadi na akawekwa chini ya uchunguzi ambao mpaka leo hakuna kilichoelezwa kwa undani tofauti na propaganda! Naweza kuamini kuwa Kakoko alitolewa pale kutokana na msimamo wake tayari kuhusu bandari ya BAGAMOYO amabayo alikuwa anaipinga sana!

Pili Rais Samia alifanya mabadiliko katika vizara ya ujenzi kwa kumtoa Chamriho hili nalo ukiliangalia kwa umakini Chamriho amekuwa katibu mkuu wa wizara ya ujenzi kwa mda mrefu kwa hiyo katika majadiriano ya bandari pendwa ya Msoga team BAGAMOYO alihusika kwa sehemu kubwa na ukizingatia tayari bandari hiyo ulikuwa ishaanza kupata mkwamo team ikaoma hata huyu Eng Chamriho anaweza kuwa kikwazo akawekwa pembeni bila sababu zenye mashiko!

Tatu ukitizama mabadiliko ya hivi karibuni ya kumtoa Kalemani bado utagundua mi mwendelezo wa kuwaondoa watu waliokiwa na msimamo wa kizalendo juu ya mikataba mibovu, hapa unaweza kuona Waziri wa sasa Makamba akifanya mikutano mingi na wawekezaji katika sekta ya gesi, kwa upande mwingine licha ya makamba kupingana na ujenzi wa bwawa la Mwl Nyerere lakini bado kupewa uwaziri ili kutimiza mision ambayo tayari ishapangwa na watawala ya awamu hii ya Sita hususani kwenye eneo la Gesi,eneo ambalo awamu ya nne ilituletea janga kubwa kwa mkataba wa ovyo wa gesi ya mtwara ambayo hata wana Mtwara wenyewe hawajui inafaida gani mpaka leo!

Nne mda si mrefu mtaona mabadiliko pia katika wizara ya nishati na madini sio kwa sababu waziri ni mbovu ila kwa sababu kuna vitu haviendi sawa vya kundi fulani la watu! Siku za hivi karibuni Waziri Biteko amekuwa akishutumiwa kwa ufisadi usio bayana akihusishwa pia na upotevu wa tanzanite kule mererani n.k yote hayo ni dalili kuwa hatakiwi kwenye hiyo wizara na bila shaka Waziri Mchengerwa amabaye huko utumishi alidokeza kuhusu uchunguzi juu ya wizara hii!
Hitimisho,Ikumbukwe kuwa nchi hii sio ya CCM na Sio ya team Msoga, haya yote yanayofanyika ya kuja kuwadanganya watanzania hususani kwenye mradi wa bandari ya BAGAMOYO ni hatari kubwa kwa hapo baadae kama yatafanyika bila umakini mkubwa,Serkali hii asidhanie kuwa watanzania ni wajinga kiasi hicho cha kuruhusu ujenzi wa bandari ambayo utaathiri bandari zetu hususani bandari ya Dar es salaam!
 
nasubiri kwa hamu uzao wa miaka ya sabini kama watakuwa tayari kuvumilia kwa kiasi hiki eti tuungane wizara nne halafu tuwape watu watutawale kwa wizara zote huku wakituwekea watumishi na wakuu wa wilaya na muda si mrefu wakuu wa mikoa kutoka Zanzibar katika maeneo yasiyo ya muungano hapa patachimbika tu! kwa sasa nafikiri tunakaribia kukubali Muungano wa serikali tatu.
 
Msitegemee mema yoyote yale katika mchakato huo ambako majizi yamepanga safu ya mashambulizi!

Mission ni bandari ijengwe wapige hela ndefu toka kwa wawekezaji wa kichina😅! Zitaongelewa story nyingi ila ni yale yale tu...

Fanikisheni dili katika zile Trillion 70 mtakula mgao wa 10 Trillion na hapo mzigo unatembea kuanzia kwa mawaziri, Ex boyfrendi wa bibi tozo pamoja na wapambe wake!
 
Hitimisho,Ikumbukwe kuwa nchi hii sio ya CCM na Sio ya team Msoga,
Na pia siyo ya team mwendazake wala wahutu wala Sukuma Gang
haya yote yanayofanyika ya kuja kuwadanganya watanzania hususani kwenye mradi wa bandari ya BAGAMOYO ni hatari kubwa kwa hapo baadae kama yatafanyika bila umakini mkubwa,Serkali hii asidhanie kuwa watanzania ni wajinga kiasi hicho cha kuruhusu ujenzi wa bandari ambayo utaathiri bandari zetu hususani bandari ya Dar es salaam!
Ila mwendazake peke yake aliyekuwa na mamlaka ya kuwafanya watanzania wote wajinga. Mwendazake angeutoa hadharani huo mkataba mbaya haya yote yasingekuwepo. Yeye angetamani hiyo Bandari ingejengwa Chalttle.
 
Hii kusema inasaidia sana,kuliko kuogopa kuitwa Sukuma gang KWA watu waliokosa uzalendo ndani ya nchi hii,Tunapigwa nje na ndani tena KWA speed ya Tozo na Mfumuko wa bei kila kona
Kwa hiyo yaliyokosa uzalendo enzi za sgang sasa yanatanatakiwa ya pate uzalendo enzi mpya, au lisilo na manufaa Kwa sgang nikukosa uzalendo, yafaa tujifunze upya maana ya kizalendo, tuachane na uzalendo wa kisiasa au uzalendo wa kitanzania🤔.
 
Na pia siyo ya team mwendazake wala wahutu wala Sukuma Gang

Ila mwendazake peke yake aliyekuwa na mamlaka ya kuwafanya watanzania wote wajinga. Mwendazake angeutoa hadharani huo mkataba mbaya haya yote yasingekuwepo. Yeye angetamani hiyo Bandari ingejengwa Chalttle.
Kwa hiyo hao niliowataja pale ni wasukuma wote? Usiwe unaendeshwa na mihemko ya propaganda hakuna kitu kinaitwa sukuma gang! Ila msoga ipo na inafanya ufisadi ma ujinga ndani ya nchi hii sana tu!
 
Back
Top Bottom