Ukiunganishwa na Yesu historia yako inabadilika

Ukiunganishwa na Yesu historia yako inabadilika

hamis77

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
13,628
Reaction score
20,992
ANDIKO LA MSINGI

Yohana 1:43-46. Biblia inasema hivi:

"43. Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate. 44. Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro. 45. Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti. 46. Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone."


Ni muhimu kufahamu kuwa Nazareti ulikuwa ni mji mdogo uliokuwa kusini mwa jimbo la Galilaya (Lower Galilee). Mji huu ulikuwa miongoni mwa miji iliyodharauliwa sana. Kwa ujumla, Israeli ilikuwa na majimbo makuu matatu:

1. Yuda


2. Samaria


3. Galilaya



Yuda liliheshimika sana kwa sababu lilikuwa eneo lililotoa manabii na viongozi wakubwa walioonyesha utii kwa Mungu. Lakini Galilaya na Samaria hayakuwa maeneo yenye heshima kutokana na historia zake za:

Kuwa na ibada za sanamu

Watu wasioshika dini

Viongozi waovu na wasiomcha Mungu


Kwa sababu hizi, Galilaya ilidharaulika na kuonekana kama mji usioweza kutoa neno jema.


images (4).jpeg


Nazareti na Unabii wa Masihi

Kwa mujibu wa unabii wa Agano la Kale, Masihi alitarajiwa kutoka Yuda, haswa katika mji wa Daudi – Bethlehemu.

Mika 5:2 inasema:
"Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele."

Hii ilithibitishwa pia katika Mathayo 2:1-6, ambapo mamajusi walikuja kuuliza:
"Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia."

Hata wakuu wa makuhani na waandishi walithibitisha kuwa Masihi atazaliwa Bethlehemu ya Uyahudi.


Kwa Nini Nathanaeli Alihoji Kuhusu Nazareti?

Kwa msingi wa mafundisho ya kiyahudi, ilikuwa vigumu kwa Nathanaeli kuamini kuwa mtu aliyetabiriwa na Musa na manabii angeweza kutoka Nazareti.

Kwa ujumla, Nazareti ulikuwa mji usioheshimika, uliosifika kwa:

Umasikini mkubwa

Mmomonyoko wa maadili

Watu wasiomcha Mungu

Waabudu sanamu


Nazareti haikuwahi kutajwa katika unabii wa Agano la Kale. Wakati huo, mtu akitoka Nazareti alionekana sawa tu na mtu anayetokea maeneo ya kawaida yasiyo na heshima, kama vile: Mbagala, Gongo la Mboto, Manzese, Kwatango, Kilosa, Mbulizaga (Pangani), Kwa Msisi (Handeni), Nchebebwa (Newala) au Naluleo (Liwale).

Katika Yohana 7:40-42, 52, tunasoma jinsi maadui wa Yesu walivyotumia mji wake kama njia ya kumdharau.


Mathayo na Unabii wa Nazareti

Mathayo 2:19-23 inaonyesha kuwa Mathayo alijaribu kuonyesha kuwa kuna unabii kuhusu Yesu kuitwa Mnazareti.

Hii inahusiana na Isaya 11:1, ambapo neno "shina" au "chipukizi" kwa Kiebrania ni "Netser", ambalo linafanana na jina Nazareti.



Mafundisho Muhimu kutoka kwa Somo Hili

✔ Mungu anaweza kuinua mtu kutoka hali ya kudharaulika.
✔ Ingawa Nazareti ilikuwa mji mdogo na usio na heshima, jina lake lilipounganishwa na Yesu Kristo, likapata umaarufu mkubwa duniani.
✔ Yesu alikubali kuitwa Yesu wa Nazareti.
✔ Majini na mapepo yalipotajiwa jina la Yesu wa Nazareti, yaliogopa na kutoka kwa nguvu.
✔ Mitume walipotenda miujiza walilitumia jina la Yesu Kristo wa Nazareti.
✔ Leo hii, mji wa Nazareti ni maarufu kwa sababu ya Yesu Kristo.

Mtu akipokea Yesu Kristo, maisha yake hubadilika kabisa. Haijalishi unatokea ukoo gani, kabila gani, au jamii gani, ukiunganishwa na Yesu, historia yako inabadilika. Hata kama ulikuwa mnyonge kiasi gani, Mungu anaweza kukuinua na kukutumia kwa njia ya ajabu.

Filipo
alimwambia Nathanaeli:
"Njoo uone!"

✅ Mtu akiunganishwa na Yesu, maisha yake yanabadilika!
 
(Ukiunganishwa) ajira tuzipate kwa connection Yesu nae hadi connection?

Hatujafika huko ☹️
 
ANDIKO LA MSINGI

Yohana 1:43-46. Biblia inasema hivi:

"43. Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate. 44. Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro. 45. Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti. 46. Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone."


Ni muhimu kufahamu kuwa Nazareti ulikuwa ni mji mdogo uliokuwa kusini mwa jimbo la Galilaya (Lower Galilee). Mji huu ulikuwa miongoni mwa miji iliyodharauliwa sana. Kwa ujumla, Israeli ilikuwa na majimbo makuu matatu:

1. Yuda


2. Samaria


3. Galilaya



Yuda liliheshimika sana kwa sababu lilikuwa eneo lililotoa manabii na viongozi wakubwa walioonyesha utii kwa Mungu. Lakini Galilaya na Samaria hayakuwa maeneo yenye heshima kutokana na historia zake za:

Kuwa na ibada za sanamu

Watu wasioshika dini

Viongozi waovu na wasiomcha Mungu


Kwa sababu hizi, Galilaya ilidharaulika na kuonekana kama mji usioweza kutoa neno jema.


View attachment 3264259

Nazareti na Unabii wa Masihi

Kwa mujibu wa unabii wa Agano la Kale, Masihi alitarajiwa kutoka Yuda, haswa katika mji wa Daudi – Bethlehemu.

Mika 5:2 inasema:
"Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele."

Hii ilithibitishwa pia katika Mathayo 2:1-6, ambapo mamajusi walikuja kuuliza:
"Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia."

Hata wakuu wa makuhani na waandishi walithibitisha kuwa Masihi atazaliwa Bethlehemu ya Uyahudi.


Kwa Nini Nathanaeli Alihoji Kuhusu Nazareti?

Kwa msingi wa mafundisho ya kiyahudi, ilikuwa vigumu kwa Nathanaeli kuamini kuwa mtu aliyetabiriwa na Musa na manabii angeweza kutoka Nazareti.

Kwa ujumla, Nazareti ulikuwa mji usioheshimika, uliosifika kwa:

Umasikini mkubwa

Mmomonyoko wa maadili

Watu wasiomcha Mungu

Waabudu sanamu


Nazareti haikuwahi kutajwa katika unabii wa Agano la Kale. Wakati huo, mtu akitoka Nazareti alionekana sawa tu na mtu anayetokea maeneo ya kawaida yasiyo na heshima, kama vile: Mbagala, Gongo la Mboto, Manzese, Kwatango, Kilosa, Mbulizaga (Pangani), Kwa Msisi (Handeni), Nchebebwa (Newala) au Naluleo (Liwale).

Katika Yohana 7:40-42, 52, tunasoma jinsi maadui wa Yesu walivyotumia mji wake kama njia ya kumdharau.


Mathayo na Unabii wa Nazareti

Mathayo 2:19-23 inaonyesha kuwa Mathayo alijaribu kuonyesha kuwa kuna unabii kuhusu Yesu kuitwa Mnazareti.

Hii inahusiana na Isaya 11:1, ambapo neno "shina" au "chipukizi" kwa Kiebrania ni "Netser", ambalo linafanana na jina Nazareti.



Mafundisho Muhimu kutoka kwa Somo Hili

✔ Mungu anaweza kuinua mtu kutoka hali ya kudharaulika.
✔ Ingawa Nazareti ilikuwa mji mdogo na usio na heshima, jina lake lilipounganishwa na Yesu Kristo, likapata umaarufu mkubwa duniani.
✔ Yesu alikubali kuitwa Yesu wa Nazareti.
✔ Majini na mapepo yalipotajiwa jina la Yesu wa Nazareti, yaliogopa na kutoka kwa nguvu.
✔ Mitume walipotenda miujiza walilitumia jina la Yesu Kristo wa Nazareti.
✔ Leo hii, mji wa Nazareti ni maarufu kwa sababu ya Yesu Kristo.

Mtu akipokea Yesu Kristo, maisha yake hubadilika kabisa. Haijalishi unatokea ukoo gani, kabila gani, au jamii gani, ukiunganishwa na Yesu, historia yako inabadilika. Hata kama ulikuwa mnyonge kiasi gani, Mungu anaweza kukuinua na kukutumia kwa njia ya ajabu.

Filipo
alimwambia Nathanaeli:
"Njoo uone!"

✅ Mtu akiunganishwa na Yesu, maisha yake yanabadilika!
Amina,Amina,kila alisikiaye na Aseme,Amina!
 
Unazungumzia Yesu yule Mtoto WA seremala au Yesu Brian deacon ?
 
Embu ndugu hamis77 naomba nikuulize jambo hivi ili jina lako linamaanisha uliwahi kuwa muislam then Nuru ya Yesu ikakutoa huko? Au wewe ni mkristo ni jina TU la kiislamu uliamua kutumia kwenye avatar Yako?
Kama ulikuwa muislam na baadae kuhamia ukiristo napenda kukupa pongezi kwa sababu umechagua upande ambao ni wa Nuru Wala Giza halitaambatana nawe daima. Na Yale makazi aliyotuahidi bwana Yesu kipindi anapaa kurudi mbinguni kwa huruma za mwakozi naamini tutafikia.
 
Embu ndugu hamis77 naomba nikuulize jambo hivi ili jina lako linamaanisha uliwahi kuwa muislam then Nuru ya Yesu ikakutoa huko? Au wewe ni mkristo ni jina TU la kiislamu uliamua kutumia kwenye avatar Yako?
Kama ulikuwa muislam na baadae kuhamia ukiristo napenda kukupa pongezi kwa sababu umechagua upande ambao ni wa Nuru Wala Giza halitaambatana nawe daima. Na Yale makazi aliyotuahidi bwana Yesu kipindi anapaa kurudi mbinguni kwa huruma za mwakozi naamini tutafikia.
Mimi nilikuwa huko ,nimezaliwa familia ya Uislamu

Kwahiyo nili ritadi na kuwa mkristo
 
Back
Top Bottom