Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,677
Asikudanganye mtu hakuna chochote kigeni kwenye hii dunia. Mambo yanayotokea leo hii yalishakuwepo kwenye huu ulimwengu miaka maelfu kwa maelfu iliyopita.
Unaongelea kuhusu rushwa, chuki, wivu, ukatili, ukabila, upendeleo, kulewa madaraka, magonjwa, mauaji etc etc yote utayakuta kwenye vitabu vitakatifu na ni vitu vilikuwa vinatokea kwenye karne zote za ulimwengu huu.
Maana yake, matukio yote ya sasa kwenye maisha tunayoishi, asilimia kubwa ni marudio tu ya mambo yaliyokwisha kutokea zama za nyuma.
Lakini kuna kitu kimoja watu huwa wanakipuuza, katika zama za enzi zilizopita, kumebarikiwa kuwa na watu wenye akili ambazo ni vigumu sana kuzipata kwenye watu wa dunia ya sasa ya kidigitali.
Akili hizi na maarifa ya wanafalsafa wa enzi, ndizo haswa zilizowezesha jamii za karne hizo kuweza kushindana na madhila na changamoto ambazo zilikuwa zinawakabili, kama ki siasa, kiuchumi, kijamii, kivita, kiteknolojia, kidini n.k
Maana yake ni kwamba Ukitaka kujifunza chochote kwenye ulimwengu wa sasa, fanya kurejelea maandiko ya wanafalsafa wa miaka ya zamani. Na huko ndiko busara ya kuchanganua maisha na changamoto za jamii itapatikana.
Ni kwanini, leo watu wanamuimba Nyerere ni kiongozi bora, ni simply kwa sababu nyerere alikuwa msomi mzuri wa falsafa.
Sikiliza hotuba zote za Nyerere kwenye masuala ya uchumi, halafu nenda kasome kazi za wanafalsafa wa uchumi akina Adam Smith, David Ricardo, au John Keynes.. utagundua anapita mule mule.. Ni kama vile alikuwa anachukua masomo ya wanafalsafa na kuyaleta kwenye applicability ya uchumi wa Tanzania..
Na hapo ndipo Nyerere alifaulu, kusoma kazi za wanafalsafa na kuzi apply kwenye content ya Tanzania. Sio kwamba Nyerere alikuwa Mungu mtu.. No.
*****
Hakuna mtu anayezijua vema falsafa, akachukua kiboko akamtandika mwenzake hadharani. Ukisoma vema falsafa, utakutana na maandiko ambayo daima yatakufanya uwe mtu mwema sana kwenye jamii, na mtu mwenye mawazo mema na ya busara.
Juzi kati hapa nilikuwa namsoma mwanafalsafa mmoja anaitwa 'Rene Deskates' kuna quote yake moja inasema "Greatest minds are capable of greatest vices and also of greatest virtues" kwa kiswahili ni kwamba, ' Watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili wana uwezo wa kufanya matendo mema na pia wanauwezo wa kufanya ukatili wa kutisha.
Mstari kama huo hapo juu unaweza kumfanya kiongozi kuwa mpole sana wakati wote anapo deal na raia wake, maana huwezi jua huyo unayemnyanyulia fimbo kumchapa ni mtu wa aina gani na anauwezo wa kukufanya kitu gani.
Mambo kama hayo, yenye ufanano huo. Ni kukumbushana tu. Kuzijua falsafa ni kitu cha lazima sana kwa viongozi na wote ambao wana deal sana na jamii.
Wanafalsafa wenyewe ni wale kama kina Plato, Aristotle, soma Bible pia, Quran, Karl Max, wapo mamia kwa mamia, just tenga mda uwe unawasoma hao watu.
Na wamegawanyika makundi makundi.. kuna wanafalsafa upande wa uchumi, dini, siasa, sanaa, saikolojia, mahusiano ya jamii, sayansi, hisabati.. n.k ni wewe tu kuchagua wapi pa kuanza.. lakino kila mmoja utayemsoma lazima ujifunze kitu kipya
Kuna saa huwa nakaa natafakari, najisemea mwenyewe, watu kama kina Magufuli, Makonda, Sabaya na wengineyo, wangekuwa ni viongozi bora sana ikiwa wangezifahamu vyema falsafa.
Hakuna mwanafalsafa atayekushauri kufanya mabovu waliyofanya. Hakuna.
Nahisi kama ingekuwa ni amri yangu, qualification ya kuwa mwanasiasa, ingepaswa kwanza iwe mtu una degree ama cheti cha kwamba umesoma falsafa.
Ni hayo tu.
N. Mushi
Unaongelea kuhusu rushwa, chuki, wivu, ukatili, ukabila, upendeleo, kulewa madaraka, magonjwa, mauaji etc etc yote utayakuta kwenye vitabu vitakatifu na ni vitu vilikuwa vinatokea kwenye karne zote za ulimwengu huu.
Maana yake, matukio yote ya sasa kwenye maisha tunayoishi, asilimia kubwa ni marudio tu ya mambo yaliyokwisha kutokea zama za nyuma.
Lakini kuna kitu kimoja watu huwa wanakipuuza, katika zama za enzi zilizopita, kumebarikiwa kuwa na watu wenye akili ambazo ni vigumu sana kuzipata kwenye watu wa dunia ya sasa ya kidigitali.
Akili hizi na maarifa ya wanafalsafa wa enzi, ndizo haswa zilizowezesha jamii za karne hizo kuweza kushindana na madhila na changamoto ambazo zilikuwa zinawakabili, kama ki siasa, kiuchumi, kijamii, kivita, kiteknolojia, kidini n.k
Maana yake ni kwamba Ukitaka kujifunza chochote kwenye ulimwengu wa sasa, fanya kurejelea maandiko ya wanafalsafa wa miaka ya zamani. Na huko ndiko busara ya kuchanganua maisha na changamoto za jamii itapatikana.
Ni kwanini, leo watu wanamuimba Nyerere ni kiongozi bora, ni simply kwa sababu nyerere alikuwa msomi mzuri wa falsafa.
Sikiliza hotuba zote za Nyerere kwenye masuala ya uchumi, halafu nenda kasome kazi za wanafalsafa wa uchumi akina Adam Smith, David Ricardo, au John Keynes.. utagundua anapita mule mule.. Ni kama vile alikuwa anachukua masomo ya wanafalsafa na kuyaleta kwenye applicability ya uchumi wa Tanzania..
Na hapo ndipo Nyerere alifaulu, kusoma kazi za wanafalsafa na kuzi apply kwenye content ya Tanzania. Sio kwamba Nyerere alikuwa Mungu mtu.. No.
*****
Hakuna mtu anayezijua vema falsafa, akachukua kiboko akamtandika mwenzake hadharani. Ukisoma vema falsafa, utakutana na maandiko ambayo daima yatakufanya uwe mtu mwema sana kwenye jamii, na mtu mwenye mawazo mema na ya busara.
Juzi kati hapa nilikuwa namsoma mwanafalsafa mmoja anaitwa 'Rene Deskates' kuna quote yake moja inasema "Greatest minds are capable of greatest vices and also of greatest virtues" kwa kiswahili ni kwamba, ' Watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili wana uwezo wa kufanya matendo mema na pia wanauwezo wa kufanya ukatili wa kutisha.
Mstari kama huo hapo juu unaweza kumfanya kiongozi kuwa mpole sana wakati wote anapo deal na raia wake, maana huwezi jua huyo unayemnyanyulia fimbo kumchapa ni mtu wa aina gani na anauwezo wa kukufanya kitu gani.
Mambo kama hayo, yenye ufanano huo. Ni kukumbushana tu. Kuzijua falsafa ni kitu cha lazima sana kwa viongozi na wote ambao wana deal sana na jamii.
Wanafalsafa wenyewe ni wale kama kina Plato, Aristotle, soma Bible pia, Quran, Karl Max, wapo mamia kwa mamia, just tenga mda uwe unawasoma hao watu.
Na wamegawanyika makundi makundi.. kuna wanafalsafa upande wa uchumi, dini, siasa, sanaa, saikolojia, mahusiano ya jamii, sayansi, hisabati.. n.k ni wewe tu kuchagua wapi pa kuanza.. lakino kila mmoja utayemsoma lazima ujifunze kitu kipya
Kuna saa huwa nakaa natafakari, najisemea mwenyewe, watu kama kina Magufuli, Makonda, Sabaya na wengineyo, wangekuwa ni viongozi bora sana ikiwa wangezifahamu vyema falsafa.
Hakuna mwanafalsafa atayekushauri kufanya mabovu waliyofanya. Hakuna.
Nahisi kama ingekuwa ni amri yangu, qualification ya kuwa mwanasiasa, ingepaswa kwanza iwe mtu una degree ama cheti cha kwamba umesoma falsafa.
Ni hayo tu.
N. Mushi