Ukiwa na hela unaanza kuona kuweka kava la simu kama ushamba

Ukiwa na hela unaanza kuona kuweka kava la simu kama ushamba

Nna mda sasa natumia simu zangu bila kuweka kava yani inafika wakati naona kama kuweka kava ni ushamba flani.

Imagine watu wamekaa Apple huko wame design product yao wamekubaliana na muonekano wake wameamua kuachia kitu na raia wamekielewa alafu anakuja mtu anaweka kava yani inaondoa mantik nzima ya design ya simu.

Zamani nilikuwa na woga kwamba nikitumia simu bila kava itachakaa mapema lakini nimegundua kuwa hata simu ikiwa na kava pia inachakaa so nikaona kuweka kava ni dalili ya umaskini nikaachaga.

Sikuhizi nikiona mtu kaweka simu kava namuona kama wale wabibi wa zamani wanaonunua kochi alafu wanaweka vitambaa ili kochi lisichafuke au wale wabibi wa marekani wananunua kochi kisha wanafunika na kava la plastic ili lisichakae.

Kama unapenda bidhaa enjoy kama ilivyo. Nikiona mtu ana kava kwenye simu namuona kama mtu aliyetoka kijijini yani wakuja View attachment 2330888
Na sie mafundi mechanical tusiweke cover babu
 
Mimi lazima niweke cover kwasababu sipendi kushika simu nikasikia ule usoft.lakini pia simu ni yangu mambo ya muonekano yananihusu mwenyewe sio mtu mwingine.
 
Mimi acha tu nionekane mshamba
Kava naweka kwasababu huwa naiangusha hovyo na kuilinda na vumbi kutokana na mishemishe zangu.
 
ukiona bado unatumia vifaa kujitangaza una pesa,mfano kuvaa nguo za gharama,saa kali,simu unaacha uchi ujue bado hujazikamata.

wenye mpunga wa kwenda wanaakuwa na majina makubwa mpaka wao ndio wanatangaza bidhaa,yaani eron musk kuonekana na iphone ni mchongo kwa apple.
Wewe unaongelea upuuzi gani sasa elon musk wawe wangapi? Nimesema ukifika level unaona simu si kitu cha kuhangaika nacho yani unakiwaza mpaka unakiwekea ulinzi kana kwamba kikifa hutapata tena huwezi ukahangaika na makava. Angalia watu wengi ambao kutoa hela kununua simu ya million 3 siyo ishu mara nyingi simu zao hata hazina kava wala glass protector yani hawazi itaharibika au itachakaa atashindwa kuiuza, yeye simu ikipasuka ananunua tu nyingine tena haendi yeye anampa dereva hela akamnunulie.

Ni sawa na mtu mwenye hela ya mawazo akipata hela ya kununua gari atanunua toyota kisa anahofia gharama za spea, ila waliovuka kiwango cha kuwaza spea za gari huwa wananunua tu gari yoyote iwe benzi au bwm bila kuhofia spea kwakuwa washavuka level ya kuhofia gharama za spea kwa kuwa wanazimudu.

Lakini then simu umenunua imetengenezwa na finishing nzuri ya titanium, aluminium na glass unaenda kuifunika na maplastiki ya bei nafuu.
 
Wewe unaongelea upuuzi gani sasa elon musk wawe wangapi? Nimesema ukifika level unaona simu si kitu cha kuhangaika nacho yani unakiwaza mpaka unakiwekea ulinzi kana kwamba kikifa hutapata tena huwezi ukahangaika na makava. Angalia watu wengi ambao kutoa hela kununua simu ya million 3 siyo ishu mara nyingi simu zao hata hazina kava wala glass protector yani hawazi itaharibika au itachakaa atashindwa kuiuza, yeye simu ikipasuka ananunua tu nyingine tena haendi yeye anampa dereva hela akamnunulie.

Ni sawa na mtu mwenye hela ya mawazo akipata hela ya kununua gari atanunua toyota kisa anahofia gharama za spea, ila waliovuka kiwango cha kuwaza spea za gari huwa wananunua tu gari yoyote iwe benzi au bwm bila kuhofia spea kwakuwa washavuka level ya kuhofia gharama za spea kwa kuwa wanazimudu.

Lakini then simu umenunua imetengenezwa na finishing nzuri ya titanium, aluminium na glass unaenda kuifunika na maplastiki ya bei nafuu.
Unahisi uko sawa???
 
Mimi kwa uzoefu wangu wa kuweka kava kwenye zimu zangu zilizopita nimegundua yafuatayo.

Cover zinatunza vumbi na uchafu hasa kwenye kingo za simu.

Cover zikiingia mchanga mdogo mdogo unasagwa baina ya mgongo wa simu na cover hali inayosababisha michubuko kwenye mgongo wa simu ( back)

Baadhi ya cover zinababua mgongo wa simu unaonekana kana madoa ya sabuni ya unga.

Cover zinasababisha joto na kuongeza uzito wa simu,

Cover hazizuii kioo kupasuka,wapo wenye cover na simu ina crack kama zote.

Cover inasababisha usiuze sura[emoji3][emoji3],wenye infinix na samsung galaxy mnakuwa na muonekano sawa.

Usipotumia cover ukiweka simu mfukoni inajisafisha yenyewe,ukitoa inakuwa smart kabisa.

Kama kazi yako ni mazingira machafu iweke pembeni sehemu laini ili usichubue mgongo.

Mimi simu natumia mpaka miaka mitatu na isidondoke hata mara moja,simu zangu zinapasuka crack baada ya kuichoka miaka mitatu hivi nakuwa careless.
 
Mimi kwa uzoefu wangu wa kuweka kava kwenye zimu zangu zilizopita nimegundua yafuatayo.

Cover zinatunza vumbi na uchafu hasa kwenye kingo za simu.

Cover zikiingia mchanga mdogo mdogo unasagwa baina ya mgongo wa simu na cover hali inayosababisha michubuko kwenye mgongo wa simu ( back)

Baadhi ya cover zinababua mgongo wa simu unaonekana kana madoa ya sabuni ya unga.

Cover zinasababisha joto na kuongeza uzito wa simu,

Cover hazizuii kioo kupasuka,wapo wenye cover na simu ina crack kama zote.

Cover inasababisha usiuze sura[emoji3][emoji3],wenye infinix na samsung galaxy mnakuwa na muonekano sawa.

Usipotumia cover ukiweka simu mfukoni inajisafisha yenyewe,ukitoa inakuwa smart kabisa.

Kama kazi yako ni mazingira machafu iweke pembeni sehemu laini ili usichubue mgongo.

Mimi simu natumia mpaka miaka mitatu na isidondoke hata mara moja,simu zangu zinapasuka crack baada ya kuichoka miaka mitatu hivi nakuwa careless.
Ni kweli kabis kava zinaweza fanya simu ikaoza na fangas kabisa. Umeeleza vema kuna vumbi zikiingia ndani ya kava zinachubua mgongo mimi nilishangaa mbona naweka kava alafu simu inachubuka? Siweki kava sikuizi, simu ya million+ kava elfu10?
 
Back
Top Bottom