Ukiwafurahisha dakika 5 watakushangilia kama vile umepatia mwaka mzima, ukuikosea kidogo tu watasahau na kukugeuka papo hapo

Ukiwafurahisha dakika 5 watakushangilia kama vile umepatia mwaka mzima, ukuikosea kidogo tu watasahau na kukugeuka papo hapo

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kwa sasa sio ajabu kumsikia Shabiki anamtolea maneno yasiyo na staha Mchezaji kwa vile tu hajaridhishwa na alivyocheza mechi kadhaa zilizopita wakakosa matokeo chanya.

Kwa mfano Mtu atasahau kabisa kuwa Boko ndiye alichangia zaidi ya nusu ya magoli yaliyopelekea timu yao kuwa Mabingwa wa nchi na hata kung'ara kimataifa.

Mpira ni Magoli, na kama mnakuwa na Mchezaji anayeweza kufunga muda wowote na amewahi kudhihirisha hivyo kwa msimu uliopita ni kwa vipi tena kukosa subira kwake?

Kwa sasa Simba wanamfurahia Ajib, si vibaya na hongera kwake kwa kuzikonga nyoyo ya Mashabiki kwenye mechi iliyopita, lakini tusimvimbishe kichwa akapotea au kumpa mzigo wa presha akashindwa kuhimili na vile vile tusiwasahau wenzake waliopo kwenye timu, maana timu ni timu, yaani timu ni Wachezaji wote 11.

Usimtukane Mchezaji mmoja ukamsifia sana mmoja tukasahau wao wote ndio wanaounda timu.
 
Tatizo makosa yale yale kila mechi halafu anachezeshwa karibia dk 70-80 kwenye mechi
 
Ajibu ataanza mechi ijayo ya Simba sifa zake zitaishia hapo kwani simba itasuluhu/kufungwa Ajibu atakosa magoli ya wazi mashabiki hawatomtaka tena...
 
Ajibu ataanza mechi ijayo ya Simba sifa zake zitaishia hapo kwani simba itasuluhu/kufungwa Ajibu atakosa magoli ya wazi mashabiki hawatomtaka tena...
Hivi mkuu kwa akili zako Ajib ni mchezaji wa kukosa magoli ya waziii? Yule ni fundi wa mpira endapo akianza tu wapinzaniii wa simba wa hesabu maumivuu (Chama kazaliwa upya msimbazii)
 
Hivi mkuu kwa akili zako Ajib ni mchezaji wa kukosa magoli ya waziii? Yule ni fundi wa mpira endapo akianza tu wapinzaniii wa simba wa hesabu maumivuu (Chama kazaliwa upya msimbazii)
Asingeozea benchi mkuu,tusubiri tu tuone kama hili tumaini lenu jipya litawapa mnachotaka,mnampa Ajibu presha kubwa kipindi hiki ambacho timu yenu haipo vizuri eti yeye ndo aje kuibeba timu baada ya msoto mkali wa benchi

Unadhani akishindwa mtamuweka kwenye kundi gani kama sio lile la kumtukana na kumuona hawafai.
 
Hivi mkuu kwa akili zako Ajib ni mchezaji wa kukosa magoli ya waziii? Yule ni fundi wa mpira endapo akianza tu wapinzaniii wa simba wa hesabu maumivuu (Chama kazaliwa upya msimbazii)
aliskika mlevi mmoja
sokomoko.jpg
 
Ajibu ataanza mechi ijayo ya Simba sifa zake zitaishia hapo kwani simba itasuluhu/kufungwa Ajibu atakosa magoli ya wazi mashabiki hawatomtaka tena...
Na hapo ndio ataijua chungu na tamu ya Mashabiki.

Kikubwa kwake asilewe sifa na abaki yeye kama yeye...na yale anayotuhumiwa kwayo basi naye ajirekebishe.

Kipaji ni jambo moja, lakini ni lazima kitunzwe na si kutegemea kelele za Mashabiki.

Mfano Mtu kama Haruna Moshi Boban sidhani kama kuna Mtu ana shaka na kipaji chake...lakini mtindo wa maisha yake ulikuwa hausapoti kabisa mzigo wa kipaji alichojaaliwa...matokeo yake wote tume/tunayashuhudia.

Dhamana yake aibebe mwenyewe asiwafuate Mashabiki.
 
Hivi mkuu kwa akili zako Ajib ni mchezaji wa kukosa magoli ya waziii? Yule ni fundi wa mpira endapo akianza tu wapinzaniii wa simba wa hesabu maumivuu (Chama kazaliwa upya msimbazii)
Tusizidishe sifa tukampoteza Mchezaji.

Na pia tumpe Chama heshima yake....Kama Ajib anao huo uwezo ni jambo jema na aelezwe wazi ya kuwa kuna gharama za kuwa anavyotamani kuwa na haitotokea kama Mtoto na titi la Mama yake.

Hizi kelele tungezitumia kwenye kumuhimiza kuongeza bidii badala ya kumdanganya na kumpoteza kabisa.
 
Hivi mkuu kwa akili zako Ajib ni mchezaji wa kukosa magoli ya waziii? Yule ni fundi wa mpira endapo akianza tu wapinzaniii wa simba wa hesabu maumivuu (Chama kazaliwa upya msimbazii)
Huyu Ajib ni usajili mpya au alikuwepo Simba tokea misimu ya nyuma?
Kipi kilimfanya akae benchi kama ni mchezaji wa kiwango kikubwa?
 
Na hapo ndio ataijua chungu ya mashabiki.

Kikubwa kwake asilewe sifa na abaki yeye kama yeye...na yale anayotuhumiwa kwayo basi naye ajirekebishe.

Kipaji ni jambo moja, lakini ni lazima kitunzwe na si kutegemea kelele za Mashabiki.

Mfano Mtu kama Haruna Moshi Boban sidhani kama kuna Mtu ana shaka na kipaji chake...lakini mtindo wa maisha yake ulikuwa hausapoti kabisa mzigo wa kipaji alichojaaliwa...matokeo yake wote tume/tunayashuhudia.

Dhamana yake aibebe mwenyewe asiwafute Mashabiki.
Point...
 
Huyu Ajib ni usajili mpya au alikuwepo Simba tokea misimu ya nyuma?
Kipi kilimfanya akae benchi kama ni mchezaji wa kiwango kikubwa?
Kukaa benchi kwa Ajib kulichangiwa zaidi na makocha kushindwa kumuelewa, makocha wengi wa kizungu walisimamia weledi wa kazi yao wakitaka Ajib ajitume mazoezinii ili apate namba kitu ambacho Ajib Migomba (Fundi wa mpira) wala hafagilii yeye ni mtu wa kuonyesha tu uwezo wake kila anapopata nafasii kucheza sio mazoezi
Ukitaka Ajib ajitume basi ujue hata simba asingekuwepo maana si mchezaji wa kucheza Afrika hii
Nadhani Hitimana na Matola imani yao waliyoiweka kwa Ajib inaenda kuwalipa na simba ipo miikono salama tena baada ya chama kuondoka

NB: Weledi sio kila kitu wakati mwengne na kujituma mazoezini si lazima kwa mchezaji mwenye kipaji kikubwa na cha asili kama Ajib ule ni mpira sio kunyanyua vitu vizito
 
Tusizidishe sifa tukampoteza Mchezaji.

Na pia tumpe Chama heshima yake....Kama Ajib anao huo uwezo ni jambo jema na aelezwe wazi ya kuwa kuna gharama za kuwa anavyotamani kuwa na haitotokea kama Mtoto na titi la Mama yake.

Hizi kelele tungezitumia kwenye kumuhimiza kuongeza bidii badala ya kumdanganya na kumpoteza kabisa.
Hebu fikiria kidogo kabla ya mechi ya Namungo juzi Mara ya mwisho kumuona Ajib anacheza ni lini? Lakini alivyoingia juzi ndani ya dk 20 tu alionyesha ni mchezaji wa class gani
Ajib ni moja ya kipaji kikubwa cha soka kuwahi kutokea Tanzania imagine ndio mnasema hajitumi na anaonyesha ubora ule Je angekuwa anajituma sasa kama Nchimbi au Mzamiru ingekuwaje??
 
Back
Top Bottom