Ukiyafahamu maisha ya wanavyuo kwenye vyuo vya Elimu ya Juu nchini, hutawalaumu wanaowabeza wasomi wa Kitanzania

Ukiyafahamu maisha ya wanavyuo kwenye vyuo vya Elimu ya Juu nchini, hutawalaumu wanaowabeza wasomi wa Kitanzania

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Joseph Kasheku Msukuma na Jumanne Kishimba "hawajashule" kiviile, lakini si wajinga. Ni miongoni mwa wanasiasa wanaoongoza kwa kuwabeza wasomi wa Kitanzania.

Kuna baadhi ya watu wameonesha kukasirishwa na kejeli za hao wanasiasa, lakini ukifuatilia kwa makini, utabaini mengi ya madai yao yana mashiko.

Hata msomi makini, CAG mstaafu, Profesa Musa Assad, alishawahi kusema kuwa asilimia sitini ya watumishi wa Serikali hawana uwezo. Serikali ililipinga hilo vikali, lakini madudu ya watumishi wake yameendelea kuiumbua.

Nimeliona sekeseke linaloendeshwa na Makonda mkoani Arusha. Watumishi wengi wanaonekana wanapwaya sana kwenye nafasi zao. Naweza kusema "hawajielewi"

Lakini kwa nini iwe hivyo? Hayo yameanzia mbali. Ni tokea wakiwa vyuoni. Wengi hawakuwa "serious" na masomo, bali kulitumbua bumu walilopewa na Serikali. Labda wa siku hizi wako makini, pengine.

Kipindi nikiwa Chuoni, nilishuhudia jinsi wengi wa wanavyuo walivyokuwa wakiendekeza maisha ya anasa. Kidogo waliokuwa wakijitahidi ni wa shahada za udaktari, ualimu, "Engineering", n.k. Lakini wengi wa waliosalia, hasa wa vitivo vya Sanaa, walikuwa ni watu wa starehe sana (japo si wote).

Weekend ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu ili waende kwenye kumbi za starehe. Kesho yake utasikia wengine wakijisifia kuwa siku iliyopita walikuwa club moja na Mbunge fulani n.k.

Sasa kama hao ndio wasomi wenyewe, wanatarajiwa kuwa na lipi jipya wakati hawakujiandaa ipasavyo kwa majukumu hayo?

Kishimba aliposema kuwa asilimia tisini ya wasomi wa Tanzania wanajua tu kusoma na kuandika hakukosea.

Wasomi nchi hii ni wachache sana kuliko takwimu zinavyoonesha. Wengi wa walio na vyeti si wasomi ilhali kuna wasomi wasiokuwa na vyeti.

Miongoni mwa hao watu ambao ni wasomi japo hawana vyeti ni Jumanne Kishimba.

Sijui kwanini hawampi "uprofesa" wa heshima😀
 
Mfumo wa kusoma ni win to win , elimu ya bongo ni uwekezaji sio maarifa ...Yaani ukiwa na pesa mwanao atafika unapotaka kwa njia yoyote ile.

Watu wanasoma kwa magumashi ila wanachukua GPA nzuri ndio pale shule ya sheria wanangukia mbavu .
 
Bomu Kali na kubwa linakuja kizazi hiki cha chatGPT wakiingia mtaani, wanafunzi vilaza sijaona, lakini GPA zinasoma kubwa maarifa zero.
ChatGPT inahusika vipi hapo. Yaani unahusisha moja ya revolutionary powerful artificial intelligence technology with free and easy access na ujinga wa wasomi wa Kitanzania?

Sijakuelewa!
 
Kusoma na kuwa na akili ya udadisi, kuchanganua na kutatua ni vitu viwili tofauti. Sababu hicho cha pili ni kitu natural kwa kila mtu husika, na kusoma ni njia tu ya kuboost hicho kipawa. Na asilimia kubwa ya watanzania hawana hicho kipawa. Ukilinganisha wengi wao hutumia elimu kama njia tu ya kujikomboa na shida za maisha. Na sio sababu wana nia ya kuboost kipawa chao. Na njia mojawapo ya kueliminate wasomi njaa ni kutatua changamoto za ugumu wa maisha kwa wananchi. Ili hao wenye vipawa waongezeke.

Honestly, hilo tatizo la wasomi uchwara na viongozi njaa sio Tanzania tu. Bali karibu dunia nzima. Na njia makini pekee ni hao wachache wenye vipawa kutengeneza mifumo mikali na makini ili kueliminate hilo tatizo.
 
ChatGPT inahusika vipi hapo. Yaani unahusisha moja ya revolutionary powerful artificial intelligence technology with free and easy access na ujinga wa wasomi wa Kitanzania?

Sijakuelewa!
ChatGPT inahusika vipi hapo. Yaani unahusisha moja ya revolutionary powerful artificial intelligence technology with free and easy access na ujinga wa wasomi wa Kitanzania?

Sijakuelewa!
Kwanza tukubaliane sehemu kubwa Ujinga unaanzia shule na tueleze ujinga kama upungufu wa maarifa..
Sasa mfano wa hawa watu wawili..10 or more yrz back then students assignment au kazi yoyote ya shule ilikuwa ikitolewa ni lazima utasoma kitabu physical au hata kama ni online utapitia articles kisha utaandaa summary na kuandika kile ulichojifunza.
Kazi uliyokuwa unasoma library na kufanya siku kadhaa kuandaa paper sasa hivi mwanafunzi swali anaplug kwenye ChatGPT tena kwenye simu kazi inafanyika ndani ya dk 1, anacopy nakupaste kazi ambayo hata hajui humo ndani imeandikwa kitu gani ila anapata marks 10 over 10 ila kichwani mweupe hana maarifa yoyote.
Hatari nayoizungumzia ndiyo hiyo wasomi wengi wakitanzania sijui itakuaje mana ni weupe,
 
Mfumo wa kusoma ni win to win , elimu ya bongo ni uwekezaji sio maarifa ...Yaani ukiwa na pesa mwanao atafika unapotaka kwa njia yoyote ile.

Watu wanasoma kwa magumashi ila wanachukua GPA nzuri ndio pale shule ya sheria wanangukia mbavu .
Mtu akiwa na hela anaweza hata kununua masters degree wakati kuandika tu barua ya kiofisi/kikazi hajui.
 
HAPO hapo unamsifia Kishimba emu tuwekee CV yake
Inasemekana ni darasa la nane la zamani ila ana akili ya kutafuta hela. Ndiyo maana kapendekeza somo la kutafuta hela lianze kugundishwa tokea madarasa ya chini.

Ukimsikiliza utafahamu kuwa ni mwelewa sana. Wasomi wengi wanamkubali.
 
Back
Top Bottom