Ukoloni unarudi Tanzania?

Ukoloni unarudi Tanzania?

Na Thadei Ole Mushi

Miaka 60 ya Uhuru tumeshindwa kabisa kusimamia rasilimali zetu wenyewe.

Migodi tumeitoa kwa Wazungu, Misitu tumeitoa kwa Mwarabu, Posta tumeitoa kwa Mwarabu, Misitu tumeitoa kwa mwarabu, Gesi tumeitoa kwa Mzungu, Uwanja wa ndege wa KIA nao tumeutoa, TPDC tumeitoa, Bandari tumeitoa kwa mwarabu, Loliondo tumeitoa kwa Mwarabu, karibi maeneo yote Muhimu tumeshatoa…. Sisi tumebakia na nini?

Maswali ni Mengi mno….

1. Tulidai Uhuru wa Nini?

2. CCM imeshindwa kuiongoza Nchi? Maana kila eneo tuliloliwekeza tunasema kuna wapigaji hivyo bora tumpe mwekezaji. Je Serikali ni dhaifu imeshindwa kuzuia upigaji?

3. Vyuo Vikuu zaidi ya 31 nchini vimeshindwa kutengeneza wasomi wa kusimamia hizi rasilimali za taifa? Kazi za Graduate wetu kubwa ni kuendesha Bodaboda, kama taifa tunajua tunakoelekea?

4. Tanzania tunaweza jambo gani kubwa hapa nchini? Mambo yote ya muhimu tunaona ni Magumu tunawapa wawekezaji je sisi ni kitu gani tunaweza? Wenzetu wanawezaje sisi tunashindwa? Huu uvivu wa kufikiri tumeutoa wapi?

5. Baada ya Bandari tunaenda kuwekeza rasilimali gani tena? Ukiona wabunge wetu wanavyovaa Suti Pale Bungeni na taifa linapoelekea utatamani kulia. Hawa watu (wabunge) tunawalipa mishahara, tunawanunulia mafuta ya magari, watoto wao tunawasomesha na bado wanatuibia kupitia mikataba hivi nani alituloga tukawa waoga hivi?

6. Tanzania ya watu Milioni 69 plus tumeshindwa kuchaguana miongoni mwetu tupate watu wanaoweza kutuvusha hapa tulipo kwa kuwa taifa linaelekea kutawaliwa kwa mara ya Pili?

7. Wakati Uganda ilipogundua kuwa ni kweli Taifa lao lina mafuta walichukua vijana wao wakakimbiziwa ughaibuni kwenda kujifunza kuhusu Oil Production na asilimia kubwa ya mradi wao wa mafuta ni vijana wanausimamia. Sisi badala ya kuandaa vijana tunatuma kina Steve Nyerere na kina Kitenge kwenda kukagua Bandari za wenzetu hivi nani alituloga?

8. Vijana asilimia 90 sasa hivi hapa nchini bila kujali elimu zao kazi zao kubwa za kujipatia kipato ni Kubet au kuendesha Bodaboda. Huku maeneo muhimu ya rasilimali za taifa lao zikigawanywa kwa wazungu na waarabu kwa jina la kusema ni mwekezaji. Hii ni hatari sana kwa taifa letu…. Tanzania ina wanyamapori kila mahali ila anayekula nyama pori first class kabisa hapa Tanzania ni Mwarabu hii ni aibu…

9. Je tuliwahi kupata Uhuru? Lakini mbona Kina Singapore walipata Uhuru nyuma yetu? Mbona leo ipo mbali sana na wanajisimamia wenyewe?

10. Hata kuzalisha mafuta ya kula ya kutosha kwa taifa zima tumeshindwa tunaagiza nje ya nchi, Ngano tunaagiza, Mbolea tunaagiza, Maziwa ya Unga na hata ya kawaidia tunaagiza, pale Bandarini asilimia 95 ni bidhaa zinaingia nchini badala ya kutoka hivi tunaelekea wapi?

CCM ikubali sasa kutumia watu ambao wapo nje ya familia zenye Connection kwenye Uongozi wa nchi hii. Babu alikuwa kiongozi, mtoto akatafutiwa connection akawa kiongozi, mjukuu naye akawa kiongozi nk …. Hizi DNA kwa mazingira ya Sasa zimechoka au CCM ikubali kuwaachia wengine wajaribu kutusogeza tulipo.

Kuna siku nilisema kama Africa itaheshimu Sanduku la Kura katika kuchaguana tutafika mbali sana. Na kama askari polisi wa Mataifa ya Africa watatimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria hili bara linapiga hatua kubwa. Askari anamlinda mtu mwenye V8, Mke ana gari, watoto wa huyo Mtu wanachukuliwa na School Bus wanakupita getini unawachekelea kama Zuzu, huku kwako ukiwa unafukuzana na Baba Mwenye nyumba anakudai kodi, kijana wako wa kwanza aliyehitimu Chuo kikuu anashinda vibanda umiza anabet, wanao wanasoma shule za makabwela kabisa huku akiwa hana uniform za kubadilisha lakini bado unaendelea kupiga Salute kwenye mageti ya viongozi.

Vijana kwa Rasilimali zilizopo hapa nchini hampaswi kukesha mkiwa mna Bet na kuendesha Boda boda. Wafanyakazi kwa rasilimali zilizopo Hampaswi kulipwa mishahara mnayolipwa. Hivyo basi watu kama kina Steve Nyerere na kina Maulid Kitenge ni wa kuwatenga kwenye jamii yetu…. Tunatakiwa tuanze kutokomeza hizi chawa kwanza kabla hatujawafikia Viongozi wetu.

Wakati ukoloni ukibisha Hodi Africa ulikuja kwa njia ya Mikataba. Ndiko tunakoelekea…..

Vijana tuliopo ndani ya CCM ni wakati wa kujitafuta sasa tuache kusifia ujinga wakati taifa limekwama. Tuzungumze, tukatae kabisa kuwa Chawa wa mtu, wakati ni sasa….. kila mtu kwenye familia yake atoe elimu ya Uraia.

Tumekwama kama Taifa….. share

Ole Mushi
0712702602
we tapeli huna unachojua, kwanza ole Mushi ndio jina gani.
 
Ndoto ya mchana ccm kuwatoa kwa njia ya ballot.
Sijawahi kukata tamaa na njia ya ballot. 2014-2015 ilibidi wapige magoti haswa....

2024-2025 hata wakitoa machozi ya kenge jibu liwe hapana[X] kuwaondoa hawa waliopo madarakani inawezekana kabisa.

CCM can be revived and cleaned Inside out. Believe me.
 
Tuchague lakini upinzani!
Haswa, ikiwa tunaweza lete upinzani ndani kuja nje, vilevile kuungana na wote wapenda NCHI. Hakika muungano wetu(sio 64) unaweza kuleta mabadiliko makubwa Nchini.

CCM hii hii inaweza kurudi, minus madubwana na madubwasha yaliyomo.
 
Sijawahi kukata tamaa na njia ya ballot. 2014-2015 ilibidi wapige magoti haswa....

2024-2025 hata wakitoa machozi ya kenge jibu liwe hapana[X] kuwaondoa hawa waliopo madarakani inawezekana kabisa.

CCM can be revived and cleaned Inside out. Believe me.
Sijakubishia mkuu ila sio kwanjia ya ballot amini nachokuambia hawa wanatakiwa kuwatoa kwanjia ya maandamano nchi mzima na kumuwela Lisu pale ikulu.
 
Kuna ukweli mahali. Ndio maana ule usemi kuwa saa mbovu kuna wakati inasema kweli.
Tulitafuta uhuru wa nini kama kwa uhuru huo tunawapa tena wakoloni rasilimali zetu?
Au tulitafuta uhuru ili kuwa na mawaziri na wabunge tuu wakitembea na magari yenye bendera?
Hawa Kenge si ndio machawa wa Makonda waeneza propaganda eti Makonda kateuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa Ccm badala ya Sofia Mjema.

Kuna watu akiwemo huyu mpuuzi Ole Mushi wamemisi kunywa damu za watu sasa wameanzisha propaganda kubwa kumpigia debe yule shetani Bashite.
 
WANACCM WOTE KWA UJUMLA WETU TUNAUNGA MKONO SUALA LA UWEKEZAJI WA DP WORLD TANZANIA,MTUNZI WA ARTICLE HII, JISEMEE KWA NAFSI YAKO!
KIGOGO WA CCM NA SERIKALI ATOA MAONI JUU YA MKATABA WA BANDARI KUPITIA KWA ASKOFU ILI ASIFUKUZWE UANACHAMA!

Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Kwenye vikao vilivyoisha (Kamati Kuu ya CCM na Halmashauru Kuu ya CCM) imeelezwa kuwa Wajumbe wamebariki mkataba tata wa Bandari. Ninajiuliza maswali kadhaa: Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao hivyo ni wanasheria au wachumi walioweza kuingia katika vikao na nakala ya mkataba na kuanza kujenga hoja ya kujadili kifungu kwa kifungu kuwa kifungu hiki hakiko sawa na hiki kiko sawa?

Je, Mwenyekiti wa kikao alitangaza maslahi yake katika jambo husika kuona busara kuwa jambo hilo lijadiliwa kwa uwazi bila yeye kuwa Mwenyekiti wa kikao kwa kuwa limepigiwa kelele sana na hivyo kujenga neutrality kwake? Je, isingekuwa ni busara kumuachia Makamu Mwenyekiti ili asimamie vikao husika?

Mpendwa Baba Askofu! Unajua kwenye Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ili mtu aweze kuingia katika Political Committee ama Kamati ya Siasa na ngazi zingine kubwa za maamuzi ni lazima awe na uelewa wa mambo hususani katika masuala ya fedha, sheria, mazingira na pia lazima awe na elimu au uwezo wa kuweza kujenga hoja.

Je ni Wajumbe wangapi katika vikao vyetu ambao ni wanasheria na wachumi walio na uwezo wa kujenga hoja katika vikao ambavyo tumeambiwa kuwa wameridhia kwa kishindo?

Ninaomba ikikupendeza Baba Askofu unisaidie kuyafikisha haya kwa Watanzania kwani sio wote ndani ya CCM tunaounga mkono mkataba huo wa Bandari. Mazingira yetu ni magumu na hivyo tunaogopa kufukuzwa uanachama ndio maana hatutoki hadharani kupinga au kukosoa.

Ndimi .....
Dar es Salaam, 10 Julai 2023
 
Posta imetolewa Kwa mwarabu?
Ushirikiano nao ni kutoa?
Kwahiyo nchi zote tunazo shirikiana ni tunawapa?...
Akili za wapi hizi?
At what percentage ukitoa more than 50% wewe sio tena unayeshirikisha bali unashirikishwa... (na kama kama asset ilikuwa yako in the beginning - hio ni another definition ya kupigwa) Na upigaji huu unatokea sio kwamba wanaoingia mikataba hawajui bali wanajali 10% zao kuliko long term welfare ya Nchi zao)

Solution ni Transparency tu..., tujue ni nini wanafanya hawa walinzi wa mali zetu waliogeuka kuwa walafi wa mali zetu (Ni kama kumpa ngedere akulindie shamba la mahindi alafu wewe mkulima usiruhusiwe kuangalia kinachoendelea)
 
Bora ya wakoloni wa awali kuliko ccm na wakoloni wa Sasa kama wawekezaji
 
Na Thadei Ole Mushi

Miaka 60 ya Uhuru tumeshindwa kabisa kusimamia rasilimali zetu wenyewe.

Migodi tumeitoa kwa Wazungu, Misitu tumeitoa kwa Mwarabu, Posta tumeitoa kwa Mwarabu, Misitu tumeitoa kwa mwarabu, Gesi tumeitoa kwa Mzungu, Uwanja wa ndege wa KIA nao tumeutoa, TPDC tumeitoa, Bandari tumeitoa kwa mwarabu, Loliondo tumeitoa kwa Mwarabu, karibi maeneo yote Muhimu tumeshatoa…. Sisi tumebakia na nini?

Maswali ni Mengi mno….

1. Tulidai Uhuru wa Nini?

2. CCM imeshindwa kuiongoza Nchi? Maana kila eneo tuliloliwekeza tunasema kuna wapigaji hivyo bora tumpe mwekezaji. Je Serikali ni dhaifu imeshindwa kuzuia upigaji?

3. Vyuo Vikuu zaidi ya 31 nchini vimeshindwa kutengeneza wasomi wa kusimamia hizi rasilimali za taifa? Kazi za Graduate wetu kubwa ni kuendesha Bodaboda, kama taifa tunajua tunakoelekea?

4. Tanzania tunaweza jambo gani kubwa hapa nchini? Mambo yote ya muhimu tunaona ni Magumu tunawapa wawekezaji je sisi ni kitu gani tunaweza? Wenzetu wanawezaje sisi tunashindwa? Huu uvivu wa kufikiri tumeutoa wapi?

5. Baada ya Bandari tunaenda kuwekeza rasilimali gani tena? Ukiona wabunge wetu wanavyovaa Suti Pale Bungeni na taifa linapoelekea utatamani kulia. Hawa watu (wabunge) tunawalipa mishahara, tunawanunulia mafuta ya magari, watoto wao tunawasomesha na bado wanatuibia kupitia mikataba hivi nani alituloga tukawa waoga hivi?

6. Tanzania ya watu Milioni 69 plus tumeshindwa kuchaguana miongoni mwetu tupate watu wanaoweza kutuvusha hapa tulipo kwa kuwa taifa linaelekea kutawaliwa kwa mara ya Pili?

7. Wakati Uganda ilipogundua kuwa ni kweli Taifa lao lina mafuta walichukua vijana wao wakakimbiziwa ughaibuni kwenda kujifunza kuhusu Oil Production na asilimia kubwa ya mradi wao wa mafuta ni vijana wanausimamia. Sisi badala ya kuandaa vijana tunatuma kina Steve Nyerere na kina Kitenge kwenda kukagua Bandari za wenzetu hivi nani alituloga?

8. Vijana asilimia 90 sasa hivi hapa nchini bila kujali elimu zao kazi zao kubwa za kujipatia kipato ni Kubet au kuendesha Bodaboda. Huku maeneo muhimu ya rasilimali za taifa lao zikigawanywa kwa wazungu na waarabu kwa jina la kusema ni mwekezaji. Hii ni hatari sana kwa taifa letu…. Tanzania ina wanyamapori kila mahali ila anayekula nyama pori first class kabisa hapa Tanzania ni Mwarabu hii ni aibu…

9. Je tuliwahi kupata Uhuru? Lakini mbona Kina Singapore walipata Uhuru nyuma yetu? Mbona leo ipo mbali sana na wanajisimamia wenyewe?

10. Hata kuzalisha mafuta ya kula ya kutosha kwa taifa zima tumeshindwa tunaagiza nje ya nchi, Ngano tunaagiza, Mbolea tunaagiza, Maziwa ya Unga na hata ya kawaidia tunaagiza, pale Bandarini asilimia 95 ni bidhaa zinaingia nchini badala ya kutoka hivi tunaelekea wapi?

CCM ikubali sasa kutumia watu ambao wapo nje ya familia zenye Connection kwenye Uongozi wa nchi hii. Babu alikuwa kiongozi, mtoto akatafutiwa connection akawa kiongozi, mjukuu naye akawa kiongozi nk …. Hizi DNA kwa mazingira ya Sasa zimechoka au CCM ikubali kuwaachia wengine wajaribu kutusogeza tulipo.

Kuna siku nilisema kama Africa itaheshimu Sanduku la Kura katika kuchaguana tutafika mbali sana. Na kama askari polisi wa Mataifa ya Africa watatimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria hili bara linapiga hatua kubwa. Askari anamlinda mtu mwenye V8, Mke ana gari, watoto wa huyo Mtu wanachukuliwa na School Bus wanakupita getini unawachekelea kama Zuzu, huku kwako ukiwa unafukuzana na Baba Mwenye nyumba anakudai kodi, kijana wako wa kwanza aliyehitimu Chuo kikuu anashinda vibanda umiza anabet, wanao wanasoma shule za makabwela kabisa huku akiwa hana uniform za kubadilisha lakini bado unaendelea kupiga Salute kwenye mageti ya viongozi.

Vijana kwa Rasilimali zilizopo hapa nchini hampaswi kukesha mkiwa mna Bet na kuendesha Boda boda. Wafanyakazi kwa rasilimali zilizopo Hampaswi kulipwa mishahara mnayolipwa. Hivyo basi watu kama kina Steve Nyerere na kina Maulid Kitenge ni wa kuwatenga kwenye jamii yetu…. Tunatakiwa tuanze kutokomeza hizi chawa kwanza kabla hatujawafikia Viongozi wetu.

Wakati ukoloni ukibisha Hodi Africa ulikuja kwa njia ya Mikataba. Ndiko tunakoelekea…..

Vijana tuliopo ndani ya CCM ni wakati wa kujitafuta sasa tuache kusifia ujinga wakati taifa limekwama. Tuzungumze, tukatae kabisa kuwa Chawa wa mtu, wakati ni sasa….. kila mtu kwenye familia yake atoe elimu ya Uraia.

Tumekwama kama Taifa….. share

Ole Mushi
0712702602
Hata tukawachagua CHADEMA ni hayo hayo tu. Kitachofanyika ni kuwatoa hao uliowataja na kuwaleta Wabelgiji. Hatuna ujanja, tumebanwa vizuri.
69 milioni, yes tumeshindwa kuchaguana. Alternative tulizonazo ni Dr Slaa (Muongo mkubwa), Lissu (mropokaji, kichwa maji + Mbelgiji). Hatuna pakukimbilia ndugu yangu.
 
Hata tukawachagua CHADEMA ni hayo hayo tu. Kitachofanyika ni kuwatoa hao uliowataja na kuwaleta Wabelgiji. Hatuna ujanja, tumebanwa vizuri.
69 milioni, yes tumeshindwa kuchaguana. Alternative tulizonazo ni Dr Slaa (Muongo mkubwa), Lissu (mropokaji, kichwa maji + Mbelgiji). Hatuna pakukimbilia ndugu yangu.
Kwa hiyo umekubali hata mwarabu akiamua kukulamba utakubali tuu kwa vile huna pa kukimbilia?
Unajitangazia unyonge bila aibu?
 
Kwa hiyo umekubali hata mwarabu akiamua kukulamba utakubali tuu kwa vile huna pa kukimbilia?
Unajitangazia unyonge bila aibu?
Rafiki yangu neno kutawaliwa kwa maana hii nyie mnayeitoa, haipo nchi afrika iliyokuwa na uhuru huo unaoufikiria.
Sasa hivi nyie mnapiga kelele huku mkimuunga Dr Slaa na Lissu bila kujua kuwa kwa kuwaunga mkono hao mnawakaribisha Wabelgiji/ Magu alikuwa anawaita mabwana zao. Napenda kurudia, ninapenda mjue mnachofanya, msije mkaanza harakati nyingine kwa kutokujua mkifanyacho sasa hivi.
 
Mbona posta inashirikiana na Makampuni mengi Tu ya Ulaya?
Nashauri punguza islamophobia na stereo types ...

Ushirikiano siku zote unaamua wewe kipi ushiriki kipi ukatae...sio mkataba wa kununua wala kukodisha...
Samahani mkuu
Unaundugu na @feizafox?
Maana wote hamna hoja zaidi ya udini
 
Rafiki yangu neno kutawaliwa kwa maana hii nyie mnayeitoa, haipo nchi afrika iliyokuwa na uhuru huo unaoufikiria.
Sasa hivi nyie mnapiga kelele huku mkimuunga Dr Slaa na Lissu bila kujua kuwa kwa kuwaunga mkono hao mnawakaribisha Wabelgiji/ Magu alikuwa anawaita mabwana zao. Napenda kurudia, ninapenda mjue mnachofanya, msije mkaanza harakati nyingine kwa kutokujua mkifanyacho sasa hivi.
Sijui kama hats unachoandika hapa we mwenyewe unakielewa!
Anyway, tutafika tuu
 
Sijui kama hats unachoandika hapa we mwenyewe unakielewa!
Anyway, tutafika tuu
Na hiyo anyway....... ndicho nilichokuwa namaanisha. Ni kweli tutaelewana tu na tutafika tuu. Nisiandike mengi, jibu lako linatosha.
 
Back
Top Bottom