when was the last time you visited postnatal clinic??
tuliobahatikaga kufundishwa ni wale tuliozaa enzi za nepi na mafuta ya nazi, siku hizi za pampers na baby oil ukishapima uzito subiri miez sita ipite ili ukaribishwe kwenye dawati la kupanga uzazi.
kwakweli disposable diapers kwa sehem za baridi kuwafunga sio jambo baya ila sasa kama sio mwangalifu chances za kupata uti ni kubwa sana.sijapitwa sana hata mimi natumia mafuta ya nazi tena ya kutengeneza mwenyewe mpendwa..naomba niulize ni sawa kama nikiwafunga pampers kwa umri huu? maana arusha ni mvua daily nep hazikauki sasa naogopa kuwafunga pampers..hebu nambie mpenz niwafunge tu ama badobado?
kwakweli disposable diapers kwa sehem za baridi kuwafunga sio jambo baya ila sasa kama sio mwangalifu chances za kupata uti ni kubwa sana.
hakikisha hawakai nazo hadi zikajaa sana na pia hata kama huwez kuwatia maji mara kwa mara lkn kuwa futa matakoni kwa kitambaa chenye maji ya uvuguvugu na kupaka mafuta ni muhimu kila unapowabadili.
sijui kwann siamini sana baby wipes lkn kama unaweza kuziamini basi tumia ila maji muhimu kuwatia mumie.
ningekuwa mimi wewe ningehakikisha nakuwa na nenpi nyingi zaidi manake ukweli ni kwamba kila mtoto akijisaidia kwenye nepi lazima utambadili tu tena utamfuta kwa maji na kumpaka mafuta. na hapa lazima ningekuwa nakuwa wa mwisho kuingia kitandani na wa kwanza kuamka manake masharti ya nepi zisilale chafu bila kulowekwa. sasa ubaya wake ni kwamba housegirl hatakaa ataona unamfanyisha kazi nyingi zaidi.
mwisho wa siku tafuta aina ya maisha ambayo ni simple na yatakayokupa furaha ya kulea wanao, ukicomplicate sana utaona tabu ya malezi, na ukiwa too hard utaota kibiongo
Kwa sisi watu wa FIQHI hiyo damu tunaita ni NIFASI,
Uchache wake ni siku moja na wingi wake ni siku 40 hadi 60. Ikizidi hapo hiyo tunaita ISTIHADHA(ni ya ugonjwa) .
sijapitwa sana hata mimi natumia mafuta ya nazi tena ya kutengeneza mwenyewe mpendwa..naomba niulize ni sawa kama nikiwafunga pampers kwa umri huu? maana arusha ni mvua daily nep hazikauki sasa naogopa kuwafunga pampers..hebu nambie mpenz niwafunge tu ama badobado?
sio kwamba hatuulizi ndugu.ntunauliza sana mfano.mim niliambiwa ni wiki1/2 sasa nkaona inaendelea na sipo karibu na doctor wala nurse nikaona si mbaya kuuliza kwann niwe na waswas maana naweza.kwenda hosp kwa suala ambalo halikustahili kama hivi..na mim nliogopa nkadhan labda sababu ni hawa mapacha labda..sio kila mtu ni mjuz ndugu wengine ndo tunaanza na kuuliza si ujinga
na sasa hizo baby wipes zimekuwa na contraindication kwa ngozi za watoto wengi sana hasa wale ambao bado hata immunity haijajijenga vizuri......nimeona ambao wamepata skin rushes kwasabbu ya kautumia wengine wanabadilika skin texture..........ukweli naogopa sana vitu ambavyo ni artificial sana kwa mtoto mchanga akikomaa kidogo sawa japo miezi 6 ama 9....mimi huwa naamin bada ya chanjo ya miezi 9 mtoto anakuwa kidogo yuko fiti na mwili unaweza kupambana na lolote ukilinganisha na akiwa na wiki 3 hivi
Uvalishaji wa diaper wahitaji uangalifu kweli usimuache nayo more than 3 hours mie namtumilia 8-10 diapers per day akijisaidia haja kubwa lazima nimuoshe na warm water na mild soap yake then nampakaa vaseline....
Btw twins wako ni wa kike au wa kiume nakuona choyo lol napenda twins jaman
Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
hapo kwenye uzee kweli hujakosea manake kwanza mwenzio sijalea kwa pampers mie, wala wipes nililea kwa kufua nepi toka kiangazi hadi kiangazi na nilianza kufunga nepi baada ya kitovu kukatika manake nilikichunga kama nachunga mbuzi asile maindi ya jirani.........niliambiwa kikimdondokea mbelen hawi tena rijali.Ndo nakuambia unazeeka. Toka day zero diapers zinahusika na wipes. Na siku hizi hakuna kuchunga kitovu kisiangukie baby boy. Kama ni contraindication ni bahati mbaya tu na nadhani hata prevalence ni ndogo
Hii ni wiki ya tatu, sasa si uende kwa dr kama alikuambia ni wiki mbili tu?
tatizo medical science inabadilika sana. Kuna operesheni mie nilifanyiwa 7 yrs ago na dr akaniambia nipumzike 6 weeks. Majuzi kafanyiwa rafiki yangu operesheni ile ile na dr yule yule hospitali ile ile, na akaambiwa apumzike wiki tu. Usikremu mambo yetu ya kizamani bwana.
hapo kwenye uzee kweli hujakosea manake kwanza mwenzio sijalea kwa pampers mie, wala wipes nililea kwa kufua nepi toka kiangazi hadi kiangazi na nilianza kufunga nepi baada ya kitovu kukatika manake nilikichunga kama nachunga mbuzi asile maindi ya jirani.........niliambiwa kikimdondokea mbelen hawi tena rijali.
hongereni sana nahisi ningekuwa nazaa sikuhizi ningezaa hata kumi manake hawana tabu ya malezi mama huchoki
Asante Farkhina..wote ni identical twins wa kike