Ukosefu wa ajira unatokana na kusoma fani zisizokuwa na tija

Ukosefu wa ajira unatokana na kusoma fani zisizokuwa na tija

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Tujifunze kusoma fani zinazotuachia ujuzi ili tuweze kujiajiri na pia kutengeneza ajira kwa wengine. Mfano mdogo tu, jaribu kutangaza nafasi ya fundi wa kushona mavazi; inaweza kuchukua wiki, miezi hakuna mtu aliyeomba. Hii inatafsiri, wenye hiyo fani wako bize na mambo yao na hawaitaji kuajiriwa.

Sasa, jaribu kutangaza nafasi za afisa rasilimali watu, wachumi, wahasibu, wanatakwimu, wagavi, ustawi wa jamii, wanasheria, waalimu n.k utashangaa ndani ya muda mfupi watu zaidi hata ya 1000 hata wenye PhD wataomba, ingawa nafasi ni moja tu; hii inatafsiri elimu waliyoipata haijawawezesha kujikomboa.

Kinachotakiwa ni jitihada binafsi, kujifunza kitu kitakachokutambulisha wewe ni nani, na una uwezo upi wa kujitengenezea ajira pamoja na kutengeneza ajiri kwa wengine.

Bado hatujachelewa, muda ni sasa.
 
Kwahiyo wote tukiwa mafundi cherehani nani atamshonea nguo mwenzie
Tafuta 'technical knowledge' ndio pointi kuu; wanaohangaika sana kwenye ajira wengi wao wana 'knowledge' ambayo ni 'universal' yaani kila mtu anaweza kufanya, awe amesoma hajasoma anaweza kufanya kama akielekezwa kwa siku mbili tu. Mfano, labda umesoma uchumi, na mwingine akasoma mambo ya 'software development' , nadhani hapo mkuu umeona utofauti.
 
Ukosefu wa ajira unatokana na katiba mbovu, utawala mbovu, ukosefu wa Tume huru ya uchaguzi, sera mbovu za maendeleo, ukosefu wa uongozi bali uwepo wa utawala, viongozi wasio na competent wala utashi, uwepo wa matabaka ya kilazima kati ya watawala na watawaliwa, uchu wa madaraka
 
Tujifunze kusoma fani zinazotuachia ujuzi ili tuweze kujiajiri na pia kutengeneza ajira kwa wengine. Mfano mdogo tu, jaribu kutangaza nafasi ya fundi wa kushona mavazi; inaweza kuchukua wiki, miezi hakuna mtu aliyeomba. Hii inatafsiri, wenye hiyo fani wako bize na mambo yao na hawaitaji kuajiriwa.
[emoji23][emoji23]Hatuwezi wote tukawa local fundi,nasoma nikipendacho kazi ikipatikana freshi isipopatikana freshi
 
Ukosefu wa ajira unatokana na katiba mbovu, utawala mbovu, ukosefu wa Tume huru ya uchaguzi, sera mbovu za maendeleo, ukosefu wa uongozi bali uwepo wa utawala, viongozi wasio na competent wala utashi, uwepo wa matabaka ya kilazima kati ya watawala na watawaliwa, uchu wa madaraka
Katiba inaathiri vipi utaalamu wako wa upasuaji wa moyo?
 
Back
Top Bottom