Ukraine: Simu za mkononi chanzo cha vifo vya wanajeshi 89 wa Urusi!

Ukraine: Simu za mkononi chanzo cha vifo vya wanajeshi 89 wa Urusi!

Raphael Thedomiri

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2019
Posts
442
Reaction score
729
Urusi imesema idadi ya vifo vya wanajeshi wake kufuatia shambulizi la Ukraine kwenye mkesha wa Mwaka Mpya katika eneo la Makiivka imepanda hadi 89.

Moscow imesema mapema leo kuwa miili zaidi ilipatikana kwenye vifusi katika mji wa Makiivka ulioko mkoa wa mashariki wa Donetsk unaodhibitiwa na Urusi.

Wizara ya Ulinzi imesema mkasa huo ulitokea kwa sababu askari wa Urusi walitumia simu za mkononi, na hivyo kufichua mahala walikokuwa kwa wanajeshi wa Ukraine.

Urusi ilisema Jumatatu kuwa wanajeshi wake 63 waliuawa, ikiwa ndio idadi kubwa kabisa ya vifo kutokana na shambulizi moja tangu kuanza kwa vita vyake Februari mwaka jana.

Ukraine iliishambulia kambi ya muda ya Urusi katika mji wa Makiivka Januari mosi usiku wa manane kwa kutumia mifumo ya makombora ya HIMARS yanayotolewa na Marekani.

Ukraine inasema idadi ya vifo huenda ni kubwa zaidi kuliko inavyoripotiwa.

Dw
 
Hiki kichapo kimewaacha warusi wote midomo wazi..,Kuna mashambulizi kadhaa ya drones na makombora yaliyofanywa na urusi dhidi ya Ukraine usiku huo wa mwaka mpya lakini ni kama hayajapewa airtime yoyote

Kweli hili lilikuwa pigo takatifu[emoji28]

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
... zile drones 39 za msaada kutoka kwa waajemi zilizotumwa na Supa Pawa mwenye kila aina ya silaha na mifumo "bora" ya kivita duniani kwenda kuua wenye haki wa Ukraine zilipasuliwa kule kule angani na hakuna hata moja iliyo-hit popote ardhini zaidi ya kuleta uchafuzi wa mazingira (debris).
 
Bado watakubali tu,wanajeshi waliokufa ni zaidi ya 400,Superpower wa mchongo anafundishwa vita.

Kwani walikuwa hawajui kwamba hawapaswi kutumia simu?
Tuseme wamekufa 400 Sasa wewe hiyo inakuongezea Nini?! Yaani unafurahia vifo vya binadamu wenzio?! Mimi ni Pro-Russia lakini sijawahi kufurahia vifo vya Askari wa Ukraine wala Russia..Hao Askari wanna Ndugu na familia...tuseme wewe una Ndugu ambaye ni Askari Yuko vitani na anafariki, je utajisikiaje Kama watu wataanza kufurahia kifo Cha huyo Askari na hata kuweka maiti yake mitandaoni ?!
 
Tuseme wamekufa 400 Sasa wewe hiyo inakuongezea Nini?! Yaani unafurahia vifo vya binadamu wenzio?! Mimi ni Pro-Russia lakini sijawahi kufurahia vifo vya Askari wa Ukraine wala Russia..Hao Askari wanna Ndugu na familia...tuseme wewe una Ndugu ambaye ni Askari Yuko vitani na anafariki, je utajisikiaje Kama watu wataanza kufurahia kifo Cha huyo Askari na hata kuweka maiti yake mitandaoni ?!
... hakuna mwenye akili timamu atakayefurahia hata kifo kimoja cha askari wa Ukraine wanaolinda nchi yao, utaifa wao, na watu wao. Kinyume chake, ni asiyekuwa na akili timamu pekee ndiye ambaye hatafurahia mamia ya vifo vya askari wavamizi wanaoua watoto, wanawake, na wazee wa Ukraine wasio na hatia.

Kwa kifo kimoja cha askari wa kirusi maisha ya makumi ya raia wasiokuwa na hatia yanakuwa yameokolewa. Mungu awabariki wanaotekeleza kazi hii njema kwa gharama ya maisha yao na awalaani warusi mara elfu! T14 Armata, Proved, kp kipanya44, Frank Wanjiru, MK254, et. al.
 
Binadamu wenzio wameenda kufanya nini katika nchi ya watu?? Wavamizi sio watu wa kuonewa huruma
Tuseme wamekufa 400 Sasa wewe hiyo inakuongezea Nini?! Yaani unafurahia vifo vya binadamu wenzio?! Mimi ni Pro-Russia lakini sijawahi kufurahia vifo vya Askari wa Ukraine wala Russia..Hao Askari wanna Ndugu na familia...tuseme wewe una Ndugu ambaye ni Askari Yuko vitani na anafariki, je utajisikiaje Kama watu wataanza kufurahia kifo Cha huyo Askari na hata kuweka maiti yake mitandaoni ?!
 
... hakuna mwenye akili timamu atakayefurahia hata kifo kimoja cha askari wa Ukraine wanaolinda nchi yao, utaifa wao, na watu wao. Kinyume chake, ni asiyekuwa na akili timamu pekee ndiye ambaye hatafurahia mamia ya vifo vya askari wavamizi wanaoua watoto, wanawake, na wazee wa Ukraine wasio na hatia.

Kwa kifo kimoja cha askari wa kirusi maisha ya makumi ya raia wasiokuwa na hatia yanakuwa yameokolewa. Mungu awabariki wanaotekeleza kazi hii njema kwa gharama ya maisha yao na awalaani warusi mara elfu! T14 Armata, Proved, kp kipanya44, Frank Wanjiru, MK254, et. al.
.., kabla ya hii vita , viongozi wote wakubwa walikuwa wakipishana mascow wakimsihi na kumpigia magoti Putin aachane na mipango yake ya kuanzisha vita, lakini yeye akajiona ana akili sana kuliko hao viongozi wote..,mtu kama huyo unaanzaje kuwa na huruma Kwa askari wake wanaouwawa?

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
.., kabla ya hii vita , viongozi wote wakubwa walikuwa wakipishana mascow wakimsihi na kumpigia magoti Putin aachane na mipango yake ya kuanzisha vita, lakini yeye akajiona ana akili sana kuliko hao viongozi wote..,mtu kama huyo unaanzaje kuwa na huruma Kwa askari wake wanaouwawa?

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
... dunia nzima ilimsihi lakini akashupaza shingo! Tutafurahia vifo vya wavamizi (walioshupaza shingo) na kuomboleza pamoja nao wanaouwawa kwenye ardhi yao na wavamizi hao.
 
Back
Top Bottom