Ukraine yakubaliana na Marekani kuhusu mpango wa Madini, asema afisa wa Ukraine

Ukraine yakubaliana na Marekani kuhusu mpango wa Madini, asema afisa wa Ukraine

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593

Tukiona DRC kajisalimisha kwa USA ili asaidiwe kuwaondoa M23 tusishangae! Je, Putin atakuwa ameingiwa ubaridi sasa?

Habari kamili;

Ukraine imekubali masharti ya mkataba mkuu wa madini na Marekani, afisa mkuu wa Kyiv ameiambia BBC. "Kwakweli tumekubaliana na marekebisho kadhaa mazuri na tunaona kama matokeo ni chanya," afisa huyo alisema, bila kutoa maelezo zaidi.

Ripoti za vyombo vya habari zinasema Washington imepunguza madai ya awali ya haki ya $500bn (£395bn) katika mapato yanayoweza kutokana na kutumia maliasili lakini haijatoa hakikisho dhabiti la usalama kwa Ukraine iliyokumbwa na vita ambalo ni hitaji kuu la Ukraine.

Bila kuthibitisha kuwa makubaliano yamefikiwa, Trump alisema Jumanne kwamba kwa malipo ya makubaliano hayo Ukraine itapata "haki ya kupigania".

Rais wa Marekani Donald Trump alisema anamtarajia mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky mjini Washington kutia saini mkataba huo wiki hii, baada ya viongozi hao wawili kurushiana maneno makali.

"Wao ni wajasiri sana," aliwaambia waandishi wa habari, lakini "bila Marekani na pesa zake na zana zake za kijeshi, vita hivi vingekuwa vimeisha kwa muda mfupi sana".

Alipoulizwa kama usambazaji wa vifaa vya Marekani na risasi kwa Ukraine utaendelea, alisema: "Labda hadi tutakapokuwa na mpango na Urusi... Tunahitaji kuwa na makubaliano, vinginevyo yataendelea."

Chanzo; BBC Swahili
 
US hana rafiki au adui wa kudumu, yy anachojali maslahi mapana ya nchi yake.
 
Ni muda sasa wa Marekani na Urusi kuanza kufakamia madini na mafuta ya Ukraine

Zele ni mwendawazimu sana huku kote asingefika kama tu asingeiletea ujinga Urusi

Kawauza wananchi wake na utajiri wa taifa lao
 
Back
Top Bottom