Ukweli kuhusu hali ya Mabenki Tanzania.

Ukweli kuhusu hali ya Mabenki Tanzania.

Wana bodi,

Kumekuwa na taarifa mbalimbali kutoka vyanzo tofauti, nyingi zikipendekeza kuwa hali ya mabenki ni mbaya, ya kutia mashaka, na kuonesha dalili ya mabenki kufilisika. Nimeamua kuandika machache na kwa ufupi, kutokana na uchunguzi na tathmini ya kitaalamu. Sababu za kuandika ni mbili. Moja, kwa kuwa uchumi na hasa sekta ya fedha ni eneo langu la taaluma, na nitakuwa sitawatendei haki watanzania kama sitasema neno. Pili, mabenki na sekta ya fedha ni moyo wa uchumi. Midororo na misukosuko mingi katika historia ya chumi za dunia, mara nyingi huanzia katika sekta ya fedha. Naomba kusema kwa ufupi, kwa hoja tatu.

Hoja ya Kwanza: kumekuwa na tatizo ambalo ni la kawaida katika sekta ya fedha la kutolipa madeni wadaiwa. Benki nyingi, na hasa CRDB imekuwa na tatizo hilo. Kwa utaratibu wa kawaida, mabenki hukisia uwezekano wa kutolipwa na kuweka pembeni uwekezano huo (provision), na wakati mwingine kufanya juhudi za kuweka mikakati ya kuyakusanya (restructuring) kihasibu na kisera. Inaposhindikana, mabenki hutambua kuwa haitalipwa na kuweka kama gharama (expensing loans write offs). Hii hupunguza faida. Kwa CRDB imekuwa na athari kubwa, na pengine hutokea mabenki yakafanya hivi kwa pamoja au kwa namna ya msimu, na hivyo hili limetokea katika robo ya tatu ya mwaka 2016. Takwimu zinaonesha kuwa katika trilioni 16.7 zilizokopeshwa, kuna uwezekana wa trilioni 1.43 kutolipwa (non-performing loans) (asilimia 8.6). Kiwango hiki kwa Tanzania ni cha kawaida, tena cha chini kuliko nchi nyingi za kusini mwa Sahara ambazo viwango vyao hufika hadi asilimia zaidi ya 20.

Hoja ya Pili: Kulikuwa na kutoelewana kati ya mabenki na serikali kuhusu kodi ya mapato yatokanayo na mikopo ya benki. Mabenki mengine yalifungua kesi dhidi ya TRA. Lakini katika mwaka 2016 mfano, CRDB walishindwa kesi na hivyo wakatakiwa kulipa kodi hiyo, ambayo ilijumuisha pia kodi ya vipindi vya nyuma (retrospective). Benki nyingi ziliona matumaini ni machache, itawalazimu kulipa kodi hiyo ya serikali. Kwa hiyo muhula wa tatu wa mwaka 2016, mabenki mengi yakatambua kodi hiyo kama gharama. Na ndio maana faida katika mabenki mengi na sekta ilishuka kwa kasi sana, ukizingatia hoja ya kwanza na hoja hii ya pili.

Hoja ya Tatu: Wengi wamehusianisha hasara hii na tatizo la mtaji katika benki ya Twiga. Ukweli ni kuwa, uhusiano ni mdogo sana. Kilichotokea benki ya Twiga, ni kuwa wamekuwa na tatizo la mtaji kwa muda mrefu, wa karibu miaka kumi. Wakaomba serikali aliye mmiliki aongeze mtaji, hilo halikufanyika. Kwa sababu serikali ni mmiliki, benki ikaendelea kuendeshwa bila mtaji wa kutosha. Pamoja na tatizo la mikopo kwa kiasi fulani, hali ikawa mbaya hadi hapo Benki Kuu walipoamua kuchukua dhamana ya benki. Jambo jema linalokuja, ni kuwa wawekezaji binafsi wamekaribishwa kuingiza mtaji, na hadi ninapoandika, Mohammed Dewji na Exim Bank ya China wana nafasi kubwa ya kushinda tenda hiyo.

Nimesikitishwa na upotoshaji unaofanywa, tena na wataalamu. Wakizungumzia kuwa kuna ukasi wa mtitiriko wa fedha (liquidity) katika sekta ya fedha kutokana na serikali kutoa fedha zake na kuziweka benki kuu. Ukweli ni kuwa serikali ilitoa shilingi bilioni 515, wakati liquidity ya mabenki yote kwa takwimu za Disemba 2015, ni bilioni 9,004. Kiasi kilichotolewa ni asilimia 5.7 pekee ya ujazo wa fedha. Na fedha hizi mabenki yanaweza kuzikopa kutoka benki kuu. Kwa tathmini yangu, viashiria vyote ya msingi (fundamentals) vya sekta ya fedha kama mtaji, ujazo wa fedha, ubora wa dhamana, faida na ubora wa uongozi wa mabenki (CAMEL) vipo katika viwango vinavyokubalika (prudential limits). Na mwisho, tathmini yangu inaonesha kuwa mwisho wa mwaka 2016, robo ya nne, mabenki mengi na kwa ujumla wake, yatarekodi faida.


Genuine Martin (Economics PhD Candidate, Northern Illinois University, USA)
Asante, tuje tukope sasa hivi hamjasimamisha mikopo?
 
Wana bodi,

Kumekuwa na taarifa mbalimbali kutoka vyanzo tofauti, nyingi zikipendekeza kuwa hali ya mabenki ni mbaya, ya kutia mashaka, na kuonesha dalili ya mabenki kufilisika. Nimeamua kuandika machache na kwa ufupi, kutokana na uchunguzi na tathmini ya kitaalamu. Sababu za kuandika ni mbili. Moja, kwa kuwa uchumi na hasa sekta ya fedha ni eneo langu la taaluma, na nitakuwa sitawatendei haki watanzania kama sitasema neno. Pili, mabenki na sekta ya fedha ni moyo wa uchumi. Midororo na misukosuko mingi katika historia ya chumi za dunia, mara nyingi huanzia katika sekta ya fedha. Naomba kusema kwa ufupi, kwa hoja tatu.

Hoja ya Kwanza: kumekuwa na tatizo ambalo ni la kawaida katika sekta ya fedha la kutolipa madeni wadaiwa. Benki nyingi, na hasa CRDB imekuwa na tatizo hilo. Kwa utaratibu wa kawaida, mabenki hukisia uwezekano wa kutolipwa na kuweka pembeni uwekezano huo (provision), na wakati mwingine kufanya juhudi za kuweka mikakati ya kuyakusanya (restructuring) kihasibu na kisera. Inaposhindikana, mabenki hutambua kuwa haitalipwa na kuweka kama gharama (expensing loans write offs). Hii hupunguza faida. Kwa CRDB imekuwa na athari kubwa, na pengine hutokea mabenki yakafanya hivi kwa pamoja au kwa namna ya msimu, na hivyo hili limetokea katika robo ya tatu ya mwaka 2016. Takwimu zinaonesha kuwa katika trilioni 16.7 zilizokopeshwa, kuna uwezekana wa trilioni 1.43 kutolipwa (non-performing loans) (asilimia 8.6). Kiwango hiki kwa Tanzania ni cha kawaida, tena cha chini kuliko nchi nyingi za kusini mwa Sahara ambazo viwango vyao hufika hadi asilimia zaidi ya 20.

Hoja ya Pili: Kulikuwa na kutoelewana kati ya mabenki na serikali kuhusu kodi ya mapato yatokanayo na mikopo ya benki. Mabenki mengine yalifungua kesi dhidi ya TRA. Lakini katika mwaka 2016 mfano, CRDB walishindwa kesi na hivyo wakatakiwa kulipa kodi hiyo, ambayo ilijumuisha pia kodi ya vipindi vya nyuma (retrospective). Benki nyingi ziliona matumaini ni machache, itawalazimu kulipa kodi hiyo ya serikali. Kwa hiyo muhula wa tatu wa mwaka 2016, mabenki mengi yakatambua kodi hiyo kama gharama. Na ndio maana faida katika mabenki mengi na sekta ilishuka kwa kasi sana, ukizingatia hoja ya kwanza na hoja hii ya pili.

Hoja ya Tatu: Wengi wamehusianisha hasara hii na tatizo la mtaji katika benki ya Twiga. Ukweli ni kuwa, uhusiano ni mdogo sana. Kilichotokea benki ya Twiga, ni kuwa wamekuwa na tatizo la mtaji kwa muda mrefu, wa karibu miaka kumi. Wakaomba serikali aliye mmiliki aongeze mtaji, hilo halikufanyika. Kwa sababu serikali ni mmiliki, benki ikaendelea kuendeshwa bila mtaji wa kutosha. Pamoja na tatizo la mikopo kwa kiasi fulani, hali ikawa mbaya hadi hapo Benki Kuu walipoamua kuchukua dhamana ya benki. Jambo jema linalokuja, ni kuwa wawekezaji binafsi wamekaribishwa kuingiza mtaji, na hadi ninapoandika, Mohammed Dewji na Exim Bank ya China wana nafasi kubwa ya kushinda tenda hiyo.

Nimesikitishwa na upotoshaji unaofanywa, tena na wataalamu. Wakizungumzia kuwa kuna ukasi wa mtitiriko wa fedha (liquidity) katika sekta ya fedha kutokana na serikali kutoa fedha zake na kuziweka benki kuu. Ukweli ni kuwa serikali ilitoa shilingi bilioni 515, wakati liquidity ya mabenki yote kwa takwimu za Disemba 2015, ni bilioni 9,004. Kiasi kilichotolewa ni asilimia 5.7 pekee ya ujazo wa fedha. Na fedha hizi mabenki yanaweza kuzikopa kutoka benki kuu. Kwa tathmini yangu, viashiria vyote ya msingi (fundamentals) vya sekta ya fedha kama mtaji, ujazo wa fedha, ubora wa dhamana, faida na ubora wa uongozi wa mabenki (CAMEL) vipo katika viwango vinavyokubalika (prudential limits). Na mwisho, tathmini yangu inaonesha kuwa mwisho wa mwaka 2016, robo ya nne, mabenki mengi na kwa ujumla wake, yatarekodi faida.


Genuine Martin (Economics PhD Candidate, Northern Illinois University, USA)
mnajitahidi kucopy faster!!

But ahsante kwa kucopy elimu nzuri ili nasi tupate kujua na kuelewa...
 
ila mbona mabenk hayaji kutuelewesha halafu mwanafunzi wa phd asiye mfanyakazi wa benk yeyote anakuja kutuelewesha? (HAINIINGII)


Mbona maelezeo yake hayaendani na uhalisia? (HAINIINGII)
 
Please Would you come in English vassion?
Angeleta kwa kingereza nina uhakika kuwa wewe ungelalamika kwa nini ametumia lugha hiyo.
Soma mada, uliza, ongezea, pinga kwa kutoa mbadala wa hoja hiyo. Siasa iwe kwenye mambo ya siasa na uchumi ubakie hivyo. kama huna hoja siyo ubaya ukanyamaza kimya
 
Mkuu unazidi kuharibu, kukosea kupo sana masuala ya typo tunaelewa , usijari tunajua ulitaka kumaanisha nini.
Naelewa unachomaanisha, nimemnukuu aliyesema nilichonukuu ili pawe na mazingira chekeshi.
Najua unajua kuwa hizi keyboard app. nyingine zina kiherehere sana cha kumalizia maneno.
 
Wana bodi,

Kumekuwa na taarifa mbalimbali kutoka vyanzo tofauti, nyingi zikipendekeza kuwa hali ya mabenki ni mbaya, ya kutia mashaka, na kuonesha dalili ya mabenki kufilisika. Nimeamua kuandika machache na kwa ufupi, kutokana na uchunguzi na tathmini ya kitaalamu. Sababu za kuandika ni mbili. Moja, kwa kuwa uchumi na hasa sekta ya fedha ni eneo langu la taaluma, na nitakuwa sitawatendei haki watanzania kama sitasema neno. Pili, mabenki na sekta ya fedha ni moyo wa uchumi. Midororo na misukosuko mingi katika historia ya chumi za dunia, mara nyingi huanzia katika sekta ya fedha. Naomba kusema kwa ufupi, kwa hoja tatu.

Hoja ya Kwanza: kumekuwa na tatizo ambalo ni la kawaida katika sekta ya fedha la kutolipa madeni wadaiwa. Benki nyingi, na hasa CRDB imekuwa na tatizo hilo. Kwa utaratibu wa kawaida, mabenki hukisia uwezekano wa kutolipwa na kuweka pembeni uwekezano huo (provision), na wakati mwingine kufanya juhudi za kuweka mikakati ya kuyakusanya (restructuring) kihasibu na kisera. Inaposhindikana, mabenki hutambua kuwa haitalipwa na kuweka kama gharama (expensing loans write offs). Hii hupunguza faida. Kwa CRDB imekuwa na athari kubwa, na pengine hutokea mabenki yakafanya hivi kwa pamoja au kwa namna ya msimu, na hivyo hili limetokea katika robo ya tatu ya mwaka 2016. Takwimu zinaonesha kuwa katika trilioni 16.7 zilizokopeshwa, kuna uwezekana wa trilioni 1.43 kutolipwa (non-performing loans) (asilimia 8.6). Kiwango hiki kwa Tanzania ni cha kawaida, tena cha chini kuliko nchi nyingi za kusini mwa Sahara ambazo viwango vyao hufika hadi asilimia zaidi ya 20.

Hoja ya Pili: Kulikuwa na kutoelewana kati ya mabenki na serikali kuhusu kodi ya mapato yatokanayo na mikopo ya benki. Mabenki mengine yalifungua kesi dhidi ya TRA. Lakini katika mwaka 2016 mfano, CRDB walishindwa kesi na hivyo wakatakiwa kulipa kodi hiyo, ambayo ilijumuisha pia kodi ya vipindi vya nyuma (retrospective). Benki nyingi ziliona matumaini ni machache, itawalazimu kulipa kodi hiyo ya serikali. Kwa hiyo muhula wa tatu wa mwaka 2016, mabenki mengi yakatambua kodi hiyo kama gharama. Na ndio maana faida katika mabenki mengi na sekta ilishuka kwa kasi sana, ukizingatia hoja ya kwanza na hoja hii ya pili.

Hoja ya Tatu: Wengi wamehusianisha hasara hii na tatizo la mtaji katika benki ya Twiga. Ukweli ni kuwa, uhusiano ni mdogo sana. Kilichotokea benki ya Twiga, ni kuwa wamekuwa na tatizo la mtaji kwa muda mrefu, wa karibu miaka kumi. Wakaomba serikali aliye mmiliki aongeze mtaji, hilo halikufanyika. Kwa sababu serikali ni mmiliki, benki ikaendelea kuendeshwa bila mtaji wa kutosha. Pamoja na tatizo la mikopo kwa kiasi fulani, hali ikawa mbaya hadi hapo Benki Kuu walipoamua kuchukua dhamana ya benki. Jambo jema linalokuja, ni kuwa wawekezaji binafsi wamekaribishwa kuingiza mtaji, na hadi ninapoandika, Mohammed Dewji na Exim Bank ya China wana nafasi kubwa ya kushinda tenda hiyo.

Nimesikitishwa na upotoshaji unaofanywa, tena na wataalamu. Wakizungumzia kuwa kuna ukasi wa mtitiriko wa fedha (liquidity) katika sekta ya fedha kutokana na serikali kutoa fedha zake na kuziweka benki kuu. Ukweli ni kuwa serikali ilitoa shilingi bilioni 515, wakati liquidity ya mabenki yote kwa takwimu za Disemba 2015, ni bilioni 9,004. Kiasi kilichotolewa ni asilimia 5.7 pekee ya ujazo wa fedha. Na fedha hizi mabenki yanaweza kuzikopa kutoka benki kuu. Kwa tathmini yangu, viashiria vyote ya msingi (fundamentals) vya sekta ya fedha kama mtaji, ujazo wa fedha, ubora wa dhamana, faida na ubora wa uongozi wa mabenki (CAMEL) vipo katika viwango vinavyokubalika (prudential limits). Na mwisho, tathmini yangu inaonesha kuwa mwisho wa mwaka 2016, robo ya nne, mabenki mengi na kwa ujumla wake, yatarekodi faida.


Genuine Martin (Economics PhD Candidate, Northern Illinois University, USA)
Haya nyumbu kata funua ingieni ulingoni kupinga bila hoja bali vihoja
 
Jamani mimi nimebahatika kuishi na huyu jamaa Pugu secondary kiukweli jamaa anajua uchumi. Kiufupi jamaa now ni mwalimu University of Dar es salaam na alipata div 1 point 7 form four na kuwa Tanzania 2, form six alipata div 1 point 4 huku economics akiongoza kitaifa. Nilivyoliona bandiko lake humu nimelisoma kwa makini maana namjua kwa hiyo kama kumponda pondeni lakini jueni huyu ni mtaalamu kweli wa uchumi.
Big up waziri mkuu wa zamani wa Pugu boys
Atakuja mtu anaitwa Malisa aliyesoma chuo cha wajinga na wapuuzi SAUT aanze kuponda na kukosoa.. Alafu jitu lenyewe lilisoma sociology sijui..

Na yule Nyerere wala elimu yake haieleweki atakuja kuponda pia
 
English vassion?? Maskinii mnatia huruma nyie bawacha
"Vassion" ni kwa lugha ya kifaransa yenye maana hiyo hiyo ya "version" (unayoifahamu pekee)

Niliamini kuwa ungeficha kutokujua kwako.
 
Mi ninaomba kueleweshwa na mtoa mada kwenye kipengele cha Liquidity- kama serikali ilitoa billioni 515 na mabenki yote yakabakiwa na billioni 9004 tena kwa takwimu za mwaka Jana, Je ili uanzishe benki inatakiwa uwe na mtaji wa sh ngapi? Pia Tanzania ina benki ngapi ili tuone mgawo huu utakuwa kiasi gani kwa hizo Benki?
 
"Vassion" ni kwa lugha ya kifaransa yenye maana hiyo hiyo ya "version" (unayoifahamu pekee)

Niliamini kuwa ungeficha kutokujua kwako.
Hapa kinazungumzwa kifaransa wewe mbweha
 
Back
Top Bottom