Ukweli kuhusu NIDA: Tuwe makini na habari za uzushi kuhusu mchakato wa vitambulisho NIDA

Ukweli kuhusu NIDA: Tuwe makini na habari za uzushi kuhusu mchakato wa vitambulisho NIDA

mjasiriamali mdogo

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2013
Posts
258
Reaction score
110
Habari waungwana. Leo ngoja nieleze mchakato wangu wa kitambulisho changu cha taifa mpaka kupata namba na niliyoyashuhudia ofisi za NIDA.

1. Kabla sijaanza kufatilia kitambulisho cha taifa, nilianza kuuluzia nyaraka zipi zinahitajika kaambatanishwa.
Nikaambiwa cheti cha kuzaliwa,(kadi ya mpiga kura, leseni ya udereva, O au A level living certificate) n.k barua ya mtendaji. Nakala ya utambulisho wowote wa wazazi (mmoja au wote)

2. Baada ya kugundua viambatanisho vinavyohitajika na kuambiwa kuwa cheti cha kuzaliwa ni cha lazima kuliko vitu vyote hapo juu. Nakaenda RITA makao makuu posta kujiandikisha kupata cheti cha kuzaliwa, nikalipa 20000 nakaambiwa baada ya siku 14 kitakuwa tayari.

3. Baada ya siku 14 (10.9.2019) mapema sana nikaenda RITA nikiwa na fomu ya NIDA imejazwa na kupigwa mhuri wa mtendaji, barua ya mtendaji, kopi ya mpiga kura, viambatanisho vya wazazi wangu wote 2 nikakuta cheti kipo tayari, nikachukua nikaenda moja kwa moja ofisi za NIDA wilaya ya Temeke.

4. Nilikuta watu wengi sana pale ilikuwa mida ya saa 6 mchana, nikauliza taratibu zipoje hapa, wakanijibu tulia tu atakuja hapa nje na kukusanya fomu, halafu mmoja mmoja atakuwa anaitwa ndani, kweli fomu zikachukulia na baada ya muda mmojammoja anaitwa na kuulizwa madogo madogo, hususani kama fomu na nyaraka zako zina kasoro, mimi niulizwa umezaliwa wapi na lini kiuzushi tu.

Saa 10 jioni nikafanikiwa kupiga picha nakuondoka. Kabla sijaondoka nikauliza lini kitakuwa tayari, nikiambiwa baada ya miezi 2 namba itakuwa tayari sio kadi.

4. Baada ya mwezi mmoja na nusu hivi nikjaribu kwa njia ya mtandao nikapata namba. Nikawapigia simu NIDA waniambie lini kitambulisho kitakuwa tayari niende kuchukua, wakaniambia kuanzia mwezi wa 2 au 3 mwaka huu.

WENGI WANAOLALAMIKA KUHUSU NIDA WANAKUWA WANA MAPUNGUFU KWENYE NYARAKA ZAO HASA VIAMBATANISHO CHETI CHA KUZALIWA NA UTAMBULISHO WA WAZAZI. SIKU MOJA TU NILIMALIZA MCHAKATO MZIMA.
 
Mimi nilipomaliza kupitisha form kote mpaka uhamiaji kasheshe ikaanza NIDA

1. Nilifika ofisin kwao saa 6 mchana wakasema hawapokei form yangu niende siku inayofuata saa 12 alfajiri.
2. Saa 12 alfajiri siku ya pili nilipofika wakasema form watazipokea saa 2 asbh kwa hiyo tusubiri
3. Ilipofika saa 2 asbh wakapokea form nilikua nimetoka kwenda kutafuta chai mie nikafika saa 2.30 wakasema hawapokei form mpaka kesho tena saa 12 asbh
4. Kesho saa 12 asbh nikajihimu tena kufika pale tukaambiwa tumpe form mlinzi then saa 2 tutaitwa kupiga picha
5. Saa 2 tukaitwa tukakaa foleni saa 5 nikapigwa picha nikaambiwa namba yangu itatoka baada ya wiki 3.
6. Mpaka sasa ni wiki ya pili na siku 4 bado sijapata namba ya NIDA
 
mjasiriamali mdogo,

Mbona sie wengine hatukuyapitia hayo?

Walipotangaza wanatoa vitambulisho, tuliambiwa NIDA wamekuja kw ofisi ya serikli, ya mtaa, tukaenda tukapewa form tukajaza na kurudisha na viambatanisho muhimu ni cheti cha kuzaliwa(namba yake waijaza kwenye cheti pia) baada yltukapigwa picha na kuchukukiwa alama z vidole. Baada ya ya muda majina yakarudi kwa ofisi ya serikali ya mtaa tuhakiki tukahakiki, baada ya muda tukajulishwa tukachukuwe vitambulisho vyetu hapo serikali ya mtaa.

Hakukuwa na usunbufu wowote.
 
MbonA sie wengine hatukuyapitia hayo?

Walipotangaza wanatoa vitambulisho, tuliambiwa NIDA wamekuja kw ofisi ya serikli, ya mtaa, tukaenda tukapewa form tukajaza na kurudisha na viambatanisho muhimu ni cheti cha kuzaliwa(namba yake waijaza kwenye cheti pia) baada yltukapigwa picha na kuchukukiwa alama z vidole. Baada ya ya muda majina yakarudi kwa ofisi ya serikali ya mtaa tuhakiki tukahakiki, baada ya muda tukajulishwa tukachukuwe vitambulisho vyetu hapo serikali ya mtaa.

Hakukuw na usunbufu wowote.
Huu ulikuwa mchakato wa mwanzo ambao ulikuwa unafanyika ofisi za mtaa, ulikuwa rahisi sana. Mchakato wa sawa nitofauti kabsa unasimamiwa na NIDA kwenye ofisi zao tu
 
Huu ulikuwa mchakato wa mwanzo ambao ulikuwa unafanyika ofisi za mtaa, ulikuwa rahisi sana. Mchakato wa sawa nitofauti kabsa unasimamiwa na NIDA kwenye ofisi zao tu

Yes, kwa kuwa watu hawakwenda na wakati wito ulipotolewa.
 
kabila01, Wengine uko NIDA cheti cha kuzaliwa kimeandikwa kwa majina ya HAJI YANGA MANARA, vyeti vingine na majina yake NIDA yameandikwa kwa majina ya HAJJI YANGA MANARA!

Hapo baadhi ya watu watawalaumu NIDA, eti wanawasumbua!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine uko NIDA cheti cha kuzaliwa kimeandikwa kwa majina ya HAJI YANGA MANARA, vyeti vingine na majina yake NIDA yameandikwa kwa majina ya HAJJI YANGA MANARA!

Hapo baadhi ya watu watawalaumu NIDA, eti wanawasumbua!

Sent using Jamii Forums mobile app
Unataka kusema NIDA wanafanya kazi kwa mfumo wa roboti?

Yaani hawawezi kutumia akili zao hata kidogo, ili kupunguza usumbufu kwa wahusika?

Kama ni hivyo basi hatuna sababu ya kuwasomesha watu vyuo, kisha kuwapa semina elekezi na mwishowe waje wafanye kazi kipumbavu hivyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu, Walipotangaza wanatoa vitambulisho, tuliambiwa NIDA wamekuja kw ofisi ya serikli, ya mtaa, tukaenda tukapewa form tukajaza na kurudisha na viambatanisho muhimu ni cheti cha kuzaliwa(namba yake waijaza kwenye cheti pia) baada yltukapigwa picha na kuchukukiwa alama z vidole. Baada ya ya muda majina yakarudi kwa ofisi ya serikali ya mtaa tuhakiki tukahakiki, baada ya muda tukajulishwa tukachukuwe vitambulisho vyetu hapo serikali ya mtaa.
[emoji867]
Huu utaratibu wakupitia serikali za mitaa wangeendeleza ungeleta nafuu kwa watu hasa wa vijijini kuliko hivi huduma kupatikana kwenye ofisi za Nida pekee zilizoko wilayani kuna wengine wanaishi zaid ya kilometer 40 kufuata huduma..garama wanashindwa kuzimudu za nauliza na kisha akifika apangiwe siku nyingine..!@!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutajuaje kama hizi ndio sio habari za uzushi tunazotakiwa kuwa makini nazo ?

Hauwezi ukachukulia kilichokutokea wewe ndio kimewatokea wote....
 
Ni kweli mwanzoni hapakuwa na utata hivyo. Kadiri walivyoendelea kuna matatizo ya ufanganyifu yalijitokeza hasa huko town. Uamuzi ukawa cheti cha kuzaliwa kiwepo.
Kuchelewa kumewagharimu wengi na wanajutia. Poleni wapendwa. Watu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mjasiriamali mdogo,

Hii kasumba ya kila anayefanikiwa hata kama ni kwa magumashi kumuona anayehangaika ni mzembe sijui itaisha lini. Umeeleza vizuri ila mwisho umeharibu, kama kuna mapungufu kwann mtu asiambiwe palepale ikibidi aelimishwe juu ya alipokosea ili aanze mchakato kuliko kumpiga kalenda? Nachelea kusema, kuna mengi ulifanya ila hujayaandika hapa. Mimi mpaka sasa nimeshaachana na mambo ya kutafuta namba maan usumbufu nilioupata sio wa nchi hii. Fikiria mmepanga folenj halafu kuna mjinga mmoja yupo mlangoni (kwakushirikiana na maafisa wa nida) anawaambia kama unataka kupiga picha leta elfu tano bila aibu. Sio kwamba sina uwezo isipokuwa niliona ni ujinga wa kiwango cha juu kuchomwa jua halafu bado nilipie. Voda wananidai songesha, mpawa, na salio la kawaida. Branch wananidai tala ndio usiseme. Wazifunge tu halafu mtu anifuate kwangu anataka hela.
 
Kama kwetu tu, mi nilitumia nusu saa kukamilisha kujiandikisha kupata kitambulisho cha NIDA, wahenga sisi hatuulizwi cheti cha kuzaliwa, ni kadi ya mpiga kura tu, basi. Ilikuwa kama burudani tu, kwenda kuonana na sura mpya

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwenye kitambulisho uliwekewa namba gani? Kama hauna tarehe ya kuzaliwa haupati kadi, namba zako zinaanza na tarehe ya kuzaliwa.
 
Back
Top Bottom